 Ndege
 za Israel zimeshambulia majengo ya serikali ya chama cha Hamas huko 
Gaza ikiwemo ofisi ya waziri mkuu baada ya baraza la mawaziri la Israel 
kuidhinisha kuitwa kwa wanajeshi wa akiba 75,000 kuvamia Gaza.
Ndege
 za Israel zimeshambulia majengo ya serikali ya chama cha Hamas huko 
Gaza ikiwemo ofisi ya waziri mkuu baada ya baraza la mawaziri la Israel 
kuidhinisha kuitwa kwa wanajeshi wa akiba 75,000 kuvamia Gaza.
Ndege hizo za Israel zimeshambulia wizara ya ulinzi na jengo la ofisi ya
 Waziri Mkuu Ismail Haniyeh ambapo hapo Ijumaa alikutana na Waziri Mkuu 
wa Misri. Kwa siku kadhaa miripuko mizito imekuwa ikilitingisha eneo la 
Gaza linalokaliwa na idadi kubwa ya watu na kusababisha kufuka kwa moshi
 mzito angani.
Hamas yaendelea kurusha maroketi
Wanamgambo wa itikadi kali za Kiislamu nao wamekuwa wakiendelea 
kuvurumiosha maroketi nchini Israel. Licha ya machafuko hayo,waziri wa 
mambo ya nje wa Tunisia amewasili Gaza leo hii kuonyesha
mshikamanona na Wapalestina na kushutumu mashambulizi hayo ya Israel kuwa sio halali na yasiokubalika.
Maafisa huko Gaza wanasema Wapalestina 41 wakiwemo raia 20 watoto wanane
 na mwanamke mmoja mjamzito wameuwawa katika huko Gaza tokea Israel 
ilipoanza operesheni zake siku nne zilizopita.Raia watatu wa Israel 
wameuwawa na shambulio la roketi hapo Alhamisi.
Jeshi la Israel limesema kikosi chake cha anga kimeshambulia takriban 
maeneo 180 waliokuwa wameyalenga jana usiku ikiwa ni pamoja na makao 
makuu ya polisi majengo ya serikali,vikosi vya kurusha maroketi na kituo
 cha mafunzo cha Hamas katika Ukanda huo wa Gaza uliozongwa na umaskini.
Jengo la ghorofa tatu la afisa wa Hamas Abu Hassan Salah pia 
lilishambuliwa na kuharibiwa kabisa mapema leo alfajiri. Waokoaji 
wamesema takriban watu 30 wametolewa kwenye kifusi cha jengo hilo.
 
 

No comments:
Post a Comment