Pages


Photobucket

Sunday, February 9, 2014

MAAJABU YA DUNIA;HII NDO PICHA YA MAITI ILIYOGANDA NA KUTAA KUZIKWA KWA MDA WA MIAKA 500

Girl Frozen For 500 years
Girl who was killed as an offering to the
Inca gods sometime between 1450 and
1480, at approximately 11–15 years old.
best-preserved mummy ever found, with
internal organs intact, blood still present in
the heart and lungs, and skin and facial
features mostly unscathed. No special
effort had been made to preserve her and
500 years later still looked like sleeping
child
Girl Frozen For 500 years
Girl who was killed as an offering to the
Inca gods sometime between 1450 and
1480, at approximately 11–15 years old.
best-preserved mummy ever found, with
internal organs intact, blood still present in
the heart and lungs, and skin and facial
features mostly unscathed. No special
effort had been made to preserve her and
500 years later still looked like sleeping
child
source- thechoicetz.com

HII NDIO HISTORIA YA MASANJA MKANDAMIZAJI................SOMA HAPA KUJUA ZAIDI


Kwa wapenzi wa sanaa ya vichekesho, jina la Masanja Mkandamizaji si geni masikioni mwao kutokana na uwezo wake wa kuwavunja mbavu watazamaji pale anapoonekana katika runinga na Kundi la Original Comedy.

Licha ya kufika hapo alipo sasa, msanii huyu anakiri wazi kuwa amepitia katika ugumu hususani wakati alipoamua kuanza maisha binafsi ya kujitegemea baada ya kutoka nyumbani kwa dada yake alipokuwa akiishi

Anasema kabla ya kuondoka kwa dada yake alimuomba amtafutie chumba ili ajitegemea na kuanza maisha binafsi kama kijana .

Nilimwambia dada anitafutie chumba na alifanya hivyo ingawa alikuwa anahofia kama nitaweza ,basi nikapata 'geto' langu maeneo ya Tabata Aroma na nilitakiwa kulipa kodi ya Sh5000 kwa mwezi, anasema Masanja.

Anakiri wazi kuwa changamoto katika maisha ndizo zilizochangia kumfikisha mahali alipo sasa kwani licha ya kuwa katika hali ngumu hakukata tama bali alizidi kujituma kwa nguvu zake zote.

Anasema kuna wakati ilikuwa vigumu kuipata hata hiyo hela ya kodi kwahiyo ilikuwa inamlazimu kurudi kwa dada yake kwa muda unapofikia wakati kulipa kodi.

Yaani hiyo Sh5000 kuipata ilikuwa shughuli maana ilikuwa ikifika karibu na mwisho wa mwezi narudi kwa dada kuzuga kidogo ili mama mwenye nyumba ajue nimesafiri,anasema.

Anasema alianza kwa kulala chini mpaka siku alipofanikiwa kupata fedha kidogo iliyomuwezesha kununua godoro la sufi jambo ambalo anajivunia nalo kwani aliweza kununua kwa jasho lake.

Anaongeza kuwa kamwe hawezi kumsahau marehemu Steven Kanumba pamoja na mtu mwingine aliyemtaja aitwaye Mtitu kutokana na mchango wao uliosaidizi kumfikisha hapo alipo sasa .

Namshukuru sana marehemu Kanumba alikuwa anakuja kunichukua kule Tabata tunaenda kupiga 'inshu' ambazo zilikuwa zikiniingizia pesa kidogo iliyoniwezesha kuishi hata hivyo maisha yalikuwa magumu.

Wakati naanza maisha sikuwahi kutoa hela hata ya kununua chipsi kavu lakini siku moja nilifanya kazi na Mtitu ambayo alinilipa laki moja sikuamini macho yangu, kwa mara ya kwanza kununua chipsi kuku kwani nilikuwa nikitamani mlo huo nililazimika kusaidia kumenya viazi kwa washikaji,

Sambamba na uchekeshaji Masanja pia amejiingiza katika shughuli za kumtukuza Mungu baaada ya kuokoa na sasa anafanya vizuri pia katika uimbaji wa nyimbo za injili na kesho Jumapili atazindua albamu yake ya pili ya muziki wa Injili inayoitwa Hakuna jipya chini ya jua.

Saturday, February 1, 2014

CCM YAZIDI KUJIIMARISHA MBEYA MJINI

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akigawa kadi kwa wanachma wapya waliojiunga na CCM baada ya kuzindua shina la Wakereketwa la Madereva wa Bodaboda Inyara,Iyunga mkoani Mbeya.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Inyara, Iyunga mjini mkoani Mbeya baada ya kuzindua shina la wakereketwa ambapo aliwaambia CCM imejiandaa vya kutosha kwa ushindi wa 2015..
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Inyara ,Iyunga baada ya kuzindua shina la wakereketwa la madereva wa Boda Boda.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wafanyabiashara ndogo ndogo wa  Inyara ,Iyunga mkoani Mbeya.

Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Iyunga mara baada ya kufungua shina la wakereketwa ambapo alisisitiza kwa madereva wa boda boda kuwa Umoja ni Ushindi hivyo kukiwa na umoja dhabiti kati yao basi watafanikiwa sana na aliwasihi vijana waepuke dhambi ya kubaguana.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa na dereva wa BodaBoda wa Iyunga Itika Mwangosi ambaye amejiunga na chama cha mainduzi na kukabidhiwa kadi yake na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na baadhi ya viongozi wa CCM Iyunga mara baada ya kufungua shina no.3 la Bodaboda .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na mmoja wa wapenzi wa CCM aliyekuwa akisafiri kwa Bajaj ,Soweto mjini Mbeya.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitembea mitaa ya Soweto kwenda kufungua shina la wakereketwa wauza chakula na wauza matairi kata ya Ruanda,Jumla ya mashina manne yalizinduliwa leo mjini Mbeya.