Pages


Photobucket

Friday, December 28, 2012

Madereva wa bodaboda wa kike wavunja vikwazo vya kijinsia Kenya


Na Bosire Boniface, Garissa

Picha ya teksi ya pikipiki ya Faith Kabura Makena kwenye barabara za Garissa nchini Kenya inatoa taswira ya nadra sana.

Grace Ruwa Asar, mwanamke wa kwanza kuwa dereva wa bodaboda Kenya, akimbeba abiria kwenye eneo la Tana River Delta. [Bosire Boniface/Sabahi]

Makena, mwenye umri wa miaka 30, alisema anajua kwamba kuchagua kwake biashara hii kumesababisha utata na mara kadhaa huwashangaza wakaazi wa huko anapowapita.

Teksi za pikipiki, zinazojulikana kama bodaboda nchini Kenya, ni njia maarufu ya usafiri kwa wasafiri wanaotaka kukwepa foleni kubwa za magari mijini. Wakati inatoa fursa ya kupata maisha mazuri kwa waendeshaji wake, hii ni biashara ambayo imekuwa ikitawaliwa na wanaume tu.

Hata hivyo, Makena alisema aliamua kuipa changamoto imani iliyopo na kuwa dereva wa bodaboda kwa sababu ni chanzo kizuri cha mapato ya kumuhudumia mtoto wake wa kiume wa miaka 6 na wazazi wake, ambao ana jukumu la kuwatunza kifedha.

"Mwanzoni nilikuwa ninakerwa na namna watu walivyonichukulia lakini kutokana na uungaji mkono wa familia yangu na marafiki, nilisonga mbele," aliiambia Sabahi. "Wiki za mwanzo zilikuwa ngumu kwa sababu sikuweza kupata wateja. Mteja mmoja hata aliwahi kuniambia kwamba nilikuwa ninatania na asingeliweza kuamini usalama wake barabarani kwenye mikono ya dereva mwanamke."

Faith Kabura Makena alivunja kikwazo cha kijinsia kwa madereva wa kike wa bodaboda mjini Garissa. [Bosire Boniface/Sabahi]

Makena alisema kwamba binamu yake alimfundisha kuendesha pikipiki kwa nia ya kujifurahisha tu. "Kutokana na uchache wa ajira, ilinipitikia kwamba kile nilichojifunza kwa kujifurahisha kinaweza kuwa fursa za kuzalisha kipato," alisema.

Makena, ambaye mwanzoni alikuwa akimiliki duka, amekuwa dereva tangu mwezi Januari, akiwa kwa wastani anapata shilingi 20,000 (dola 233) kwa mwezi. Kwa sasa anafanya kazi na dereva mwingine lakini anatarajia kuweka akiba hadi shilingi 80,000 (dola 931) kufikia mwezi Februari ili aweze kununua pikipiki yake mwenyewe na kuwa dereva anayejitegemea.

Lengo lake kuu, hata hivyo, ni kuwa mwalimu wa sekondari ya juu. Makena alisema amekuwa akiweka fedha kila mwezi kulipia shule, ambako ataanza mwezi Juni ujao.

No comments:

Post a Comment