Pages


Photobucket

Thursday, June 20, 2013

TAZAMA WADADA WATATU WA FAMILIA MOJA WENYE UGONJWA WA KUOTA NYWELE MWILI MZIMA:


 

Ndugu hawa wote wanatokea nchini india wa kwanza anaitwa Savita (23),Monisha (18)na Savitri (18)ambao wote hawa katika maisha yao wamelazimika kutumia dawa ambazo huweza kuwasaidia kupunguza uwezo wa nywele kuota kwa kasi. Ndugu hawa watatu kati ya sita waliozaliwa katika familia moja wameathirika na ugonjwa huu uitwao kitaalamu werewolf syndrom.Ugonjwa huu unaweza kumfanya mgonjwa kuweza kuota nywele karibu kila sehemu ya mwili wake hasa sehemu za usoni.Ni mara chache sana kumpata mgonjwa anayeumwa ugonjwa huu.Kwani wataalamu wanasema kuwa hutokea kwa mtu mmoja kati ya watu billioni moja. Chanzo cha ugonjwa mama wa watoto hawa amesema kwamba ni kutoka kwa baba yao ambaye alikua na ugonjwa huu.Na yeye alilazimishwa kuolewa naye bila kujua kama anaugonjwa huu.Kutokana na umasiki walionao wameshindwa kulipia gharama za upasuaji kwa mgonjwa mmoja ni zaidi ya dola za kimarekani 7,000.Mama huyu anaomba msaada wa kumsaidia watoto wake hawa kuweza kufanyiwa upasuaji ili siku moja waweze pona na kuolewa.

No comments:

Post a Comment