Pages


Photobucket

Saturday, December 29, 2012

Marekani yafunga ubalozi wake nchini Jamhuri ya Afrika ya kati, Ufaransa yagoma kutoa msaada


Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Francois Bozize
Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Francois Bozize
Na Sabina Chrispine Nabigambo
Marekani imeondoa ubalozi wake katika nchi ya Jamhuri ya Kati wakati huu ambapo kiongozi wa taifa hilo ameomba msaada wa kijeshi kwa Ufaransa na Marekani baada ya waasi kudhibiti miji kadhaa nchini humo.
Jana Marekani ilisema kuwa imeondoa mabalozi wake nchini humo na kusitisha utendaji wake kwa muda na kwamba haijavunja uhusiano wa kidiplomasia na serikali ya nchi hiyo ingawa imewaonya raia wake kutosafiri kuelekea nchini humo wakati huu machafuko yakiendelea.
Umoja wa mataifa pia umeanza kuwaondoa wafanyakazi wake huku wapiganaji waasi wamepiga hatua kuingia katika mji mkuu Bangui na kuamsha hofu kwa wakazi wa mji huo.
Aidha rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema kuwa nchi yake haitatumia vikosi vyake kuingilia mzozo unaoendelea nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati huku akisisitiza kuwa uwepo wao nchini humo si kwa lengo la kulinda serikali bali kulinda na kutetea maslahi yao.
Rais Francois Bozize ameomba mataifa yenye nguvu ikiwa ni pamoja na Ufaransa na Marekani kuisadia kijeshi ili kudhibiti waasi wanaoendelea kupig a hatua kuingia mji wa Bangui huku akitaka pia msaada wa kufanikisha mazungumzo ya kutatua mzozo huo mjini Libreville.

Chanzo-kiswahili.rfi.fr

No comments:

Post a Comment