Watu wawili wanadaiwa wamefariki dunia na wengine watatu wamejeruhiwa baada ya kupigwa na watu wanadaiwa kuwa ni askari wa JWTZ.
Akizungumzia tukiohilo  kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya DIWANI ATHUMAN amesema 
katika vurugu hizo mtu mmoja ndiye aliyeripotiwa amefariki dunia hadi 
saa ambaye naye bado hajafahamika mara moja na kuongeza kuwa wengine 
watatu wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Ifisi Mbeya.
hata
 hivyo habari kutoka eneo la Tukio zinadai kuwa Novembeer 17 majira ya 
saa tano za usiku ktk eneo la DDC mbalizi walinzi wakiwa kwenye doria 
zao za maduka walimsimamisha askari mmoja wa JWTZ kisha kuanza kumpiga 
hali iliyopelekea maumivu makali na kukimbilia kwenye kituo cha polisi 
Mbalizi kwa ajili ya kutoa taarifa.
Badaa
 ya kufika ktk kituo hicho alipewa huduma mara moja ambapo askari hao 
waliondokana kwenda eneo la tukio na kuanza kufanya msako wa watu 
waliohusika hata hivyo usiku hawakufankiwa kumkamata hata mmoja.
siku
 inayofuata askari hao walifanikiwa kuwakamata walinzi watano na kuanza 
uchunguzi mara moja ambapo siku hiyohiyo majira ya saa tano za usiku 
askari wa JWTZ walivamia eneo hilo na kuanza kutembeza kipigo kwa 
wananchi waliokuwa eneo hilo ambapo kutokana na vurumai hizo watu wawili
 waliumia vibaya na wengine kujeruhiwa.
aidha
 watu hao walipelekwa ktk hospital ya Ifisi ambapo majira ya saa 5 siku hiyo
 hiyo wawili kati ya hao waliokuwa wamepigwa walifariki dunia.
Hata
 hivyo RPC DIWANI alisema kuwa uchunguzi unaendelea kwa ushirikiano wa 
Polisi na JWTZ kuwapata waliohusika na tukio hilo la uvunjifu wa sheria. 
 Habari Chimbukoletu Blog.
 
 


No comments:
Post a Comment