Pages


Photobucket

Thursday, August 8, 2013

MAAJABU YA CHADEMA: DR. SLAA AWAUNGA MKONO WAASI WA KONGO NA KUMKINGIA KIFUA KAGAME


Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kauli yake ya kumshauri Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kuzungumza na waasi wa serikali yake ...


Dk. Slaa amesema haoni busara kwa Rais Kikwete kuwaambia viongozi wa Rwanda, akiwamo Rais Kagame, kuzungumza na wafuasi wa chama cha FDRL walioko Congo.

Slaa aliyasema hayo wakati akizungumza katika kongamano la vijana wa Chadema (BAVICHA) la uchumi na ajira lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

“Rais Kikwete hapa nyumbani hawezi kuzungumza na wapinzani na hajachukua hatua dhidi ya wauaji wa mwandishi Daudi Mwangosi...

"Alishauriwa amuwajibishe Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda na badala yake amempandisha cheo,” alisema Slaa.


Kauli Dk Slaa imekuja siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kueleza kuwa Tanzania haina mgogoro na nchi ya Rwanda, kutokana na kauli za kejeli na matusi zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa nchi hiyo dhidi yake na Tanzania.


Kumezuka sitofahamu ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Rwanda, baada ya Rais Kikwete kuitaka Rwanza imalize ugomvi na waasi kwa njia ya mazungumzo ya amani...

Rais Kikwete aliutoa ushauri huo wakati wa mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia hivi karibuni.

Ushauri huo ulionekana kumchukiza Rais Kagame, anayedaiwa kuhutubia mikutano kadhaa nchini kwake na kutumia lugha ya matusi, kejeli na dhihaka dhidi ya Rais Kikwete na Tanzania.

Kitendo cha Dr Slaa kumkingia kifua Kagame kinatia shaka uzalendo wake na chama chake kwa taifa hili ...

Sote tumekuwa tukishuhudia matusi ya Kagame dhidi ya Tanzania.Iwaje Rais Kikwete aonekane mbaya kwa kumjibu Kagame, tena kwa lugha ya kizalendo??


Kagame amekuwa akituhumiwa na jumuiya mbalimbali za kimataifa kwa kutoa misaada ya kivita kwa waasi wa M23 ambao wamekuwa wakiua raia na kuwabaka wanawake....

Kauli ya Dr Slaa ina mambo mengi yaliyojificha na huenda yeye na chama chake ni wafuasi wa karibu wa M23 kama ilivyo kwa Kagame.

Kuwa mpinzani, haimaanishi ukosoe kila kitu

No comments:

Post a Comment