Pages


Photobucket

Sunday, November 18, 2012

ISRAEL YASHAMBULIA MAKAO MAKUU YA HAMAS


An explosion and smoke are seen after Israeli strikes in Gaza City November 17, 2012. Israeli aircraft pounded Hamas government buildings in Gaza on Saturday, including the building housing the prime minister's office, after Israel's Cabinet authorised the mobilisation of up to 75,000 reservists, preparing the ground for a possible invasion into Gaza. REUTERS/Suhaib Salem (GAZA - Tags: CIVIL UNREST MILITARY POLITICS TPX IMAGES OF THE DAY)Ndege za Israel zimeshambulia majengo ya serikali ya chama cha Hamas huko Gaza ikiwemo ofisi ya waziri mkuu baada ya baraza la mawaziri la Israel kuidhinisha kuitwa kwa wanajeshi wa akiba 75,000 kuvamia Gaza.

Ndege hizo za Israel zimeshambulia wizara ya ulinzi na jengo la ofisi ya Waziri Mkuu Ismail Haniyeh ambapo hapo Ijumaa alikutana na Waziri Mkuu wa Misri. Kwa siku kadhaa miripuko mizito imekuwa ikilitingisha eneo la Gaza linalokaliwa na idadi kubwa ya watu na kusababisha kufuka kwa moshi mzito angani.

Hamas yaendelea kurusha maroketi

Wanamgambo wa itikadi kali za Kiislamu nao wamekuwa wakiendelea kuvurumiosha maroketi nchini Israel. Licha ya machafuko hayo,waziri wa mambo ya nje wa Tunisia amewasili Gaza leo hii kuonyesha
mshikamanona na Wapalestina na kushutumu mashambulizi hayo ya Israel kuwa sio halali na yasiokubalika.

Maafisa huko Gaza wanasema Wapalestina 41 wakiwemo raia 20 watoto wanane na mwanamke mmoja mjamzito wameuwawa katika huko Gaza tokea Israel ilipoanza operesheni zake siku nne zilizopita.Raia watatu wa Israel wameuwawa na shambulio la roketi hapo Alhamisi.

Jeshi la Israel limesema kikosi chake cha anga kimeshambulia takriban maeneo 180 waliokuwa wameyalenga jana usiku ikiwa ni pamoja na makao makuu ya polisi majengo ya serikali,vikosi vya kurusha maroketi na kituo cha mafunzo cha Hamas katika Ukanda huo wa Gaza uliozongwa na umaskini.

Jengo la ghorofa tatu la afisa wa Hamas Abu Hassan Salah pia lilishambuliwa na kuharibiwa kabisa mapema leo alfajiri. Waokoaji wamesema takriban watu 30 wametolewa kwenye kifusi cha jengo hilo.

No comments:

Post a Comment