Pages


Photobucket

Monday, October 15, 2012

UGONJWA WA AJABU WAHARIBU SURA YA KHATANA (HUJAFA HUJAUMBIKA)

                                      BW.KHATANA  (MUONEKANO WA SURA YAKE)

Mkazi wa  kashmir,nchini India ,Mohammad Latif Khatana (Pichani) Amejitokeza  hadharani  kwa mara ya kwanza  na kuzungumza juu ya ugonjwa wa ajabu unaomsumbua , ambao umeziba kabisa sura yake. kutokana na ugonjwa huo Khatana mwenye umri wa  miaka 32  sasa hana uwezo wa kuona ,wala kufanya kazi  pamoja na kuwa katika hali hiyo Khatana  amepata mke ambaye ana mimba ya miezi saba ingawa bwana huyo anayo hofu juu ya mtoto wake kuweza kupata ugonjwa huo.
"Nasubiri kuwa baba na kuwa  na furaha kama wanaume wengine ,lakini  nakuwa mwoga  siku baada ya siku  na ninamuomba  Mungu mtoto wangu asifanane na mimi.alisema Khatana.
Latif ,anaishi katika Milima ya Tuli Bana  katikati ya  jammu na kashmir na mke wake salima  mwenye umri wa miaka 25 ,husafiri kwa muda wa miezi minne kila mwaka kwa ajili ya kwenda mjini kuombaomba fedha.
Katika historia yake alizaliwa na  donge dogo juu ya paji la uso lakini liliendelea kukua mpaka kuunda nyamanyama ambazo zimeziba sura yake.Anasema siku zote mama yake  amekuwa akilia.Tangu utoto wake  alikuwa akitengwa na jamii iliyomzunguka.
Akiwa na umri wa miaka minne alipoteza jicho lake moja (la kushoto), na hivyo wenzake walimzomea na kumuita "jicho moja" pamoja  na hayo  mke wake naye ni mlemavu kwani  anao mguu mmoja.Yeye na mke wake huyo  wamekuwa  wakiishi kwa furaha siku zote.
                                             
                                               BW.KHATANA ALIVYO SASA

No comments:

Post a Comment