Pages


Photobucket

Wednesday, November 21, 2012

CHADEMA KUTOA MAFUNZO YA M4C KAGERA



CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinatarajia kuzindua mafunzo ya operesheni ya vurguvugu la mabadiliko (M4C) yatakayoanza Novemba 22 mwaka huu hadi Novemba 23 katika Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera. Mafunzo hayo yatatolewa kwa wenyeviti  na makatibu wa vyama hivyo ngazi ya wilaya hadi mkoa yenye lengo la kuleta uongozi bora na kueneza sera sahihi ya chama hicho. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mafunzo na Oganaizesheni, Benson Kigaila alisema mafunzo hayo yamekuwa wakifanywa kwa wanachama wao ili kupata mbinu mbalimbali ya kudai haki na uwajibikaji wa viongozi na wananchi. “Lengo la kutoa mafunzo kwa wenyeviti na makatibu wa vyama vyetu ni pamoja na kuwajengea uwezo wa uwajibikaji, kudai haki zao ili kuleta hamasa kwa Watanzania kushiriki kikamilifu kwenye mchakato wa mabadiliko, jambo ambalo linaweza kuwapa matumaini ya maisha,”alisema Kigaila. Aliongeza kutokana na hali hiyo wanaamini kuwa, mabadiliko hayo yataweza kuleta uhuru wa kweli na kubadili mfumo wa kiutawala, jambo ambalo litaweza kuonyesha mafanikio. Alisema kutokana na hali hiyo, jumla ya watu 64 watashiriki kwenye mafunzo hayo yakiwamo ya darasani na vitendo ili wajumbe hao waweze kusambaza elimu hiyo kwa wananchi katika vijiji na vitongoji,jambo ambalo litaweza kurahisisha ufanyikaji wa mikutano ya hadhara. Alisema mbali na mafunzo hayo, kutakuwa na mikutano ya hadhara itakayotoa mwongozo kwa viongozi hao kuonyesha uelewa wao katika mafunzo hayo, jambo ambalo wanaamini wanaweza kufanikiwa. Kwa mujibu wa Kigaila, Chadema inatarajia kufanya operesheni ya M4C katika mikoa 32 na kwamba operesheni hiyo itakuwa kubwa zaidi ikilinganishwa na zilizowahi kufanyika nchini kwa sababu tayari baadhi ya wajumbe watakuwa na elimu ya kutosha kuhusu zoezi hilo. 
Mwananchi

No comments:

Post a Comment