By Majid Ahmed, Mogadishu
Wakazi wa Mogadishu wanafanya jukumu kubwa katika usafishaji wa mabaki 
ya al-Shabaab katika mji mkuu, maofisa wa usalama wa Somalia wamesema.

Washukiwa wa Al-Shabaab wakipanda katika 
gari ndogo ya wazi ya polisi tarehe 10 Oktoba, mwaka 2012 katika kituo 
cha polisi huko Mogadishu ya kusini. [Abdurashid Abdulle Abikar/AFP]
Fununu kutoka kwa wakazi katika eneo la Yaqshid huko Mogadishu ya 
kaskazini Jumamosi (tarehe 24 Novemba) ilisababisha katika kukamatwa kwa
 washukiwa 21 wa al-Shabaab na ugunduzi wa maficho ya silaha, kwa mujibu
 wa maofisa usalama.
Siku mbili kabla, vikosi vya usalama vilifanya operesheni kutokana na 
fununu kutoka kwa mmiliki wa shamba huko Yaqshid ambayo matokeo yake 
ilikuwa mauaji ya kamanda wa al-Shabaab Abdinur Gardhub . Operesheni ya 
tarehe 22 mwezi Novemba pia ilisababisha kukamatwa kwa wanamgambo 
wengine 16 ambao walifanya shughuli nje ya kikundi kidogo cha watu 
katika maeneo ya Yaqshid, Suqa Holaha na Gubta, kwa mujibu wa kamanda wa
 Idara ya Usalama wa Taifa huko Benadir Koloneli Khalif Ahmed Ereg.
Ereg alisema maficho ya al-Shabaab huko Yaqshid yaligundulika kutokana na taarifa zilizotolewa na wakazi wa eneo hilo.
"Vikosi vya usalama viliwatia kizuizini wanachama 37 wa kikundi cha 
wapinga amani wa al- Shabaab, wakati wa mfululizo wa mashambulizi ya 
usiku yaliyofanywa kitongoji cha kaskazini ya Mogadishu," Ereg aliiambia
 Sabahi. "Mashambulizi haya yalilenga katika usafishaji wa mabaki ya 
al-Shabaab katika eneo hilo."
"Operesheni hizi zilisababisha kunyang'anywa kwa maficho ya aina tofauti
 za silaha ikiwa ni pamoja na silaha za vita, bunduki AK-47, silaha, 
milipuko na maguruneti ya kurusha kwa mkono," alisema.
Ereg alisifu ushirikiano wa wakazi pamoja na vikosi vya usalama. 
"Tunathamini ushirikiano wa raia na vikosi vya usalama wakati wa 
operesheni za hivi karibuni ambazo zilisababisha kukamatwa kwa wanachama
 wa al-Shabaab na ugunduzi wa maficho ya silaha zilizokuwa zinamilikiwa 
na wanamgambo hao," alisema.
Serikali ya Somalia ilitangaza mwishoni mwa mwezi Aprili kwamba ingetoa 
hadi dola 500 kwa wananchi watakaojitokeza na taarifa zitakazosaidia 
kukamatwa au kuuawa kwa wanachama wa al-Shabaab.
Wananchi wapo tayari kusaidia jitihada za usalama
Mzee wa Mogadishu Suleiman Abdullahi alisema kwamba kupigana na 
wanamgambo ambao wanavuruga usalama wa Somalia ni wajibu wa kidini na 
kitaifa.
"Vikosi vya usalama wa taifa, polisi na jeshi wote wanafanya kazi 
inayotakiwa ya kusafisha mji na maeneo yanayozunguka ya wanamgambo," 
aliiambia Sabahi. "Tunawapongeza katika operesheni hii yenye mafanikio 
ambayo italeta utulivu zaidi huko Mogadishu, na tupo tayari kutoa msaada
 kwa vikosi vya usalama."
"Magaidi wanaishi miongoni mwetu na kwa bahati mbaya kuna wale wanaowapa
 kimbilio salama," alisema Abdullahi. "Kama tunataka kuishi kwa utulivu,
 amani na usalama, tunapaswa kushirikiana na vikosi vya usalama ili 
kulinda usalama wetu na pia tunapaswa kutowapa makazi magaidi kwa sababu
 inamaanisha tunajisaliti sisi wenyewe, taifa letu na nchi yetu kwa 
ujumla."
Osman Mohamed, kanali mstaafu wa polisi Somalia, alisisitiza umuhimu wa 
kujenga ujasiri na kushirikiana kati ya wananchi na vikosi vya usalama. 
Alisema hii ni sababu ya msingi katika mafanikio ya jitihada za polisi 
na vikosi vya usalama kuendeleza utulivu huko Mogadishu na maeneo 
mengine yaliyokombolewa hivi karibuni.
"Kuimarisha mawasiliano kati ya wananchi na wafanyakazi wa usalama 
kunachangia kuelekea katika uimarishaji wa imani ya umma kwa vikosi vya 
usalama na kuleta kujisikia kuridhika kwa jitihada zao," Mohamed 
aliiambia Sabahi.
Alisema vikwazo ambavyo vilikuwepo zamani kati ya wananchi na vikosi vya
 usalama sasa havipo tena. "Vikosi vya usalama vimefanikiwa kwa kiwango 
fulani kuiteka mioyo na mawazo ya wananchi kwani watu hawaogopi tena 
vikosi vya usalama na sasa mawasiliano kati ya pande zote yako imara," 
alisema.
Kuendeleza usalama ni wajibu wa pamoja
Kaimu Gavana wa Masuala ya Usalama wa Benadir Warsame Mohamed Hassan 
alisema ushirikiano kati ya vikosi vya usalama na wananchi katika 
kutafuta watu ambao wanavuruga usalama wa umma ni muhimu.
"Shukrani kwa ushirikiano kati ya wananchi na vikosi vya usalama, hali 
ya usalama huko Mogadishu imeboreshwa kwani viwango vya mauaji na 
vitendo vya kuvuruga usalama vimepungua kwa wiki chache zilizopita," 
Hassan aliiambia Sabahi.
Alitoa wito kwa jamii kwa ujumla kuwajibika katika jitihada 
zinazoendelea zinazokusudia kudhibiti usalama na kuendeleza utulivu huko
 Mogadishu.
"Majeshi ya usalama hayawezi kufanya kazi yake ya kuendeleza hali ya 
usalama na kusafisha Mogadishu dhidi ya al-Shabaab bila ushiriki wa 
jamii," alisema. "Kuimarisha usalama ni wajibu wa pamoja na kila mmoja 
anapaswa kuwajibika katika hili."
Hassan alisema operesheni za usalama zingeendelea huko Mogadishu hadi 
mji uwe huru dhidi ya al-Qaeda wanaoshirikiana na wanamgambo wa 
al-Shabaab.
Chanzo sabahionline.com
Chanzo sabahionline.com
 
 

No comments:
Post a Comment