Pages


Photobucket

Monday, June 24, 2013

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA (TCRA) KANDA YA MASHARIKI WATOA SEMINA YA MAWASILIANO KWA WADAU WAO KATIKA WILAYA YA BAGAMOYO

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Ahamed Kibozi akihutubia wakati wa uzinduzi rasmi wa semina ya wadau wa huduma za Mawasiliano iliyowalenga wawakilishi wa jumuiya mbalimbali za vijiji na vitongoji vya Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.aliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzanizi(TCRA ) Kanda ya Mashariki hivi karibuni.Katikati ni Mkurugenzi wa Huduma za Mawasiliano wa TCRA, Dk.Raynold Mfungahema na Kushoto ni Meneja wa Kanda ya Mashariki Mhandisi Oscar Mwanjesa.
Mkurugenzi wa Huduma za Mawasiliano Dk.Raynold Mfungahema akitoa mada ya Haki na wajibu wa watumiaji wa huduma za mawasiliano wakati wa semina ya watumiaji wa huduma za mawasiliano iliyofanyika katika chuo cha sanaa cha Bagamoyo kwa kuwashilikisha wawakilishi wa jumuiya mbalimbali za vijiji na vitongoji vya Wilaya ya hiyo.
Afisa wa Idara ya Posta wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA,Bi,Ccilia Sylvester,akitoa mada juu ya mfumo mpya wa anuani za posta semina ya wadau wa huduma za Mawasiliano iliyowalenga wawakilishi wa jumuiya mbalimbali za vijiji na vitongoji vya Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.aliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzanizi(TCRA ) Kanda ya Mashariki wakiwakatika foleni ya kujiandikisha wakati wakuingia katika semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha sanaa Bagamoyo.
Mkurugenzi wa Huduma za Mawasiliano wa TCRA, Dk.Raynold Mfungahema,akionyeshwa na Rajabu Husein ujumbe kwenye simu yake wakati alipokuwa akitoa mada ya haki na wajibu wa watumiaji wa huduma za mawasiliano katika semina ya watumiaji wa huduma za Mawasiliano (wadau) iliyowashirikisha wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.Semina hiyo iliandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Kanda ya Mashariki.
Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Mashariki Mhandisi Oscar Mwanjesa akimkabidhi zawadi ya simu Mwanahamisi Muhamed baada ya kujishindia wakati wa semina ya watumiaji wa Mawasiliano (wadau) iliyowashirikisha wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.Semina hiyo iliandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Kanda ya Mashariki.

Mhasibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)Patrice Lumumba akitao zawadi ya simu kwa mmoja wa wasshiriki wa semina ya wadau wa huduma za Mawasiliano iliyowalenga wawakilishi wa jumuiya mbalimbali za vijiji na vitongoji vya Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.aliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzanizi(TCRA ) Kanda ya Mashariki hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment