Pages


Photobucket

Saturday, June 8, 2013

YAKIWA YAMEBAKI MASAA MACHACHE TAIFA STARS KUSHUKA DIMBANI NA MOROCCO,KOCHA POULSEN AWATOA HOFU WATANZANIA

“Wachezaji wako katika hali nzuri kabisa na
 wana ari ya kushinda mechi hii…tuna nguvu na tunajua namna ya kuwapiga Morocco,”Akaongeza kwa kusema,swala si mchezaji
 gani anaanza au washambulizi ni wangapi, bali ni
 kazi itakayofanyika uwanjani na ubora wa
 wachezaji wa Taifa Stars, Alisema Morocco ni timu kubwa
 na ina wachezaji wengi wa kulipwa
 lakini inafungika na Taifa Stars itaweka
 nguvu kuanzia mwanzo wa mechi.
“Unapocheza mechi kama hii inabidi uweke nguvu
 dakika za kwanza za mechi ili umpe mpinzani
 wakati mgumu kwa hivyo dakika za mwanzo zitakuwa
 muhimu sana katika mechi hii,” alisema.
Poulsen alisema baadhi ya watu nchini Morocco bado
 wanaamini kuwa ushindi wa mechi ya awali Jijini
 Dar es Salaam wa 3-1 dhidi ya Morocco ulikuw
a wa kibahati tu. “Tunataka kuwadhihirishia kuwa
 tunaweza na Taifa Stars sio timu ndogo kama wanayodhani.”
Akizungumzia swala la kuwekewa mazingira 
mabaya ya kambi pale wanapocheza mechi za nje,Poulsen
alisema mazingira ya kambi ni mazuri kabisa na
 wachezaji wote wako katika hali nzuri na tayari kwa mchezo huu...
“Katika hali ya kawaida ungetegemea hujuma nyingi
 ikiwemo hoteli mbovu, viwanja vibovu vya mazoezi na
 kadhalika lakini hapa ni tofauti kabisa…kwani 
mazingira ni mazuri,” alisema Poulsen.
Taifa Stars imeweka kambi katika Hoteli ya Pullman
 iliyoko nje kidogo ya Mji wa Marrakech.
Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Taifa stars.

No comments:

Post a Comment