Pages


Photobucket

Friday, December 21, 2012

Waziri Wa Habari Zanzibar Azindua Bodi Ya Tume Ya Utangazaji Zanzibar


Na: Ali Issa Maelezo Zanzibar
Waziri wa Habari Utamaduni, utalii na Michezo Zanzíbar Saidi Ali Mbaruok amesema wakati umefika sasa kwa wandishi wa habari wa Zanzíbar kupata nafasi ya kwenda nchi za nje kuitangaza Zanzíbar kiutalii kila itapo fanyika Maonyesho, makongamano na mikutano ya utalii duniani. 

Hayo ameyasema leo huko Ofisini kwake Wizara ya Habari Utamaduni, Utalii na Michezo kikwajuni wakati alipo kutana na wajumbe wa Bodi ya ushauri wa magazeti na majarida walio fika ofisini kwake kwa kujitambulisha. 
Amesema kua ni vyema kwa waandishi wa habari kwenda kuandika habari zinazi huso utalii na zaidi pale Zanzíbar inapo shiriki katika maonesho ya kimataifa nyanayo mfanyika katika nchi mbalimbali ili kuutangaza utalii wake . 
“Wandishi kupata frusa hii ya kwenda nje kuitangaza Zanzíbar kiutalii ni jambo zuri na linalo kubalika kwani tume shuhudia kuona wandishi wahabari kutoka nchi mbali mbali duniani wana tangaza nchizao na sioni haja kwanini sisi tusifanye hivyo kwani asilimia kubwa za fedha za kigeni za Zanzíbar hupatikana kwajia hiyo.
Alisema kuwa wandishi ni hakiyao kwenda na hakuna sababu kua wasende kwani watacho kifanya wao ni maendeleo ya taifa lao kijumla na wataweza kuitangaza Zanzíbar kwa njia pana na kuweza kueleweka zaidi utalii na hatimae kufaidika. 
Nae Mwenyekiti wa Bodi hiyo ambae pia ni Mshauri wa Rais wa masuala ya utalii Issa Ahmed Othuman mapema akimkaribisha waziri alisema kua maonyesho ya utalii yajayo kuazia ni vizuri kwa mwandishi wa Habari akawemo katika katika msafara utakao shiriki katika maonesho yatakayo katika nchi yoyte Duniani. 
“Naahidi waandishi wahabari watakuwemo kila safari kwa kuitangaza Zanzíbar kiutalii na nitaazia safari ya ujerumani”.alisema Issa Ahamed.
Aidha mwenyekiti huyo alima kua atakuwa pamoja na waziri kuona kua bajeti maalumu inawekwa ilikuhakikisha kua wandishi wanapata fursa ya kushiriki kikamilifu katika maonesho yote ya utalii yanayo fanyika ndani na nje ya nchi kwa miajili ya kuitangaza zaidi Zanzíbar kiutalii.
Wakati huo huo waziri wa habari Utamaduni ,Utalii na Michezo Said Ali Mbaruok amezindua Bodi ya Tume ya Utangazaji Zanzíbar huko katika Ofisi za Tume ziliopo kikwajuni Zanzíbar .
Waziri ameitaka bodi hiyo kuwa makini katika kusajili vyombo vya redio na Televisheni kwa mustakbali wakuwa na vyombo bora vyenyekuelimisha jamii na kuondokana na vyombo vitakavyo leta mfarakano nchini . 
Bodi hiyo ipo chini ya Mwenyekiti wake Abdalla Mwinyi Khamis ambae pia Mkuu wa Mkoa Mjini Maghari Unguja iliteuliwa hivi karibuni ambapo Rais wa Zanzíbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi alimteua Mwenyekiti na wajumbe kuteuliwa na Waziri.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment