Pages


Photobucket

Wednesday, October 31, 2012

HAYA NDIO YALIYO MKUTA HAMAD RASHIDI (MB) NDANI YA MASAA 4

Picture
Francis Godwin (kofia nyekundu) akihojiana na Mhe. Hamad huko Iringa jana.



Uhaba  wa mafuta  ya petroli na dizeli ambao  umeendelea  kuukumba mji  wa Iringa kwa  zaidi ya  siku tano  sasa, umeendelea  kuwatesa  wananchi  wa kada mbalimbali ambapo jana, Mbunge  wa  jimbo la Wawi katika  Serikali ya Mapinduzi  ya  Zanzibar, Hamad Rashid Mohamed (CUF) ameonja keor hiyo baada ya kuingia mjini Iringa  na  kujikuta akisota kwa  zaidi ya saa nne katika foleni ya kusubiri kununua mafuta katika  kituo cha kimoja wapo  kilichokuwa  kikiuza mafuta katika eneo la Ipogolo.
Mbunge  Hamad  alikuwa  safarini  kutokea  mkoani Morogoro  akielekea Mafinga  wilaya ya  Mufindi. Mbunge huyo amesema,  "serikali inapaswa  kuangalia  uwezekano  wa  kutatua tatizo hilo la uhaba wa mafuta hapa nchini vinginevyo uchumi  wa nchi utaendelea  kuyumba  zaidi"

Amesema  kuwa kitendo  cha  wananchi  kushinda katika foleni kwa  saa zaidi ya sita  wakisubiri kununua mafuta katika  kituo hicho ni sawa na wananchi hao kupoteza muda wa kuzalisha, hivyo Serikali iliyopo madarakani inapaswa  kushughulikia tatizo hilo ambalo linasababishwa na  waagizaji  wakubwa wa mafuta hapa nchini.

Mbunge huyo alisema  alifika katika  foleni  hiyo majira ya saa 8 mchana na  kufanikiwa  kununua mafuta  saa 12 jioni.

Mbali ya uhaba  huo  wa mafuta, uchunguzi  uliofanywa na Francis Godwin (kutoka
francisgodwinblog )   umebaini  kuwa baadhi ya  vijana  walikuwa  wakishirikiana na wafanyakazi  wa vituo  hivyo vya mafuta kwa  kununua mafuta na kujaza katika mapipa na kupakia katika magari na kwenda kuyauza kwa bei  kubwa  zaidi mjini Iringa.

No comments:

Post a Comment