MBUNGE wa 
Jimbo la Ubungo, John Mnyika (Chadema) amesema licha ya kuwa na orodha 
ya vigogo walioficha fedha Uswiss, lakini hawezi kutoa orodha ya majina 
hayo kama Serikali inavyotaka kwa vile orodha ya vinara wa ufisadi 
ambayo ilitajwa Mwembe Yanga bado haijashughulikiwa.
Akizungumza 
katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Sahara jijini 
Mwanza, Mnyika alisema kwamba kama Serikali ya CCM inasisitiza kutaka 
majina ya walioficha fedha huko Uswiss yatajwe, wanapaswa kusimama na 
kueleza ile orodha ya mafisadi ambayo Chadema waliitaja pale Mwembe 
Yanga imefanyiwa kazi gani.
“Watu 
wanapotutaka tutaje majina, na sisi tunawambia kwanza wasimame na 
kutueleza ile ‘list’ (orodha) ya mafisadi ambayo tuliitaja kwa majina 
wameishughulikia vipi?” alihoji Mnyika na kuongeza kwamba wanajua jinsi 
ambavyo CCM wanalivyonufaika na ufisadi kupitia Kampuni ya Kagoda jambo 
ambalo linadhihirisha kuwa haiwezi kuwa rahisi kwao kushughulika na vita
 ya ufisadi.
Alisisitiza 
kuwa wanaotaka majina yatajwe wanayo ajenda yao na wao wameshaifahamu 
hivyo hawatashughulika nayo na kusema ukifika wakati ambao wao 
wanautambua wataweka kila kitu nje, lakini siyo kwa kushinikizwa na 
Serikali ya CCM.
“Tunajua 
serikali hii inayoundwa na Chama Cha Mapinduzi haina dhamira ya 
kushughulika na ufisadi, na hili ndilo litakalowaondoa madarakani,” 
alifafanua.
Hata hivyo 
mkutano huo uliingia dosari wakati Mnyika akiendelea kuhutubia ambapo 
mawe yalianza kurushwa na vijana wanaodaiwa kuwa ni vijana wa Diwani wa 
Kata ya Kitangiri kwa tiketi ya Chadema, Henry Matata aliyevuliwa 
uanachama.
Kutokana hali hiyo vijana wa Chadema walizungumza katika maeneo mbalimbali na kufanikiwa kuwanasa vijana wawili ambao walishambuliwa na kueleza na kunusuriwa na Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje aliyeita polisi na kuwaomba waache kuwashambulia.
Awali 
akizungumza katika mkutano huo Mbunge wa Jimbo la Nyamagana,Wenje 
alieleza wananchi kuwa katika mkakati wake wa kuboresha elimu ya msingi 
na sekondari amefanikiwa kutengeneza madawati mengine 400 baada ya 
madawati ya awali 500 kugawiwa katika shule.
Alisema 
madawati hayo yatagawanywa kwa shule 30 za wilaya ya Nyamagana na 
kubainisha kwamba kutokana na madaati ya awali 500 kutolewa bila 
utaratibu na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza,Wilson Kabwe hivyo madawati 
haya alieleza kuwa yatasambazwa na madiwani wa Chadema katika shule 
pamoja na katibu wa ofisi yake ili kuhakikisha yanafika katika shule 
husika iliyopangwa.
Mwananchi
 
 


No comments:
Post a Comment