Pages


Photobucket

Tuesday, October 23, 2012

MAHAKAMA KUU KANDA YA ARUSHA YAMWACHIA HURU ALIYEKUWA KATIBU WA MBUNGE WA ARUSHA MJINI

MAHAKAMA  kuu  kanda ya  Arusha, imemwachia huru aliyekuwa Katibu wa Mbunge wa Arusha mjini Gervas Mgonja baada ya mahakama kudhibitisha  kutokuwa na kesi ya kujibu iliyokuwa ikimkabili  mahakamani   hapo.

Akitoa maamuzi madogo (Rulling)  mahakamani hapo,    Hakimu Mkazi  wa mahakama kuu, Judith Kamala kwa kushirikiana na Mwendesha mashtaka wa serikali ,Haruna Matagane alisema kuwa ,mahakama imeamua kumwachia huru mshtakiwa huyo na wenzake wawili baada  ya kubaini kuwa hawana kesi ya kujibu katika shitaka la kula njama na kutenda kosa lililokuwa likiwakabili.
Mgonja  alishtakiwa na wenzake wawili akiwemo aliyekuwa katibu wa vijana wa chadema wilaya ya Arusha ,Anold Kamnde na Frank Njau aliyekuwa katibu wa vijana kata ya Ngarenaro kupitia chadema ,ambapo kwa pamoja mahakama imewaachia huru baada ya kupitia upande wa ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka ambao walileta mashaidi sita .
Hakimu Kamala alisema kuwa,washtakiwa hao watatu kwa pamoja walikuwa wakishtakiwa na wenzao wengine watatu jumla sita kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha ambapo upelelezi ulipokamilika ulibaini kuwa washtakiwa watatu akiwemo Mgonja  walifungliwa shitaka hilo la unyang’anyi wa kutumia silaha kimakosa na hivyo mahakama kuwaondoa katika shitaka hilo na kubakia na washatakiwa watatu ambao wanaendelea na kesi hiyo.
Washtakiwa waliobakia na kesi hiyo ya unyan’ganyi  wa kutumia silaha baada ya mahakama kudhibitisha kuwa Mgonja na wenzake wawili walifungulia shitaka hilo kimakosa  ni Frank Ismail, Philemon Inyasi, na Charles George.
Aidha kufuatia kesi hiyo ya unyang’anyi  wa kutumia silaha  iliwapelekea mgonjwa na wenzake kukaa ndani kwa siku 120 tangu walipofunguliwa shitaka agosti 20 hadi upelelezi ulipokamilika ,januari 15 ,2012 na  kuwaondoa katika kesi hiyo na kusomewa shitaka jipya la  kula njama ya kutenda kosa na kupewa dhamana. .
Ambapo  kesi hiyo mpya  ilianza kusikilizwa  januari 15 mwaka huu , huku upande wa mashtaka ukileta mashaidi 6  ambapo  kesi  ilirindima kwa kipindi cha miezi kumi ndipo maamuzi maamuzi madogo ya mahakama  yalipotolewa kuwa mshatakiwa hana shitaka la kujibu.
‘Kutokana na kusikiliza upande wa mashahidi kwa makini  nimetosheka na ushahidi uliotolewa na mahakama  na nimemwachia huru  Gervas Mgonja na wenzake wawili  na kuwa hawana kesi ya kujibu ‘alisema Kamala.
Akizungumza mara baada ya maamuzi hayo ,Gervas Mgonja alisema kuwa, anamshukuru Mungu sana kwani haki imeweza kutendeka na leo hii ameachiwa huru , pamoja na kuwa kesi zote hizo alibambikiziwa .
‘Kwa kweli sijui hata niseme nini namshukuru Mungu  kwa  kunitetea na kesi yangu imeisha na leo hii nipo huru , kwa kweli sina cha kusema ila  nawaomba polisi  wawe  makini kabla ya kuchukua hatua,  wafanye uchunguzi  ili waweze kuwatendea haki sawa raia wote.
 Alitoa wito kwa  jeshi la polisi kuwa makini katika utendaji wake ili kuepuka uonevu mkubwa unaofanyika kwa kuwafungulia watu kesi ambazo hawakuhusika kitendo kilichompelekea   kukaa ndani miezi 5 bila kosa lolote na baadaye ndipo alipogundulika kuwa alifunguliwa shitaka hilo kimakosa na hiyo ni kutokana na kutokuwa makini kwa jeshi hilo.
 
 
***Habari hii ni kwa msaada wa blogu ya "woindeshizza" ****

No comments:

Post a Comment