Pages


Photobucket

Friday, January 31, 2014

Chadema kususia Bunge la Katiba

Wakati Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akisema wabunge wa chama chake watasusia vikao vya Bunge Maalumu la Katiba ikiwa hoja ya kuundwa kwa Serikali tatu itapingwa na wabunge wa CCM, Mwakilishi wa Mji Mkongwe (CUF), Ismail Jussa Ladhu ametaka kuvunjwa kwa Muungano.
Akihutubia kwenye Uwanja wa Tubuyu nje kidogo ya Mji wa Morogoro juzi, Mbowe alisema wabunge wa chama chake wataandamana nchi nzima kufikisha ujumbe kwa wananchi kwamba maoni yao yamepingwa na wabunge wa CCM walio wengi.
“Tutawaeleza wananchi kwamba maoni ya CCM ndiyo yameonekana ya maana kuliko ya wananchi ambao ni wengi zaidi,” alisema Mbowe kwenye mkutano huo ambao ni sehemu ya Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko - M4C Pamoja Daima.
Alisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilikusanya maoni na kubaini kuwa asilimia 62 ya Watanzania wanataka Serikali tatu za Tanganyika, Zanzibar na ya Muungano.
“Serikali ya CCM haitaki kusikia maneno Serikali tatu wanasema sera yao ni ya Serikali mbili, wanafanya kila hila ili kuikataa hoja hiyo. Natangaza kwamba wakifanya hivyo tutasusia na kwenda kuwashtaki kwa wananchi,” alisema Mbowe.
Aliongeza kwamba wataandamana kuanzia Kagera hadi Mtwara kuwaeleza wananchi kwamba hoja yao imepingwa na CCM.
Mbowe alisema baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa wakitoa kashfa dhidi ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kwamba amechukua maoni ya Chadema.
“Wanakosea hayo si maoni ya Chadema, bali ni maoni ya wananchi, Warioba amezingatia maoni ya wananchi,” alisema.
Mwenyekiti huyo alisema Katiba inayotafutwa si ya chama, bali ni ya Watanzania na kwamba inashangaza CCM kuipinga hoja Serikali tatu.
“Tunafahamu wanaogopa kuikubali hoja ya Serikali tatu kwa sababu wanafahamu huo ndiyo utakuwa mwisho wao wa kuwa madarakani,” alisema Mbowe huku akishangiliwa na wafuasi wa chama hicho.
Alisema CCM wanaelewa kwamba kukiwa na Serikali tatu, Chadema kitashinda Tanganyika na CUF Zanzibar katika uchaguzi wowote utakaoitishwa.
“Kwa hiyo hivi sasa wana wasiwasi kweli, wanatafuta kila njia ya kuichakachua hoja ya Serikali tatu lakini wafahamu kuwa Chadema wanaifuatilia hoja hiyo kwa ukaribu,” alisema.
Aliwataka wananchi kufuatilia Bunge Maalumu la Katiba litakapoanza mwezi ujao ili kuangalia wabunge wao wanavyowawalisha katika suala hilo muhimu.
Hata hivyo, Mbowe alisema chama hicho kikishinda katika uchaguzi wa mwaka 2015 hakitahangaika kulipa kisasi kwa kuwachukulia hatua za kisheria viongozi, bali kitajikita kutafuta maendeleo.
“Wasituogope tutasamehe kama alivyosamehe aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. Hatutalipa kisasi tukiingia Ikulu, kwa sababu hakuna binadamu asiye na makosa. Tutaelekeza nguvu zetu kuwaletea maendeleo Watanzania,” alisema Mbowe.
Jussa na Muungano
Akihutubia mkutano wa kampeni katika Jimbo la Kiembesamaki jana, Jussa alisema hakutakuwa na maendeleo yatakayofikiwa Zanzibar ikiwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hautang’oka.
Jussa ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa la CUF, alisema Zanzibar yenye watu milioni 1.5 haiwezi kuwa na tatizo la watu kukosa ajira lakini sera na mipango ya kiuchumi imekuwa ikikwama katika utekelezaji wake kutokana na kukosa mamlaka kamili.
Alisema Zanzibar haiwezi kukopa katika taasisi za kimataifa bila ya kuwekewa dhamana na Waziri wa Fedha wa Muungano wakati Zanzibar ni nchi na kuwataka wananchi kutumia kura zao katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 kuleta mabadiliko ya kiutawala.
“Hakuna sababu ya vijana Zanzibar kukosa ajira, kuna watu wasiozidi milioni 1.5, Muungano umefika wakati ung’oke, ndiyo kikwazo cha maendeleo ya Zanzibar na watu wake kiuchumi na kisiasa,” alisema Jussa.
Alisema mradi wowote unaobuniwa Zanzibar hauwezi kupata mfadhili bila kuwekewa dhamana na Serikali ya Muungano na kukwama kwa juhudi zote za kujiunga na jumuiya za kimataifa akitolea mfano Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu (OIC).
Alisema Rais wa Zanzibar amepoteza mambo muhimu chini ya mfumo wa Muungano ikiwa ni pamoja na kutopigiwa mizinga 21 akiwa nje ya nchi, kupeperusha bendera ya Zanzibar, kutokagua gwaride na kupigiwa wimbo wa Taifa la Zanzibar.
“Haya ya sasa si mamlaka kamili, wapi Dk Shein alikokwenda akapigiwa mizinga 21 au alipeperushwa wapi bendera ya Zanzibar wakati wa safari zake za nje?” alihoji Jussa.

FIRST MEETING OF THE AFRICAN AMBASSADORS IN THE AFRICA HOUSE

 Balozi wa African Union nchini Marekani Mhe. Amina Salum Ali (kulia) akiongoza mkutano wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya African Union lililopo Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano January 29, 2014
 Waheshimiwa Mabalozi waliohudhuria mkutano huo wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya African Union lililopo Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano January 29, 2014.

 Waheshimiwa mabalozi wakifuatilia mkutano wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya African Union lililopo Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano January 29, 2014

D’BANJ NA YAYA TOURE WAUNGA MKONO KAMPENI YA KILIMO YA RAIS KIKWETE

page
D’Banj alishirikiana na washirika wa Kilimo wa Afrika katika uzinduzi wa kampeni ya ‘Shiriki Kilimo’ (Do Agric) kwenye kongamano la Umoja wa Afrika. Kampeni hiyo inalenga kuwasaidia watu zaidi ya milioni 85 barani Afrika kutoka katika lindi la umasikini kupitia uwekezaji maalumu katika kilimo na sera za kilimo za Maputo zilizoboreshwa.
D’Banj alikuwa mmoja wa waliozungumza Addis Ababa jana wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo yenye lengo la kuwahamasisha viongozi wa kisiasa kutumia sera nzuri zitakazonyanyua uzalishaji, kuongeza kipato na kuondoa mamilioni ya Waafrika kutoka katika umasikini.
“Nataka Waafrika kufahamu kilimo ni msingi mzuri wa uchumi ambacho kinatakiwa kutiliwa mkazo na kuleta mabadiliko katika uchumi wa wananchi na nchi na pia tukitilia mkazo tunaweza kuilisha dunia nzima kwa ujumla sisi kama Waafrika,” alisema D’Banj.
Kwa upande wake mchezaji wa timu ya Manchester City, Toure alisema wakati viongozi wengine wa Kiafrika wakitoa kauli zenye nia njema, kwa sasa ni nchi 8 tu zililizotimiza ahadi zake za kuwekeza 10% ya bajeti za nchi katika kilimo.
“Kwahiyo ni muhimu kufanya zaidi na kwenda mbele zaidi. Kilimo sio muhimu pekee, pia ni lazima. Kilimo kinalipa,” alisemaToure.
Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na asasi mbalimbali za kiraia zikiwemo Pan African Farmers Association (PAFO), Action Aid International , Acord International, Oxfam na Alliance for Green Revolution In Africa (AGRA) mbali na asasi hizo mwanasoka wa kimataifa wa Ivory Coast Yaya Toure pia ametia saini kuunga mkono uhamasishaji huo.
Source:Habari leo

JUSTIN BIEBER AJISALIMISHA POLISI NCHINI CANADA KWA KOSA LA KUMSHAMBULIA DEREVA WA LIMO

Bieber mwenye miaka 19 alijisalimisha mwenyewe kwenye kituo cha polisi jijini Toronto ambako alizungukuwa na kundi kubwa la maripota wa TV, wapiga picha na mashabiki wake waliokuwa wakishangilia. Kesi hiyo inakuja ikiwa ni wiki moja baada ya kushikiliwa na polisi kwa kosa jingine huko Miami kwa kuendesha gari akiwa amelewa. Hata hivyo wakili wa muimbaji huyo amesema mteja wake hana hatia.
Polisi jijini Toronto wanasema Justin Bieber alikuwa miongoni mwa watu sita waliochukuliwa na limousine nje ya klabu ya usiku December 30. “Wakati kundi hilo linapelekwa hotelini, ugomvi ulitokea kati ya abiria mmoja na dereva wa limousine hiyo,” maelezo ya polisi yalisema.
Maelezo hayo yamedai wakati wa vurugu huyo, mmoja wao alimpiga dereva nyuma ya kichwa chake mara kadhaa na hivyo limousine kusimama na dereva akaita polisi lakini mtu aliyemshambulia dereva huyo alikimbia.
Kutokana na kosa hilo, Bieber atapanda kizimbani kwenye mahakama ya Toronto, March 10.
Mapema Jumatano hii, jumla ya sahihi 100,000 zilikusanywa kupitia website ya ikulu ya Marekani zinazodai Bieber afukuzwe nchini Marekani. Rais wa Marekani hana mamlaka ya kuagiza kufukuzwa kwa mtu na haijulikani kama White House itajibu malalamiko hayo.

Magazeti ya leo January 31 2014

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Thursday, January 30, 2014

PICHA KIJANA ALIYEGONGWA NA TRENI BAADA YA KUWEKA HEADPHONE MASKIONI



Jamaa mmoja amekubwa na mkasa wa aina yake pale alipogongwa na treni ambayo ilikuwa na kazi kubwa ya
kumpigia honi ili atoke pembezoni mwa reli alipokuwa akitembea. Walioshuhudia tukio hilo wamesema treni hiyo ilipiga honi lakini jamaa alikuwa ameweka Head phones masikioni. 
Credit:Udaku Specially

MABASI YA MWAKYEMBE YAANZA KUTESA APA MUJINI BONGO LIVE!!


 Basi la mwendo kasi likikatiza mtaa wa Lumumba ikiwa sehemu ya majaribio ya mabasi hayo ambayo yanaaminika yataondoa kabisa tatizo la usafiri katika jiji la Dar.

KWA MADADA:LIPSTICK NI HATARI , SOMA HAPA KAMA HUJUI



 
NewsImages/6705586.jpg
Wataalamu hao wamesema kuna umuhimu mkubwa wa kupunguza matumizi ya Lipstick, hasa kwa wanawake wajawazito na watoto

wa dogo, mmoja ya wataalamu hao akielezea madhara yaliyopo katika kipodozi hicho pendwa kivutio cha wengi amesema, kila lipstick moja ina Material 55% ya madhara kwa afya ya mtoto.Uchunguzi uliyofanywa na wataalamu hao katika mashirika 22 makubwa duniani yanayojihusisha na utengenezaji wa kipodozi hicho, umebaini kwamba mashirika 12 kati ya 22 yanatumia material yenye madhara kwa watoto, miongoni mwa madhara ya kipodozi hicho, ni kudhofika kwa akili ya motto na kupunguwa uwezo wa kujifunza.

Katika siku za hivi karibuni midomo imekuwa sehemu muhimu sana katika kukamilisha urembo na unadhifu wa wanawake, lipstick imekuwa inawafanya waonekane wana mvuto zaidi na kuongeza kupendeza katika muonekano wao.

SERIKALI YAIJIBU GAZETI LA SERIKALI YA RWANDA BAADA YA KUMSINGIZIA UONGO JK


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ubalozi wa Tanzania katika Rwanda usiku wa jana, Jumatano, Januari 29, 2014 ulitoa taarifa kwa vyombo vya habari ikikanusha habari za uongo na uzushi ambazo ziliandikwa mwishoni mwa wiki na gazeti la Serikali ya Rwanda la News of Rwanda.
Ifuatayo ni taarifa kamili iliyotolewa na Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Rwanda,
Mheshimiwa Francis Mwaipaja:
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

30 Januari, 2014

STATEMENT ON CLAIMS BY THE NEWS OF RWANDA
The Embassy of Tanzania in Rwanda is deeply saddened by malicious and untrue reports, published over the weekend by the Rwanda Government Owned Newspaper, The News of Rwanda, in which it accuses the President of the United Republic of Tanzania, HE Jakaya Mrisho Kikwete, of supporting and holding meetings with members of rebel groups opposed to the Government in Kigali.
Indeed, these reports are nothing but a bunch of dangerous lies fabricated by editors of this publication with obvious malicious intent to attack the person of the President of a friendly neighbouring country and create an impression that Tanzania is working with enemies and groups opposed to the Government of Rwanda.
The News of Rwanda, which has gained uneviable notoriety of reporting and publishing malicious, dangerous and perpetual propaganda, quoting unnamed sources claims, among other things, that two founding members of the Rwanda National Congress (RNC) including Dr. Theogene Rudasingwa met secretly in Dar es Salaam with top commanders of the Democratic Forces for Liberation of Rwanda (FDLR).
Given the enormity and dangerous nature of these reports, the Embassy of Tanzania in Rwanda would like to make the following clarification:
1.       That the so called founding members of Rwanda National Congress, Dr.  Rudasingwa and adviser Condo Gervais together with top commanders of FDLR, namely Lt. Col Wilson Irategeka and Col Hamadi were not in Tanzania last week. Indeed, our records do not show that they have visited Tanzania in the recent years.

2.     That, there was no meeting of any kind at any official residences of President Kikwete, either in Dar es Salaam or in Dodoma or anywhere. Indeed, President Kikwete has never met any of those people mentioned anywhere – in Tanzania or outside. Moreover, on the day that News of Rwanda claims that the meeting took place, Thursday 23rd, this month, the President was not even in the country – he was in Davos attending the meeting of the World Economic Forum (WEF).

3.     That, the former Prime Minister of Rwanda Faustin Twagiramungu was also not in Tanzania on any or the same mission and did not attend the meeting with representatives of RNC and FDLR as no meeting of such nature took place in Dar es Salaam or anywhere in Tanzania as alleged by this paper. The Immigration Department in Tanzania does not have a record of such people entering or exiting the country.

4.     That, The Tanzania Immigration Department has never issued any travel document to any Rwandan citizen including those claimed in the News of Rwanda that they travelled to Mozambique using Tanzanian passports on or around December 20th 2013. It is not the business of Tanzania to issue travel documents to citizens of other countries.

5.     That it is also untrue that the so-called, “insider establishment” in Tanzania is providing the base for organization and facilitation for travel for FDLR fighters. It is open secret that there is no presence of even a single FDLR fighter in Tanzania. The News of Rwanda should know better where these fighters are based and operate from.
As mentioned earlier, this report and other similar reports published in recent weeks by the News of Rwanda are not only untrue, baseless and mere fabrication but also dangerous and threatening to the excellent and sound diplomatic and social relations between our two neighbouring countries, both of which are members of the East African Community (EAC).
President Kikwete is deeply hurt by these lies and his humble advice to the editors of this publication is to stop fabricating untrue claims which potentially could create and fuel animosity and confusion among the people of our two neighbouring and friendly countries. At a time when President Kikwete and President Paul Kagame of Rwanda had agreed in Kampala to foster friendly relations, such newspaper claims can only sour the atmosphere and President Kikwete would like to know what the editors of the publication are up to?
The Embassy of Tanzania in Rwanda does not take lightly these allegations by the News of Rwanda given the position that this publication occupies in Rwanda.

VIDEO YA SNURA YAPIGWA ''STOP'' KWENYE VITUO VYA TV

Inawezekana ukawa unashangaa baada ya kuona ukimya mara baada ya kutambulishwa kwa video ya Msanii Snura kisha kutoiona ikionekana mara kwa mara kwenye televisheni yako,kiu ya swali hili naikata kwa kusikiliza alichokisema Bosi anaesimamia kazi za Snura meneja wake ‘HK’.

Hk ameanza kwa kusema>>’Kilichotokea ni kwamba video ya Nimevurugwa ni video tuliyokua tunakata kiu ya mashabiki wetu waliokua wamemis vitu fulani kwenye video ya Majanga’
‘Wengi tulivyotoa video ya Majanga walizungumza mengi sana wakidai kwamba video haikuwa nzuri sana,video ya kawaida na sababu kubwa ilikua ni Snura hakukata mauno kwenye hiyo video,tukaona tukate kiu ya wapenzi wetu ambao ukiacha tu nyimbo za Snura watu wanapenda kumuona Snura akitumia maumbile yake kwenye kucheza’

‘Kwenye video ya Nimevurugwa kumekua na style tofauti sana kwenye upande wa kucheza,matokeo yake video ilipotoka siku chache vituo vya televisheni viliacha kupiga wimbo wa msanii wangu,nikiwa kama meneja nikaanza kuzunguka kujua ni sababu gani hawapigi video ya msanii wangu’
‘Baada ya kuzunguka kwenye baadhi ya vituo sababu waliniambia hawapigi kwa sababu ina viuno vingi sana na kudai vimezidi,vinashawishi ngono nilipoenda sehemu nyingine wakanambia hivyo hivyo kwamba sijui wakipiga hiyo video Tcra wanawapa barua ya onyo lakini vituo vya nje ya nchi inapigwa tu’
‘Kitu kinachonishangaza ni baadhi ya nyimbo zenye mahadhi kama ya nyimbo ya Snura zinapigwa kwenye vituo vya televisheni,nachofanya sasa hivi ni kuelekea Basata na Tcra na kuwapelekea ile nakala watuambie kama kweli ile video hairuhusiwi na ni kweli wamewakataza watu wasipige ile video,lakini mimi kama meneja sijapokea barua yoyote inayosema video ya msanii wangu imefungiwa’.
‘Hatua ya kwanza nayoifanya ni kwenda Tcra na Basata kujua kama hii kitu imefungiwa nikijua hapo nitajua kama ni kufanya upya ile video au kutoa hivyo vipande wanavyosema vinashawishi hivyo vitu,kisha nitoe upya hiyo

PICHA:SPIKA WA BUNGE, MH. ANNE MAKINDA ATEMBELEA MAKAZI YA BALOZI MODEST MERO, GENEVA

 Picha ya pamoja, Mh. Modet Mero, Mh. Anne Makinda na mama Mero, kwenya makazi ya balozi.
 Mh. Spika Anne Makinda akishukuru baada ya kukabidhiwa na mwenyekiti wa watanzania, nakala ya Katiba ya Jumuiya ya Watanzania
Mh. Spika katika picha ya pamoja na Mh. Balozi Modest Mero pamoja na viongozi wa Jumuiya ya Watanzania waishio Uswisi.
---
Spika wa Bunge, Mh. Anne Makinda ametembelea makazi ya Balozi Modest Mero, kumsalimu na pia kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Jumuiya ya watanzania waishio hapa Uswisi.

Mh. Spika pamoja na ujumbe wake alikuwa Geneva, 27-28 Januari 2014, kuhudhulia kikao cha kwanza cha kamati ya Maspika  kwa ajili ya kuandaa mkutano mkuu wa Dunia wa Maspika.

PICHA KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS(IKULU):MAKAMU WA RAIS DKT.GHARIB BILAL AKUTANA NA MAWAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, SAYANSI ELIMU IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Asha-Rose Migiro, wakati alipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo kwa mazungumzo.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwakaribisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa (katikati) wakati walipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo kwa mazungumzo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa (katikati) wakati walipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo.Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

PICHA KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS(IKULU):RAIS JAKAYA KIKWETE AWAAPISHA WAZIRI NA MANAIBU WAZIRI IKULU LEO JIJINI DAR ES SALAAM

 Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri na Manaibu Waziri waliokuwa wakiapisha Ikulu Dar es Salaam, leo wakati alipokuwa akiwasili katika hafla hiyo.
 Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Ummy Mwalimu, kuwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo.
  Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha George Boniface Tuguluvala Simbachawene, kuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,  wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo.
 Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Kaika Saning’o Telele, kuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo.
  Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Eng. Dr. Binilith Satano Mahenge, kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo.
  Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakia katika picha ya pamoja na Waziri na Manaibu Waziri walioapishwa katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam, leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wapya na wa zamani wa Ofisi yake, baada ya kuapishwa wapya katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo. Kutoka (kulia) ni aliyekuwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Charles Muhangwa Kitwanga, ambaye kwa sasa ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano)Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Eng. Dr. Binilith Satano Mahenge, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu na aliyekuwa Waziri wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Terezya Huvisa, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri, iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo.Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais