Pages


Photobucket

Wednesday, November 21, 2012

Djibouti inakabiliwa na kuongezekwa kwa changamoto ya wakimbizi



Makambi ya Ali Addeh na Holl-Holl huko Djibouti ni makaazi ya wakimbizi wanaokadiriwa kufikia 25,000 pamoja na kuwa na changamoto kwa maofisa wa serikali na mashirika ya kimataifa.

Awali ilijengwa kuwahifadhi watu 7,000, kambi ya wakimbizi ya Ali Addeh huko Djibouti ambayo sasa inawahifadhi wakimbizi 20,000, wengi wako katika mahema ya muda. [Harbi Abdillahi Omar/Sabahi]

Hali ya wakimbizi huko Djibouti inabakia kuwa ya wasiwasi. Ukosefu wa maji ya kunywa, utokeaji tena wa ukame, utapiamlo na uhaba wa chakula vimefanya mchakato wa kuchanganyikana kwao kuwa mgumu, kwa mujibu wa Aden Hassan wa Ofisi ya Taifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani kwa ajili ya Msaada wa Wakimbizi na Watu wasio na Makaazi (ONARS), ambayo inasimamia makambi hayo.

Kambi ya Ali Addeh, ambayo kwa sasa ni kambi kubwa ya wakimbizi huko Djibouti, ilifungua milango yake mwaka 1991 baada ya serikali kuu ya Somalia kuanguka. Ilijengwa kuwahifadhi wakimbizi 7,000, lakini kwa sasa inawahifadhi kama 20,000.

Mwezi Disemba 2013, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) alikadiria kuwepo kwa wakimbizi zaidi ya 30,000 wanaoishi Djibouti.

Katika jitihada za kupunguza msongamano, UNHCR na ONARS ilitaka serikali kufungua tena kambi ya Holl-Holl, ambayo ilifungwa 2006. Ilifunguliwa tena Juni 2012 na sasa inawahifadhi wakimbizi zaidi ya 1,000.

Ingawaje baadhi ya wakimbizi huko Djibouti wamesema wanataka kurudi nyumbani mara nchi zao zikiwa na utulivu, wengi wangependelea kuhamishiwa tena katika nchi ya tatu. Hadi mwaka huu, UNHCR iliwasaidia kuhamishwa wakimbizi 225 huko Marekani, Uswidi, Kanada na nchi nyingine, idadi iliyozidi 117 ya mwaka 2011.

Karibu asilimia 90 ya wakimbizi wa nchi wanatokea Somalia pamoja na wanaobakia wengi wao kutokea Eritrea na Ethiopia.

Wakimbizi wakabiliwa na maisha magumu kambini

Abdi Maalin, mkimbizi wa Somalia akiwa na miaka 30, amekuwa akiishi katika kambi za Ali Addeh kwa miaka mitano. Aliiambia Sabahi kwamba japokuwa al-Shabaab wamedhoofishwa, Somalia bado hakupo salama na anamatumaini ya kufaidi kutokana na mpango wa uhamishaji.

"Leo sina uwezo wa kuendelea na masomo yangu ya chuo kikuu na siwezi kufanya kazi nchini Djibouti kwa sababu sina kitambulisho chochote," Maalin alisema. Alisema watu wote wazima waliopo kambini wanakubwa na ukosefu wa ajira na kukosa shughuli za kuwaingizia kipato.

Omar Idleh, mshauri katika Wizara ya mambo ya Ndani, alisema kuna mahitaji ya kuongeza idadi ya vituo vya kupokelea wakimbizi na kuwafundisha mtu mmojammoja kushughulikia vizuri wahamiaji katika mateso.

"Nchi yetu inakabiliwa na wimbi kubwa la wakimbizi wanaoingia kutoka mikoa tunayopakana nayo ya majirani zetu wa karibu katika majaribio ya kufika rasi ya Uarabuni, ambako wanakuona kama El Dorado, hata kama katika baadhi ya matukio inaweza kuwagharimu maisha," Idleh aliiambia Sabahi.

"Kuwepo kwao katika nchi yetu ni mzigo mkubwa ambao unaleta ushiriki wao katika uchafuzi, uharibifu na uchafu unaoharibu usalama wa mazingira ya nchi nzima," alisema.

Amina Youssouf, mjane na mama wa watoto watatu mwenye umri wa miaka 42, ambaye ameishi miaka 10 katika kambi ya Ali Addeh, alisema atahamia Kanada mwaka 2013.

"Leo, sina mtu yeyote nchini Somalia," aliiambia Sabahi. "Wapendwa wangu walifariki au kuhama nchini. Kwa hiyo kwa nini nihatarishe maisha yangu na watoto wangu kwa kurejea tena?"

Alisema maisha katika kambi za wakimbizi yamekuwa ni mapambano zaidi ya kukosa umeme na maji. "Watoto wangu hawakupata na elimu kwa sababu shule ya msingi huko Holl-Holl imejengwa mwezi Septemba tu na iliyopo huko Ali Addeh ina miaka minne tu," alisema.

Hata kama kungekuwa na shule, alisema, hakuwa na kitambulisho muhimu cha kuandikishia watoto wake shule.

"Ni mwezi Mei tu Shirika la Watoto la UN lilitambulisha vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wanaozaliwa, na uongozi huko Ali-Sabieh, ambao unachukua kambi mbili za wakimbizi, lilianzisha vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa wakimbizi wenye umri wa chini ya miezi minne, pamoja na sheria za nyongeza kuwalinda wote wenye umri wa zaidi ya miezi minne," alisema.

Uhamiaji haramu pia ni hatari
Mahali ilipo Djibouti katika Bahari ya Shamu na ukaribu na Mashariki ya Kati pia vinafanya uhamiaji haramu kuwa tatizo kuu kwa viongozi wa Djibouti.

Ingawa sheria za Djibouti zinaruhusu wakimbizi kufanya kazi nchini, kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira na tatizo la chakula cha nchini havisaidii mchanganyiko, Mkurugenzi Msaidizi wa ONARS Aden Hassan aliiambia Sabahi. "Sehemu kubwa ya vijana na wakimbizi wa muda mrefu ambao wanageuka kuwa wahamiaji haramu kwa sababu ya kutokuwa na mafunzo na elimu na kwa sababu ya hali ngumu ya maisha."

Mwezi Agosti, UNHCR iliripoti kwamba uingiaji wa wakimbizi na wahamiaji kutoka Pembe ya Afrika kwenda Yemen umevunja rekodi ya zaidi ya 63,800 katika miezi saba ya mwanzo ya 2012, ongezeko la asilimia 30 kutoka rekodi ya awali mwaka 2011, wakati jumla ya wakimbizi 48,700 walivuka mpaka.

Mkimbizi mmoja kati ya sita waliyovuka mpaka walikuwa Wasomali wakati wengine walio wengi walikuwa Waethiopia. Idadi kubwa ya wakimbizi walivuka kutoka mji wa bandari ya Djibouti wa Obock, UNHCR ilisema, pamoja na ukumbusho kutoka mikoa ya Somaliland na Puntland ya Somalia.

No comments:

Post a Comment