Pages


Photobucket

Saturday, October 20, 2012

KUFUATIA KUZUKA KWA VURUGU ZANZIBAR, ASKOFU WA ANGLICAN ZANZIBAR MICHAEL HENRY HAFIDHI ATOWEKA.


Askofu Michael Henry Hafidhi ( mwenye vazi jekundu)  Askofu wa Anglican zanzibar

Akizungumza na shirika la utangazaji BBC kupitia vipindi vyake vinavyorushwa na kituo  cha Television ya  Star TV (Jana 19/10/2012  saa 3 usiku) Askofu huyo  amesema ameamua kuchukua hatua hiyo  kutokana na vitisho vilivyo tolewa kwake na  kikundi cha Uamsho, kwamba wanahitaji kumkamata  kwa sababu kiongozi wao (FARID) ameshikwa kwa  hiyo kushikwa  kwake kutaishinikiza Serikali iweze kumtoa huyo kiongozi, Hata hivyo Bw.Salim Kikeke (Mtangazaji wa shirika la utangazaji la BBC) alitaka kufahamu  uhakika alio nao Askofu huyo  kwa kuamini vitisho hivyo vinatoka katika kikundi cha uamsho, Askofu huyo alisema ' Tayari  anazo meseji za vitisho (meseji zinazo jitambulisha kuwa wao ni uamsho) katika simu yake ambazo zimetoka katika kundi hilo la uamsho na kuongeza kuwa katika Tovuti yao pia wamebainisha suala hilo  ambapo kundi hilo limebainisha kwamba kama sio yeye basi atakamatwa Askofu SHAYO"
Akisisitiza,Askofu huyo amesema  lengo la  kundi hilo kuwakamata ni kuishinikiza Serikali imuachie kiongozi wao.
Hata hivyo Salim Kikeke alimuuliza Askofu huyo kama tayari amefika katika vyombo vya usalama kufuatia vitisho hivyo.Askofu  huyo alisema " tayari tumetoa taarifa na mpaka sasa vyombo vya usalama vinafahamu suala hilo ambapo vyombo hivyo vimesema vitalishughulikia ,ingawa wamesema niandike maelezo na mimi nikaona maelezo ya nini wakati kila kitu kinaonekana" alisema Askofu huyo.
Askofu huyo alipotakiwa  kueleza sababu   za yeye hasa kwanini anadhani kwamba  Kundi la uamsho lingeweza kumdhuru, alisema   "kikundi cha uamsho  kimekuwa  kikitimiza malengo yake ,mfano kilisema  kitahitisha mkutano wake ,na mkutano huo ulifanyika,hivyo na sisi tunaogopa na kuwa na hofu kubwa  maana uamsho wakifanya kitu wanafanya kweli".Alisema Askofu huyo  na kudai kutopewa ulinzi na jeshi la polisi licha ya  kutoa taarifa hizo katika vyombo vya usalama.
Kwa upande wake mtangazaji wa Shirika la utangazaji la BBC  Bw. Salim Kikeke  alisema  jana alizungumza na jeshi la polisi kupitia kwa  mkurugenzi wa makosa ya jinai DCI Yusuph Ilembo kutoka zanzibar ambalo lilisema halina taarifa yoyote kuhusiana na tukio hilo .

No comments:

Post a Comment