Pages


Photobucket

Tuesday, December 11, 2012

WIZARA YA NISHATI NA MADINI YAJIPANGA KUWAINUA WACHIMBAJI WADOGO


Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (wa kwanza kushoto), na Naibu wake Mhe. Stephen Masele wakishiriki katika mkutano mkuu wa mwaka wa wachimbaji wadogo wa madini uliofanyika hivi karibuni mjini Dodoma.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Mhe. Stephen Masele akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa wachimbaji wadogo wa madini nchini, uliofanyika mjini Dodoma hivi karibuni.

Uongozi wa mpito kitaifa wa Chama cha Wachimbaji Wadogo wa Madini mara baada ya kuchaguliwa na mkutano wao mkuu wa mwaka uliofanyika hivi karibuni mjini Dodoma.

Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (wa kwanza kushoto), na Naibu wake Mhe. Stephen Masele wakishiriki katika mkutano mkuu wa mwaka wa wachimbaji wadogo wa madini uliofanyika hivi karibuni mjini Dodoma.

Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (katikati) katika picha ya pamoja na makamishna wasaidizi wa madini kutoka kanda mbalimbali, mara baada ya kufunga mkutano mkuu wa mwaka wa wachimbaji wadogo wa madini uliofanyika hivi karibuni mjini Dodoma.


Wizara ya Nishati na Madini imetenga jumla ya shilingi bilioni 8.9 kwa dhamira ya kuwainua wachimbaji wadogo wa madini nchini ili kukuza kipato chao na hivyo kuboresha maisha yao.

Aidha, jitihada za kuwainua wachimbaji wadogo zinalenga pia kuinua pato la taifa kutokana na kuongezeka kiwango cha kodi na tozo mbalimbali zinazopaswa kulipwa na wachimbaji hao kwa serikali.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo alipokuwa akizungumza na wajumbe waliohudhuria mkutano mkuu wa mwaka wa wachimbaji wadogo wa madini nchini, uliofanyika mjini Dodoma tarehe sita na saba mwezi huu.

No comments:

Post a Comment