Pages


Photobucket

Saturday, June 15, 2013

NAPE: PUUZENI VITISHO VYA CHADEMA


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Ndg.Nape Nnauye amewataka wananchi kwenye kata zinazofanya uchaguzi mdogo kesho kupuuza alivyoviita vitimbi vya Chadema na wafuasi wao badala yake wajitokeze kwa wingi kushiriki kwenye upigaji wa kura kwa amani na utulivu.
Nape ameyasema hayo jijini Arusha jana wakati alipokuwa anajibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua tathimini ya kampeni na jinsi CCM ilivyojipanga kwenye uchaguzi mdogo katika kata mbalimbali nchini.

Nape alisema kwa ujumla wake kampeni zimekwenda vizuri karibu katika kila kata ukiacha matukio kadhaa machache ya vurugu ambayo alidai yamekuwa yakiratibiwa na Chadema na wafuasi wao baada ya kuvuta bangi na kunywesha vijana wao viroba.

"nimekuwa Arusha kwa siku mbili tatu, hakuna mashaka kuwa Arusha wamechoshwa na vurugu za Chadema , baada ya kuhangaishwa kwa miaka mitatu na vurugu za Chadema wameamua sasa kurudisha utulivu na heshima ya jiji la Arusha, hivyo nawapongeza sana" alisema Nape.

" ni kweli hata mie nimesikia wenzetu baada ya kuona maji ya shingo wameamua kutumia vitisho kujaribu kutisha watu hasa kina mama na wazee wasiende kupiga kura, lakini nawahakikishia CCM tumejipanga kuwalinda waende kupiga kura kwa amani na utulivu. Isitoshe taarifa tulizoziapata zinaonyesha serikali imejipanga vizuri sana kulinda amani na utulivu, hivyo tunawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kupiga kura bila hofu" alisisitiza Nape.

Aidha Nape alidai kwa taarifa walizonazo wanamatumaini kuwa kata zote 25 zinazofanya uchaguzi mdogo CCM itashinda kwani wanaamini kuwa wananchi wana imani kubwa na CCM na kuwa vitimbi vinavyofanywa na wapinzani nchini vimewachefua sana wananchi.

Itakumbukwa kuwa chaguzi ndogo nchini zinafanyika kwenye kata 25 kufuatia kata hizo kuwa wazi kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo vifo na baadhi kuhama au kufukuzwa vyama vyao vya siasa.

Ushindani mkubwa ulitegemewa sana jijini Arusha ambapo kuna kata nne zinafanya ucahguzi mdogo kufuatia Chadema kuwafukuza madiwani wake. Hata hivyo hali jijini Arusha inaonyesha Chadema kulemewa sana kiasi cha kuwa na uwezekano wa kupoteza kata zote ambazo walikuwa wakizimiliki mwanzoni.

Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary

No comments:

Post a Comment