Pages


Photobucket

Friday, November 30, 2012

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROF. MUHONGO AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UJERUMANI



Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akiwa pamoja na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Klaus-Peter Brandes mara alipomtembelea Profesa Muhongo ofisini kwake. Balozi huyo aliongozana na watendaji kutoka kampuni ya Koch Engineering & Construction ya nchini Ujerumani ambao wanania ya kuwekeza katika miradi ya nishati ikiwamo gesi asilia, umeme wa upepo, jua pamoja na kuwekeza katika viwanda vya uzalishaji mbolea.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akimuonesha Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Klaus-Peter Brandes ramani ya bomba la kusafirisha gesi asili kutoka Mnazi Bay Mtwara na Songosongo hadi Dar es Salaam. Profesa Muhongo alimueleza mheshimiwa Balozi kuwa Serikali ina mpango wa kuzalisha umeme kwa njia ya gesi katika eneo la Somangafungu.

 Picha na Afisa Habari Wizara ya Nishati na Madini.

No comments:

Post a Comment