
 Uhuru Kenyatta ni mmoja wa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007
Washukiwa wawili wakuu wa ghasia
 za baada ya uchaguzi nchini Kenya, Uhuru Kenyatta na William Ruto 
wanajadiliana kwa lengo la kuunda muungano wa kisiasa watakaotumia 
kugombea uongozi wa nchi.
Taarifa za awali zilisema kuwa wawili hao tayari
 wameunda muungano huo ingawa baadaye afisa wa mawasiliano wa vigogo hao
 alikana kuwepo makubaliano yoyote.
Wawili hao ambao ni mahasimu wa jadi
 kisiasa,wanaanda mkutano wa pamoja siku ya Jumamosi mjini Nakuru 
mojawapo ya maeneo yaliyokumbwa na ghasia mbaya zaidi za kikabila baada 
ya uchaguzi mkuu mwaka 2007.
Na hataua ya wawili hawa inakuja wakati mahakama
 ikitarajiwa kutoa uamuzi kuhusu ikiwa wanaweza kugombea uongozi wakati 
wanakbiliwa na tuhuma za kuhusikana ghasia za baada ya uchaguzi ambapo 
mamia ya watu waliuawa.
Wanasema wameamua kuunda muungano watakaoutumia 
kuwania nafasi ya rais na makamu wake katika uchaguzi mkuu mwaka ujao 
kama ishara ya kuwapatanisha wakenya.
Wanatarajiwa kufika mbele ya mahakama ya ICC 
baada ya uchaguzi mwaka ujao kujibu mashtaka ya kuhusika na ghasia 
zilizotokea baada ya uchaguzi mwaka 2007-2008
Kenyatta ambaye ni naibu waziri mkuu na Ruto 
ambaye ni mbunge , wanasema kuwa muungano wao utakuwa wenye kauli mbiu 
ya kupigia debe umoja wa kitaifa, ustawi na kupatanisha wakenya .
Katika uchaguzi uliopita, wawili hao walikuwa 
pande pinzani. Na ulikuwa uchaguzi ulioshuhudia upinzani mkali zaidi 
katika historia ya Kenya.
Ulifuatiwa na ghasia za kikabila ambapo mamia ya watu waliuawa na maelfu wengine kuachwa bila makao mwaka 2007.
Wawili hao wamekanusha madai ya kuhusika na 
ghasia za baada ya uchaguzi hasa kupanga makundi ya watu walioshambulia 
makundi hasimu.
Na. BBCSwahili 
 
 

No comments:
Post a Comment