Pages


Photobucket

Saturday, December 15, 2012

Rais Wa Madagascar Awasili Nchini




 
Rais wa Madagascar, Mheshimiwa Andry Rajoelina ambaye amewasili mjini Dar es Salaam mchana jana Ijumaa, Desemba 14 kwa ziara ya kikazi ya siku mbili nchini akiwa  na mwenyeji wake,  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Ikulu, tayari kuanza mazungumzo rasmi.
Rais Kikwete ni Mwenyekiti wa Tume ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo amepewa jukumu na viongozi wenzake ndani ya Jumuiya hiyo kukutana na viongozi wa Madagascar kuwaelezea maamuzi ya mkutano wa viongozi hao wa SADC uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dar Es Salaam.Kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, mwanzoni mwa wiki hii, Mheshimiwa Ravalomanana alithibitisha kuwa amekubaliana na maamuzi ya viongozi wa SADC. 
Miongoni mwa mambo mengine, viongozi hao wa SADC wanataka viongozi hao wawili wa Madagascar washawishiwe na wakubali kutogombea katika Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika nchini humo mwakani.

No comments:

Post a Comment