Pages


Photobucket

Thursday, January 30, 2014

MWILI WA SHEKHE WA MKOA WA MARA WAWASILI UWANJA WA NDEGE MUSOMA.


Mkuu wa mkoa wa Mara, John Tuppa akielekea kwenye ndege kuongoza waombolezaji
  Rubani wa ndege akielekeza namna ya kutoa jeneza lenye mwili wa marehemu


ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI



  Waumuni wa dini ya kiislamu pamoja na wananchi wa mjini Musoma wakiwa uwanja wa ndege
  Afidh Waziri mmoja wa watu waliotoka na mwili wa Shekh Magee Dar akiagana na rubani wa ndege

  Mwili ukiondoka uwanja wa ndege tayari kupelekwa nyumbani

  Msafara wa magari ukisindikiza mwili wa marehemu Shekh Magee nyumbani

  Mkuu wa mkoa wa Mara akiwasili nyumbani kwa shekh
  Mwili ukishushwa kutoka kwene gari baada ya kufika nyumbani kwake
  Waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu


MKUU wa mkoa wa Mara Mh. John Gabriel Tuppa ameongoza maelfu ya Wananchi wa Mji wa Musoma kupokea mwili wa Shekh wa Mkoa wa Mara Athumani Magee aliyefariki dunia usiku wa januari 28 katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

Shekh Athumani Magee alifikwa na mauti baada ya kugua kwa muda na mrefu na kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Bugando kwa muda kabla ya kuhamishiwa Muhimbili kwa uangalizi zaidi na akiwa njiani kupelekwa nchini India kwa matibabu zaidi.

Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislam waliokuwepo kwenye uwanja wa ndege Musoma wakiusubili mwili wa shekh Magee wamesema  wamepata pigo kubwa kutokana na msiba huo kutokana na Shekh kuwa mstari wa mbele katika kuhimiza masuala ya dini.

Shekh wa mkoa wa Mara anatarajiwa kuzikwa kesho kabla ya swala ya adhuhur katika makabari ya Musoma Bus mjini Musoma.

   INNAH LILLAH WAINNAH ILLAH RAJIUUN

HABARI NA PICHA KWA HISANI YA SHOMARI BINDA

No comments:

Post a Comment