Pages


Photobucket

Saturday, January 18, 2014

MADIWANI WOTE KAHAMA WAUNGANA NA NCCR-MAGEUZI

Matembezi ya amani siku ya Pasaka wilayani kahama mwaka jana 2014 yaliyosababisha kushuka kwa gharama za matibabu hospitali ya wilaya kikao cha leo.
Leo tarehe 17/01/2014 Baraza la madiwani wilayani kahama katika kikao chake cha bajeti limeungana na chama cha NCCR-Mageuzi kwa kukubali mapendekezo ya kushusha malipo ya hospitali ya wilaya kutoka Shilingi 3000/= mpaka Shilingi 1000/=. Aidha madiwani hao baada ya kikao waliwaomba viongozi wa NCCR-Mageuzi hasa katibu aliyekuwa kikaoni hapo kuwa wasisite kuibua hoja za msingi. Ikumbukwe kuwa mwezi wa pili mwaka jana 2013 Chama cha NCCR-Mageuzi kilikuwa na ziara ya Opersheni UZALENDO iliyokuwa ikiongozwa na katibu mwenezi wa vijana Taifa ndugu Deogratius Kisandu ajenda kuu ilikuwa ni kupunguza gharama za malipo hospitali.
Pia swala hilo liliendelea kuzungumzwa mwezi  Desemba 2013 katika uzinduzi wa kitabu cha Utani wa Serikali na Wananchi hapa wilayani kahama. Leo madiwani wote wa CCM, CHADEMA, CUF na TLP wameendelea kusema tunakubali changamoto za kila aina na tutaendelea kuungana na chama cha NCCR-Mageuzi katika hoja zake ili kuboresha wilaya yetu. hata hivyo Gharama ya sh.1000/= itaanza rasmi tarehe 1/7/2014.

Mytake; AKSANTENI SANA MADIWANI, MWENYEKITI WA HALMASHAURI, MKURUGENZI NA MKUU WA WILAYA KWA KUONA UMHIMU WA KUFANYA HIVYO NA MUNGU AWABARIKI SANA. PAMOJA TUTASHINDA.

No comments:

Post a Comment