Pages


Photobucket

Wednesday, November 28, 2012

Washukiwa wa ICC Kenya kuunda Muungano


 Uhuru Kenyatta ni mmoja wa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007

Washukiwa wawili wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya, Uhuru Kenyatta na William Ruto wanajadiliana kwa lengo la kuunda muungano wa kisiasa watakaotumia kugombea uongozi wa nchi.
Taarifa za awali zilisema kuwa wawili hao tayari wameunda muungano huo ingawa baadaye afisa wa mawasiliano wa vigogo hao alikana kuwepo makubaliano yoyote.
Wawili hao ambao ni mahasimu wa jadi kisiasa,wanaanda mkutano wa pamoja siku ya Jumamosi mjini Nakuru mojawapo ya maeneo yaliyokumbwa na ghasia mbaya zaidi za kikabila baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007.
Na hataua ya wawili hawa inakuja wakati mahakama ikitarajiwa kutoa uamuzi kuhusu ikiwa wanaweza kugombea uongozi wakati wanakbiliwa na tuhuma za kuhusikana ghasia za baada ya uchaguzi ambapo mamia ya watu waliuawa.
Wanasema wameamua kuunda muungano watakaoutumia kuwania nafasi ya rais na makamu wake katika uchaguzi mkuu mwaka ujao kama ishara ya kuwapatanisha wakenya.
Wanatarajiwa kufika mbele ya mahakama ya ICC baada ya uchaguzi mwaka ujao kujibu mashtaka ya kuhusika na ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi mwaka 2007-2008
Kenyatta ambaye ni naibu waziri mkuu na Ruto ambaye ni mbunge , wanasema kuwa muungano wao utakuwa wenye kauli mbiu ya kupigia debe umoja wa kitaifa, ustawi na kupatanisha wakenya .
Katika uchaguzi uliopita, wawili hao walikuwa pande pinzani. Na ulikuwa uchaguzi ulioshuhudia upinzani mkali zaidi katika historia ya Kenya.
Ulifuatiwa na ghasia za kikabila ambapo mamia ya watu waliuawa na maelfu wengine kuachwa bila makao mwaka 2007.
Wawili hao wamekanusha madai ya kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi hasa kupanga makundi ya watu walioshambulia makundi hasimu.

Na. BBCSwahili

No comments:

Post a Comment