Pages


Photobucket

Friday, December 14, 2012

Suzan Rice ajitoa kuwania Uwaziri wa Mambo ya nje Marekani.


Mjumbe maalumu wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa Suzan Rice ambaye pia ni mtu wa karibu wa Rais Barack Obama wa Marekani amejitoa katika orodha ya watu wanaotazamiwa kuchukua nafasi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo.

Bi. Rice amekuwa akikabiliwa na shutuma kali kutoka kwa wafuasi wa chama cha Republican kutokana na kauli aliyoitoa baada ya kutokea kwa mashambulizi dhidi ya ubalozi mdogo wa Marekani mjini Benghazi, Libya tarehe 11 Septemba mwaka huu ambayo yalisababisha vifo vya maafisa wanne akiwemo Balozi Chris Stevens.

Katika barua aliyomuandikia Rais Obama, Bi. Rice amemweleza kiongozi huyo kuwa anathamini heshima aliyopewa ya kuwa mmoja wa watu wanaotazamiwa kushika nafasi ya waziri wa mambo ya nje, lakini akasema kuwa anaamini kama atateuliwa, hatua hiyo inaweza kuambatana na mtafaruku wa kisiasa.

Chanzo: dewjiblog.com

No comments:

Post a Comment