Pages


Photobucket

Friday, October 19, 2012

WAZIRI MKUU WA TANZANIA KUPITIA SHIRIKA LA UTANGAZAJI BBC, AZITAJA SABABU ZA NCHI YAKE KUTOFANYA VIZURI KATIKA MICHEZO NA BADALA YAKE KUWA WASINDIKIZAJI


Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda
                                     WAZIRI MKUU WA TANZANIA MIZENGO  PINDA

Waziri Mkuu wa Tanzania,Mh Mizengo Pinda Akizungumza na Mtangazaji wa shirika la utangazaji  BBC Bw. Salim Kikeke  jana (18/10/2012) katika vipindi vyao vinavyorushwa  kila siku za jumatatu-ijumaa kuanzia saa 3:00 usiku kupitia kituo cha Television ya Star Tv, Kikeke alitaka kufahamu Kwanini nchi kama Tanzania haifanyi vizuri katika michezo na badala yake kuwa wasindikizaji . 
Akijibu swali hilo Mh Mizengo pinda  alisema:-  
"Lazima tufanye jitihada kubwa kwanza kuahinisha watu wenye  vipaji  hivi mapema  tangu wanapokuwa  kwenye shule hususani  shule za msingi na sekondari  na kuwajenga ,
Tangu zamani tulikuwa na utaratibu huo  ingawa hapa  katikati ndio tukapiga marufuku  mambo ya michezo mashuleni n.k.Nadhani hili  ndilo lililo tuhathiri , Eneo ambalo tulikuwa tunalichukulia  kama chachu  likawa tena halipo, kwa hiyo tukawa tunangoja mpaka itokee  bahati  nasibu kitu ambacho hakiwezekani.
 Ile hali ya kutoruhusu  hali hii  kuendelea ,kwakweli  tulivuruga sana  kitu ambacho  kimetugharimu sana ,sasa tumeanza ikiwa ni pamoja na kuruhusu  michezo mashuleni na michezo yote.
Na sasa  tunayo mashindano kila mwaka  ikiwa sasa ni kujaribu kuona  ni nani wanaoweza na wenye vipaji  wakiwa wadogo  ili tuweze kuwaendeleza kama tulivyo kuwa tuna fanya tangu zamani."


No comments:

Post a Comment