KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema CCM watazunguka nchi 
nzima lakini majibu yatajulikana 2015 kwani ndiyo utakuwa mwisho wao.
 Pia
 Dk Slaa amesema Chadema hakiyumbishwi na kuahimia CCM kwa waliokuwa 
madiwani wake mkoani  Arusha, na badala yake kinapata nguvu ya kuweza 
kusimamia maadili ya viongozi wake.
Pia
 Dk Slaa amesema Chadema hakiyumbishwi na kuahimia CCM kwa waliokuwa 
madiwani wake mkoani  Arusha, na badala yake kinapata nguvu ya kuweza 
kusimamia maadili ya viongozi wake.
Dk Slaa alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na gazeti hili kuhusu 
mambo mbalimbali ya kisiasa yanayoendelea nchini, ikiwa ni siku moja 
tangu uongozi wa juu wa CCM ukiongozwa na Katibu Mkuu wake, Abdulrahaman
 Kinana umalize ziara yake ya kwanza katika Mikoa ya Mtwara, Rukwa, 
Geita na Arusha.
Alisema Chadema siku zote kitabaki kuwa mwalimu na vyama vingine vitafuata kwa kuiga mambo ambayo chama hicho kimeyaanzisha.
“CCM kuzunguka huku na huko na ni kutuiga sisi kwani tumeanza muda 
mrefu, baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 tumekuwa tukizunguka na 
kuwaeleza wananchi mambo mbalimbali,” alisema Dk Slaa na kuongeza; “Wao 
(CCM) wazunguke tu lakini mambo yote yatajulikana 2015 kwani Watanzania 
wa sasa siyo wa kudanganywa tena.”
Dk Slaa alisema anashangaa kwa nini CCM wanazunguka huku wakilalamika 
wakati wao ndiyo wanaiongoza nchi hivyo majibu ya matatizo ya wananchi 
wanayo.“Chadema ni mwalimu na wao hufuata, waendelee na mzunguko wao 
lakini waache kulalamika kama sisi bali watoe majibu kwa kuwa wao ndiyo 
wanaongoza Serikali,”alisema Dk Slaa.
Akizungumzia baadhi ya madiwani wa chama hicho waliohamia CCM, Dk Slaa 
alisema kuwa hawakiyumbisha chama chao na kwamba hata kama wamehama 
wasipolipa Sh15 milioni kama amri ya mahakama ilivyotolewa watakwenda 
jela.
Juzi katika mkutano wa CCM Arusha, madiwani wa Chadema walitangaza 
kujiunga na CCM huku wakipinga hatua ya Dk Slaa, kuwa alikuwa akitaka 
kuwafunga baada ya kuwatimua ndani ya chama hicho.
Madiwani hao ambao walitimuliwa na Chadema kutokana kitendo chao cha 
kumtambua Meya wa Jiji la Arusha Gaudensi Lyimo wa CCM ni Rehema 
Mohamed, Simba Salum wa Kata ya Kati na Frank Joseph Takachi wa Kata ya 
Olasiti.
Jana Dk Slaa alisema kitendo hicho kinaonyesha jinsi gani kuna wanasiasa
 ambao ni matapeli hapa nchini kwani madiwani hao walikwenda mahakamani 
kutaka warudishiwe uanachama wao sasa wamekimbilia  CCM. 
“Watanzania sasa wanajua aina ya wanasiasa matapeli, kama walienda 
mahakamani kuomba uanachama wanahangaika nini,”alisema Dk Slaa na 
kuongeza; “Chama hakitayumba na tutaendelea kusimamia maadili ndani 
chama kama ilinavyotakiwa.” 
Alisema baadhi ya madiwani wameshaanza kulipa fedha ambazo mahakama 
imesema, hivyo hao waliokimbilia CCM wasipolipa fedha hizo ndani ya 
miezi miwili watakwenda jela kama mahakama ilivyosema.
NCCR wanena
Katika hatua nyingine Chama cha NCCR-Mageuzi kimemtaka Makamu Mwenyekiti
 wa CCM, Tanzania Bara,  Philip Mangula kushughulikia rushwa ndani ya 
chama hicho kwa muda wa siku saba na siyo miezi sita kama alivyoahidi.
Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho, Faustin Sungura amesema vinginevyo 
chama hicho kitawahamasisha wananchi waikatae CCM katika Uchaguzi Mkuu 
wa 2015.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Sungura alisema wahusika wa 
rushwa wanafahamika na ametoa siku hizo kutokana na kuona miezi sita ni 
mingi na watendaji wa vitendo hivyo wanafahamika katika chama na 
Serikali na kwamba kinachokosekana ni dhamira ya dhati ya kuchagua 
viongozi wenye mikono safi.
Chanzo Mwananchi
 
 

No comments:
Post a Comment