Pages


Photobucket

Thursday, September 19, 2013

SEMINA YA BLOGGERS NA MITANADAO MINGINE YA JAMII WAMALIZA SEMINA YAO LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma, akifunga semina ya Wamiliki wa Blog na Wasimamizi wa Mitandao ya Jamii, baada ya semina hiyo kumalizika leo, Makao Makuu ya TCRA, Dar es Salaam,  Semina hiyo iliyoandaliwa  na TCRA kuboresha weledi wa Wanahabari hao, ilianza jana, ambapo wataalam mbalimbali wakiwemo kutoka Kampuni ya Google na Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Shule ya Uandishi wa habari, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, walitoa mada moto moto ambazo bila shaka zimewaongezea ujuzi wanahabari hao.
 MKurugenzi wa TCRA, Profesa John Nkoma akimkabishi cheti cha kuhitimu semina hiyo, Mmiliki na Mtayarishaji Mkuu wa theNkoromo Blog.
    Mmiliki wa Habari Mseto Blogu, Francis Dande akipokea cheti chake
 Othman Michuzi kutoka Michuzi Media, akipokea cheti cha kushiriki semina hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano TCRA Innocent Mungy.
 Mwanadada huyu ambaye pia ni Blogger mahiri akipokea cheti chake
 Sambaya kutoka Tanuru la Fikra akipokea cheti chake
 Blogger Doto Kahidni akipokea cheti chake
 Mwana Mtandao, Magnus Mahenge akipokea cheti chake
 Mroki Mroki wa Father Kidevu Blogu akipokea cheti chake
 Muhidin Sufiani wa Sufiani Mafoto akipokea cheti chake
 Sufian akikifurahia cheti chake
 Henry Mdimu maarufu kama Nzee la Nyeti, akipokea cheti chake
 John Badi wa Daily Mitikasi Blog akipokea cheti chake
 Mike wa Jamii Forums akipokea cheti chake
 Blogger wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurigenzi wa TCRA, Prof, John Nkoma na Mungy
 Mablogger wakiwa katika picha ya pamoja na Prof Nkoma na Mungy mbeye ya jengo la TCRA
Timu ya Mablogger wanawake tu hii hapa

No comments:

Post a Comment