Pages


Photobucket

Friday, September 13, 2013

MSHINDI WA NYUMBA YA PILI AIRTEL YATOSHA ANNE LYMO APOKEA CHETI CHA USHINDI RASMI LEO.

 Meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmmbando (kushoto)  akimkabidhi cheti Mshindi wa Nyumba wa Airtel Yatosha bi. Anna G.Lyimo mkazi (kulia) wa  Dar Es Salaam  akishuhudiwa na Meneja masoko wa Airtel Tanzania Anethy Muga.
Mshindi wa Nyumba wa pili wa Airtel Yatosha  bi. Anna G. Lyimo akionyesha cheti chake alichokabidhiwa na Meneja wa uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando (kulia), wakishuhudiwa na Meneja masoko wa Airtel Anethy Muga (kushoto).
 Wanahabari wakirekodi tukio wakati Anna G. Lyimo anakabidhiwa cheti chake cha nyumba leo jijini Dar es salaam.
****** 
Mshindi wa nyumba ya pili ya Airtel Yatosha yenye thamani ya shilingi milioni 65/- amekabidhiwa cheti cha ushindi leo ikiwa ni uthibitisho maalum mbele ya wanahabari ambapo ni muda mfupi baada ya mshindi huyo kuibuka mshindi kupitia droo kubwa ya mwisho wa mwezi iliyochezeshwa wiki iliyopita Airtel Tanzania kupitia promosheni hiyo imekuwa ikitoa zawadi mbalimbali kwa wateja wake zikiwemo pesa taslim pamoja na nyumba 3 ambapo kila mwezi nyumba moja huenda kwa mshindi mmoja .

Akizungumza kwa furaha Mshindi wa nyumba hiyo ya pili Bi Anna Gustav Lyimo ambae ni mkazi wa Dar es salaam alisema “namshukuru sana Mungu kwa kuniwezesha kuwa mshindi wa nyumba ya Airtel Yatosha, Nilipopigiwa nilijua ni matapeli, mpaka siku ya pili nilipopigiwa kwa mara ya pili na Airtel ndipo nilipojua si utapeli” “Nawashukuru sana Airtel kwa zawadi hii kwani imenirahisishia mipango yangu ya kuanza ujenzi wa Nyumba mwishoni mwa mwaka huu. ,” alisisitiza Bi, Lyimo “Ninawashauri wateja wengine wa airtel kuendela kutumia huduma ya Airtel yatosha ili na wao waibuke washindi kama mimi” alimalizia kusema Bi Anna Lymo .

Kwa upande wake Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw Jackson Mmbando alisema “makabidhiano ya cheti hiki ni taratibu za awali ambapo hivi karibuni mshindi huyu atakabidhiwa rasmi nyumba yake iliyopo maeneo ya Kigamboni jijini Dar es salaam. “Airtel tutaendelea kutoa zawadi bora kwa wateja wetu nchi nzima kupitia promosheni mbalimbali tulizonato” 

“Kama alivyo na furaha mshindi wetu ndivyo na sisi tunavyofurahi na hii sio kikomo bado tunatoa zawadi za pesa taslim kila siku kwa wateja mbalimbali wa Airtel nchi nzima. Njia ni rahisi tu! Jiunge sasa na vifurushi mbalimbali vinavyopatikana kupitia Yatosha na utapata nafasi ya kuingia kwenye droo ya kushinda,” alisema Mmbando.

Kujiunga na vifurushi hivyo mteja anapaswa kupiga *149*99# na kuchagua 1 au 2 kisha aweze kujiunga na kifurushi chochote cha Wiki, Siku au Mwenzi. Airtel kupitia promosheni ya Airtel yatosha imeshatoa zaidi ya shilingi milioni 60 kwa wateja wake kupitia promosheni hii ambapo Promosheni hii inadumu kwa siku 90 toka ianze, hadi sasa bado kuna nyumba moja kati ya tatu zilizopo Kigamboni itashindaniwa kwa mwezi huu.

No comments:

Post a Comment