Pages


Photobucket

Friday, November 30, 2012

Mwendesha mashtaka Korea Kusini ajiuzulu

Mwendesha mashtaka mkuu nchini Korea Kusini amejiuzulu, baada ya kuomba msamaha hadharani kushusiana na kashfa kadhaa katika idara yake.
Han Sang-dae alisema matukio hayo, yaliyowahusisha maafisa chini ya usimamizi wake, yaliwashangaza na kuwavunja moyo watu wengi nchini humo.
Katika kisa kimoja, ofisa wa ngazi ya juu ameshtakiwa kwa kupokea rushwa, huku mwingine ameshtakiwa kwa kupunguza adhabu ya mshukiwa fulani na badala yake kuomuomba wawe wapenzi.

Chanzo ni BBC

No comments:

Post a Comment