Pages


Photobucket

Sunday, January 26, 2014

HUYU NDO JENNIFER WA KANUMBA ANALIPWA MILLIONI 2 KWA KILA FILAMU ANAYOCHEZA !


Jennifer
Hanifa Daud(Jennifer) ambaye ni mtoto alityetamba katika filamu za Uncle JJ na This Is It akiwa na marehemu Steven Kanumba anadaiwa kulipwa si chini ya sh.million 2 za kitanzania kwa kila filamu anayoigiza. Chanzo kimoja ambacho ni star wa filamu na pia producer maarufu Swahiliwood kilisema kuwa Jenifer anapendwa na ana mashabiki wengi licha ya kuwa mtoto hivyo analipwa kama baadhi ya mastaa wakubwa wanavyolipwa nchini kwa kila filamu.

 " Jenifer ana fans wengi na anapendwa na wengi, dau lake si chini ya milioni 2 za kibongo kwa kila filamu, hachezi filamu nyingi kwa wakati mmoja so filamu anazoigiza hufanya vizuri, watu huwa hawamuoni sana kwenye filamu nyingi ndiyo sababu hupata hamu ya kuona filamu zake mpya" kilisema chanzo hicho kikichonga na Swahiliworldplanet

Kwasasa Jennifer anasoma kidato cha kwanza(form one) na baadhi ya filamu zake mpya zinatarajiwa kuingia sokoni mapema mwaka huu.

                            Jenifer akiwa na marehemu Kanumba

Cred

No comments:

Post a Comment