Pages


Photobucket

Monday, October 15, 2012

HUYU NDIO MZEE WA MIAKA 63 ALIYEANZA KUSOMA SHULE YA MSINGI



Mzee  mmoja katika kijiji cha Bundibugyo(Nchini Uganda), Iddi Mulangira(Pichani mkono wa kulia) amezua mshangao mkubwa  kwa wakazi wa kijiji hicho  baada ya kuonekana akisoma katika shule ya Msingi Boma .
Mzee huyo mwenye  umri wa Miaka  63 alisema kuwa ameamua  kuanza  tena mafunzo  tena katika shule hiyo  ili aweze kujifunza somo la kingereza  kwa lengo la kumsaidia katika kusoma nyaraka mbalimbali.
"Nimeamua  kurudi tena darasani ili niweze  kujifunza  somo la kingereza kwa   kuwa najua litanisaidia katika kutafsiri nyaraka  ambazo napewa  ofisini" alisema Mulangira
Aliongeza kuwa anaamini  kurudi  darasani  kutamsaidia  katika kusimamia familia yake  kwa kuwa kusoma kutamwezesha  kuwa  na usimamizi  mzuri wa fedha  na biashara zake .
Mulangira ambaye anafanya kazi ya kubeba mizigo katika  makao makuu  ya wilaya  hiyo alisema  kuwa amefanya kazi  hiyo  kwa muda wa miaka 30, jambo ambalo limemsababisha kuchoshwa na kazi  hiyo ya ubebaji wa mizigo.
"Sipendi  kuendelea na kazi hii ya ubebaji mizigo  ndiyo maana nimeamua   kwenda shule kwa sababu nina imani nikipata elimu naweza  kuwa msimamizi mkuu na mshahara wangu ukaongezeka "alisema .
Alisema kuwa rafiki yake  ambaye  alikuwa akisoma kitabu cha haki za binadamu  alimvutia  na kusababisha  kujiunga  na elimu ya msingi kwa lengo la kupata elimu zaidi .
"Rafiki yangu alikuwa akisoma kitabu cha haki za binadamu  baada ya hapo aliniomba  niandike jina langu,baada ya kushindwa ndipo alinishauri niende nikasome  kwa kuwa ni haki yangu kupata elimu",alisema Murangira.
Aliongeza  kuwalicha ya  kufanikiwa  kusoma katika shule hiyo bado anakumbana na changamoto nyingi ikiwamo kukosa  chakula cha mchana  hali ambayo inamsababisha  kukaa na njaa kwa muda mrefu.
Baada ya kukaa shule kwa miezi minne  mzee huyo  kwa sasa  anaweza kuandika jina lake na kiwango chake cha kusoma na kuandika kimekua.
"Kabla ya kwenda shule nilikuwa najua kusalimia  na baadhi ya  maneno  kidogo kama kikombe,kalamu,lakini sasa nafahamu mambo mengi nawasifu sana walimu wa shule hii ", alisema.

No comments:

Post a Comment