Pages


Photobucket

Monday, December 31, 2012

MAZISHI YA MWANAFUNZI WA UDAKTARI ALIYEBAKWA NCHINI INDIA YAFANYIKA








Hatimaye mazishi ya mwanafunzi wa Udaktari aliyefariki jana jumamosi katika hospitali ya Mount Elizabeth nchini Singapore yamefanyika huko India. Juhudi za Madaktari kuokoa maisha yake zilishindikana kutokana na kuathiriwa zaidi na unyama aliofanyiwa na kundi la wanaume sita katikati ya mwezi huu.

Maombolezo nchini India

Mwili wa mwanamke huyo aliyekuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu tayari uliwasili nyumbani mapema leo asubuhi na kupokelewa kwa heshima kubwa ambapo Waziri Mkuu wa India Manmohan Singh naye alikuwepo katika mapokezi hayo.

Maelfu ya raia nchini India jana jumamosi waliendelea kukusanyika katika mji mkuu New Delhi wakiwa na mishumaa kama ishara ya maombolezo ya kifo cha mwanafunzi huyo aliyebakwa ndani ya basi katikati ya mwezi huu.

Kwa takribani majuma mawili kumekuwa na ghasia kubwa nchini humo waandamanaji wakipinga unyanyasaji dhidi ya wanawake na kutaka adhabu ya kifo itekelezwe kwa wanaotuhumiwa kwa tukio hilo.

Wanaume sita wanaoshikiliwa kwa kufanya unyama huo sasa wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya binti huyo aliyefariki jana asubuhi katika hospitali ya Mount Elizabeth nchini Singapore ambako alipelekwa kwa matibabu zaidi.
 

No comments:

Post a Comment