Pages


Photobucket

Wednesday, November 28, 2012

Wakazi wasaidia kusafisha mabaki ya al-Shabaab Mogadishu


By Majid Ahmed, Mogadishu

Wakazi wa Mogadishu wanafanya jukumu kubwa katika usafishaji wa mabaki ya al-Shabaab katika mji mkuu, maofisa wa usalama wa Somalia wamesema.

Washukiwa wa Al-Shabaab wakipanda katika gari ndogo ya wazi ya polisi tarehe 10 Oktoba, mwaka 2012 katika kituo cha polisi huko Mogadishu ya kusini. [Abdurashid Abdulle Abikar/AFP]

Fununu kutoka kwa wakazi katika eneo la Yaqshid huko Mogadishu ya kaskazini Jumamosi (tarehe 24 Novemba) ilisababisha katika kukamatwa kwa washukiwa 21 wa al-Shabaab na ugunduzi wa maficho ya silaha, kwa mujibu wa maofisa usalama.

Siku mbili kabla, vikosi vya usalama vilifanya operesheni kutokana na fununu kutoka kwa mmiliki wa shamba huko Yaqshid ambayo matokeo yake ilikuwa mauaji ya kamanda wa al-Shabaab Abdinur Gardhub . Operesheni ya tarehe 22 mwezi Novemba pia ilisababisha kukamatwa kwa wanamgambo wengine 16 ambao walifanya shughuli nje ya kikundi kidogo cha watu katika maeneo ya Yaqshid, Suqa Holaha na Gubta, kwa mujibu wa kamanda wa Idara ya Usalama wa Taifa huko Benadir Koloneli Khalif Ahmed Ereg.

Ereg alisema maficho ya al-Shabaab huko Yaqshid yaligundulika kutokana na taarifa zilizotolewa na wakazi wa eneo hilo.

"Vikosi vya usalama viliwatia kizuizini wanachama 37 wa kikundi cha wapinga amani wa al- Shabaab, wakati wa mfululizo wa mashambulizi ya usiku yaliyofanywa kitongoji cha kaskazini ya Mogadishu," Ereg aliiambia Sabahi. "Mashambulizi haya yalilenga katika usafishaji wa mabaki ya al-Shabaab katika eneo hilo."

"Operesheni hizi zilisababisha kunyang'anywa kwa maficho ya aina tofauti za silaha ikiwa ni pamoja na silaha za vita, bunduki AK-47, silaha, milipuko na maguruneti ya kurusha kwa mkono," alisema.


Ereg alisifu ushirikiano wa wakazi pamoja na vikosi vya usalama. "Tunathamini ushirikiano wa raia na vikosi vya usalama wakati wa operesheni za hivi karibuni ambazo zilisababisha kukamatwa kwa wanachama wa al-Shabaab na ugunduzi wa maficho ya silaha zilizokuwa zinamilikiwa na wanamgambo hao," alisema.

Serikali ya Somalia ilitangaza mwishoni mwa mwezi Aprili kwamba ingetoa hadi dola 500 kwa wananchi watakaojitokeza na taarifa zitakazosaidia kukamatwa au kuuawa kwa wanachama wa al-Shabaab.

Wananchi wapo tayari kusaidia jitihada za usalama
Mzee wa Mogadishu Suleiman Abdullahi alisema kwamba kupigana na wanamgambo ambao wanavuruga usalama wa Somalia ni wajibu wa kidini na kitaifa.

"Vikosi vya usalama wa taifa, polisi na jeshi wote wanafanya kazi inayotakiwa ya kusafisha mji na maeneo yanayozunguka ya wanamgambo," aliiambia Sabahi. "Tunawapongeza katika operesheni hii yenye mafanikio ambayo italeta utulivu zaidi huko Mogadishu, na tupo tayari kutoa msaada kwa vikosi vya usalama."

"Magaidi wanaishi miongoni mwetu na kwa bahati mbaya kuna wale wanaowapa kimbilio salama," alisema Abdullahi. "Kama tunataka kuishi kwa utulivu, amani na usalama, tunapaswa kushirikiana na vikosi vya usalama ili kulinda usalama wetu na pia tunapaswa kutowapa makazi magaidi kwa sababu inamaanisha tunajisaliti sisi wenyewe, taifa letu na nchi yetu kwa ujumla."

Osman Mohamed, kanali mstaafu wa polisi Somalia, alisisitiza umuhimu wa kujenga ujasiri na kushirikiana kati ya wananchi na vikosi vya usalama. Alisema hii ni sababu ya msingi katika mafanikio ya jitihada za polisi na vikosi vya usalama kuendeleza utulivu huko Mogadishu na maeneo mengine yaliyokombolewa hivi karibuni.

"Kuimarisha mawasiliano kati ya wananchi na wafanyakazi wa usalama kunachangia kuelekea katika uimarishaji wa imani ya umma kwa vikosi vya usalama na kuleta kujisikia kuridhika kwa jitihada zao," Mohamed aliiambia Sabahi.

Alisema vikwazo ambavyo vilikuwepo zamani kati ya wananchi na vikosi vya usalama sasa havipo tena. "Vikosi vya usalama vimefanikiwa kwa kiwango fulani kuiteka mioyo na mawazo ya wananchi kwani watu hawaogopi tena vikosi vya usalama na sasa mawasiliano kati ya pande zote yako imara," alisema.

Kuendeleza usalama ni wajibu wa pamoja
Kaimu Gavana wa Masuala ya Usalama wa Benadir Warsame Mohamed Hassan alisema ushirikiano kati ya vikosi vya usalama na wananchi katika kutafuta watu ambao wanavuruga usalama wa umma ni muhimu.

"Shukrani kwa ushirikiano kati ya wananchi na vikosi vya usalama, hali ya usalama huko Mogadishu imeboreshwa kwani viwango vya mauaji na vitendo vya kuvuruga usalama vimepungua kwa wiki chache zilizopita," Hassan aliiambia Sabahi.

Alitoa wito kwa jamii kwa ujumla kuwajibika katika jitihada zinazoendelea zinazokusudia kudhibiti usalama na kuendeleza utulivu huko Mogadishu.

"Majeshi ya usalama hayawezi kufanya kazi yake ya kuendeleza hali ya usalama na kusafisha Mogadishu dhidi ya al-Shabaab bila ushiriki wa jamii," alisema. "Kuimarisha usalama ni wajibu wa pamoja na kila mmoja anapaswa kuwajibika katika hili."

Hassan alisema operesheni za usalama zingeendelea huko Mogadishu hadi mji uwe huru dhidi ya al-Qaeda wanaoshirikiana na wanamgambo wa al-Shabaab.

Chanzo sabahionline.com

No comments:

Post a Comment