Makambi ya Ali Addeh na Holl-Holl huko Djibouti ni makaazi ya wakimbizi 
wanaokadiriwa kufikia 25,000 pamoja na kuwa na changamoto kwa maofisa wa
 serikali na mashirika ya kimataifa.

Awali ilijengwa kuwahifadhi watu 7,000, 
kambi ya wakimbizi ya Ali Addeh huko Djibouti ambayo sasa inawahifadhi 
wakimbizi 20,000, wengi wako katika mahema ya muda. [Harbi Abdillahi 
Omar/Sabahi]
Hali ya wakimbizi huko Djibouti inabakia kuwa ya wasiwasi. Ukosefu wa 
maji ya kunywa, utokeaji tena wa ukame, utapiamlo na uhaba wa chakula 
vimefanya mchakato wa kuchanganyikana kwao kuwa mgumu, kwa mujibu wa 
Aden Hassan wa Ofisi ya Taifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani kwa ajili ya 
Msaada wa Wakimbizi na Watu wasio na Makaazi (ONARS), ambayo inasimamia 
makambi hayo.
Kambi ya Ali Addeh, ambayo kwa sasa ni kambi kubwa ya wakimbizi huko 
Djibouti, ilifungua milango yake mwaka 1991 baada ya serikali kuu ya 
Somalia kuanguka. Ilijengwa kuwahifadhi wakimbizi 7,000, lakini kwa sasa
 inawahifadhi kama 20,000.
Mwezi Disemba 2013, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi 
(UNHCR) alikadiria kuwepo kwa wakimbizi zaidi ya 30,000 wanaoishi 
Djibouti.
Katika jitihada za kupunguza msongamano, UNHCR na ONARS ilitaka serikali
 kufungua tena kambi ya Holl-Holl, ambayo ilifungwa 2006. Ilifunguliwa 
tena Juni 2012 na sasa inawahifadhi wakimbizi zaidi ya 1,000.
Ingawaje baadhi ya wakimbizi huko Djibouti wamesema wanataka kurudi 
nyumbani mara nchi zao zikiwa na utulivu, wengi wangependelea 
kuhamishiwa tena katika nchi ya tatu. Hadi mwaka huu, UNHCR iliwasaidia 
kuhamishwa wakimbizi 225 huko Marekani, Uswidi, Kanada na nchi nyingine,
 idadi iliyozidi 117 ya mwaka 2011.
Karibu asilimia 90 ya wakimbizi wa nchi wanatokea Somalia pamoja na wanaobakia wengi wao kutokea Eritrea na Ethiopia.
Wakimbizi wakabiliwa na maisha magumu kambini
Abdi Maalin, mkimbizi wa Somalia akiwa na miaka 30, amekuwa akiishi 
katika kambi za Ali Addeh kwa miaka mitano. Aliiambia Sabahi kwamba 
japokuwa al-Shabaab wamedhoofishwa, Somalia bado hakupo salama na 
anamatumaini ya kufaidi kutokana na mpango wa uhamishaji.
"Leo sina uwezo wa kuendelea na masomo yangu ya chuo kikuu na siwezi 
kufanya kazi nchini Djibouti kwa sababu sina kitambulisho chochote," 
Maalin alisema. Alisema watu wote wazima waliopo kambini wanakubwa na 
ukosefu wa ajira na kukosa shughuli za kuwaingizia kipato.
Omar Idleh, mshauri katika Wizara ya mambo ya Ndani, alisema kuna 
mahitaji ya kuongeza idadi ya vituo vya kupokelea wakimbizi na 
kuwafundisha mtu mmojammoja kushughulikia vizuri wahamiaji katika 
mateso.
"Nchi yetu inakabiliwa na wimbi kubwa la wakimbizi wanaoingia kutoka 
mikoa tunayopakana nayo ya majirani zetu wa karibu katika majaribio ya 
kufika rasi ya Uarabuni, ambako wanakuona kama El Dorado, hata kama 
katika baadhi ya matukio inaweza kuwagharimu maisha," Idleh aliiambia 
Sabahi.
"Kuwepo kwao katika nchi yetu ni mzigo mkubwa ambao unaleta ushiriki wao
 katika uchafuzi, uharibifu na uchafu unaoharibu usalama wa mazingira ya
 nchi nzima," alisema.
Amina Youssouf, mjane na mama wa watoto watatu mwenye umri wa miaka 42, 
ambaye ameishi miaka 10 katika kambi ya Ali Addeh, alisema atahamia 
Kanada mwaka 2013.
"Leo, sina mtu yeyote nchini Somalia," aliiambia Sabahi. "Wapendwa wangu
 walifariki au kuhama nchini. Kwa hiyo kwa nini nihatarishe maisha yangu
 na watoto wangu kwa kurejea tena?"
Alisema maisha katika kambi za wakimbizi yamekuwa ni mapambano zaidi ya 
kukosa umeme na maji. "Watoto wangu hawakupata na elimu kwa sababu shule
 ya msingi huko Holl-Holl imejengwa mwezi Septemba tu na iliyopo huko 
Ali Addeh ina miaka minne tu," alisema.
Hata kama kungekuwa na shule, alisema, hakuwa na kitambulisho muhimu cha kuandikishia watoto wake shule.
"Ni mwezi Mei tu Shirika la Watoto la UN lilitambulisha vyeti vya 
kuzaliwa kwa watoto wanaozaliwa, na uongozi huko Ali-Sabieh, ambao 
unachukua kambi mbili za wakimbizi, lilianzisha vyeti vya kuzaliwa kwa 
watoto wa wakimbizi wenye umri wa chini ya miezi minne, pamoja na sheria
 za nyongeza kuwalinda wote wenye umri wa zaidi ya miezi minne," 
alisema.
Uhamiaji haramu pia ni hatari
Mahali ilipo Djibouti katika Bahari ya Shamu na ukaribu na Mashariki ya 
Kati pia vinafanya uhamiaji haramu kuwa tatizo kuu kwa viongozi wa 
Djibouti.
Ingawa sheria za Djibouti zinaruhusu wakimbizi kufanya kazi nchini, 
kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira na tatizo la chakula cha nchini 
havisaidii mchanganyiko, Mkurugenzi Msaidizi wa ONARS Aden Hassan 
aliiambia Sabahi. "Sehemu kubwa ya vijana na wakimbizi wa muda mrefu 
ambao wanageuka kuwa wahamiaji haramu kwa sababu ya kutokuwa na mafunzo 
na elimu na kwa sababu ya hali ngumu ya maisha."
Mwezi Agosti, UNHCR iliripoti kwamba uingiaji wa wakimbizi na wahamiaji 
kutoka Pembe ya Afrika kwenda Yemen umevunja rekodi ya zaidi ya 63,800 
katika miezi saba ya mwanzo ya 2012, ongezeko la asilimia 30 kutoka 
rekodi ya awali mwaka 2011, wakati jumla ya wakimbizi 48,700 walivuka 
mpaka.
Mkimbizi mmoja kati ya sita waliyovuka mpaka walikuwa Wasomali wakati 
wengine walio wengi walikuwa Waethiopia. Idadi kubwa ya wakimbizi 
walivuka kutoka mji wa bandari ya Djibouti wa Obock, UNHCR ilisema, 
pamoja na ukumbusho kutoka mikoa ya Somaliland na Puntland ya Somalia.
 
 

No comments:
Post a Comment