Pages


Photobucket

Thursday, November 1, 2012

Vitisho vya al-Shabaab vyajaribu kuvuruga kwa kupoteza kwao Kismayo

Na Bosire Boniface, Wajir

Al-Shabaab inajaribu kupata nguvu ya msaada wa kimataifa kwa wapiganaji wake waliokata tamaa baada ya kupoteza ngome ya mji wa bandari wa Kismayu kwa kutoa vitisho kwa nchi kadhaa, maofisa wa usalama na wachambuzi wasema.
Mwanaume akitia rangi ya kufuta alama ya al-Shabaab huko Wanlaweyn tarehe 11 Oktoba baada ya vikosi vya Umoja wa Afrika na vya serikali kukamata mji huo kutoka kwa kikundi hicho cha wanamgambo. [Mohamed Abdiwahab/AFP]Al-Shabaab imekuwa ikihuisha akaunti yao ya Twitter mara kwa mara kutoka ilipopoteza katika jaribio la kubakia kuwa muhimu na kushawishi wafuasi wake kujilinda dhidi ya kile inachokiita vita na ukatili dhidi ya Waislamu wasio na hatia.
Kikundi hicho cha wanamgambo kimetishia kushambulia Uingereza pamoja na nchi jirani na Somalia.

Katika mfululizo wa matangazo 15 yaliyotolewa kwenye mtandao wa Twitter tarehe 22 Oktoba, al-Shabaab ilisema kuwa Uingereza "itagharimia sana jukumu lake la kutokuwa na haya katika vita dhidi ya Uislamu na ukatili usiokwisha dhidi ya Waislamu wasio na hatia".

"Jinamizi ambalo kwa siri lilionekana kuwa tishio kubwa kwenye fuko za Uingereza lilikwenda mpaka kusababisha vitisho vilivyounganishwa vya 7/7 na 21/7," al-Shabaab ilisema.

Mabomu yaliyopiga London tarehe 7Julai, mwaka 2005, yalikuwa mfululizo wa mashambulio ya kujitoa muhanga yaliyoratibiwa kwenye mfumo wa usafiri wa umma wa jiji hilo ambayo yaliwaua raia 52 na walipuaji wanne. Wiki mbili baadaye, mashambulio manne yalijaribu kuharibu sehemu ya mfumo wa usafiri wa umma wa jiji hilo.

Al-Shabaab pia iliapa kulipiza kisasi kwa uamuzi wa Mahakama Kuu ya London kumrejesha mwalimu wa dini ya Kiislamu mwenye msimamo mkali Mustafa Kamel Mustafa, ambaye anajulikana sana kama Abu Hamza al-Masri, kwenda Marekani tarehe 5 Oktoba kuhukumiwa katika nchi aliyofanya kosa. Mustafa alishtakiwa kwa kuweka kambi ya mafunzo huko Oregon, kosa ambalo alilikana tarehe 9 Oktoba katika mahakama ya New York
Siku ya Jumapili (tarehe 28 Oktoba), kikundi hicho cha wanamgambo hao ilirudia tena vitisho dhidi ya Kenya , ambayo jeshi lake limekuwa likipigana na al-Shabaab nchini Somalia kwa kipindi cha zaidi ya mwaka.

"Maadui tunaokumbana nao wamefanya ukokotozi mbaya wa kihistoria wakati walipotuma Kenya kuvamia ardhi ya Kiislamu ya Somalia," alisema mmoja wa wasemaji wake anayedhaniwa kuwa kiongozi wa al-Shabaab Mukhtar Abu Zubayr, pia anayejulikana kama Ahmed Godane. "Kenya hivi punde itajuta kwa kujiingiza kwake katika jambo hili, Insha Allaah [Mungu akipenda]."

Vitisho ni mwito wa kukusanya nguvu ya kuongeza hamasa
Wachambuzi na viongozi wa usalama waliiambia Sabahi kwamba vitisho vinafanywa na kundi lililofungamana na al-Qaeda ili kubadili mwelekeo kutokana na kuipoteza Kismayo.

Mwanajeshi mstaafu Meja Bashir Hajji Abdullahi, mchambuzi na mshauri wa usalama anayeishi Nairobi, alisema uongozi wa kundi hilo una matumaini ya vitisho hivyo kuifikia operesheni ya nchi za ugenini ambayo haitawawafanya al-Shabaab wahusike tu kimataifa, lakini pia kuwashangaza wapiganaji wake ambao alisema wanajisikia kushushwa hadhi baada ya kupotoshwa kufikiria kwamba walikuwa wasioshindika huko Kismayo.

David Ochami, mwandishi wa habari anayeishi Mombasa ambaye anayefuatilia wanamgambo huko Mashariki ya Kati na Pembe ya Afrika wa gazeti la The Standard la Kenya, aliiambia Sabahi kwamba vitisho vya al-Shabaab visidharauliwe kutokana na upotevu wa hivi karibuni.

"Kwa kuwa na wanajihadi wageni katika ngazi zake, hata mwanamgambo moja ni hatari," alisema Ochami. "Wanaweza kukosa eneo ambalo watalitumia kuunda, lakini watajipanga sana katika mbinu za vita vya msituni ili waendelee kuwepo."

Tishio linaweza kuonekana kama mwito wa kukusanya nguvu kwa ajili ya kuongeza hamasa ya wapiganaji wa al-Shabaab ambao wametoroka na kuungana na wananchi wengine, kwa mujibu wa Ochami.

Alisema vitisho vya al-Shabaab dhidi ya Uingereza haitomaanisha kushambulia ardhi ya Uingereza, aliongeza kwamba uangalifu mkubwa unahitajika kuilinda Uingereza na nchi nyingine za kigeni huko Kenya na sehemu nyingine.

Bado, Ochami aliudharau uwezo wa al-Shabaab kufanya shambulio kubwa, hata karibu na nyumbani.

"Hakuna anayepoteza usingizi siku hizi wanapotoa vitisho kwa sababu hawana uwezo wa kufanya shambulio la hali ya juu kwa muda mfupi," alisema.

Waziri wa Ulinzi wa Kenya Yusuf Haji alisema serikali inavizingatia vitisho hivyo na inawasiliana na balozi za nchi za nje kila siku kuangalia vitisho hivyo na kutafuta njia gani nzuri za kukabiliana navyo.

"Tupo tayari kwa vita na wanamgambo," aliiambia Sabahi. "Itakuwa ndefu, lakini uzuri wakati wote hushinda ubaya."
 
 

No comments:

Post a Comment