Pages


Photobucket

Thursday, August 8, 2013

Breaking News!!!! Manchester United inatarajia hii habari njema ndani ya saa 48.

Katika hali ya kawaida Fabregas amekuwa na nafasi kwenye kikosi cha Barcerlona japo si nafasi ya kiungo ambayo anapenda kucheza ambapo kusajiliwa kwa mchezaji wa kimataifa toka Brazil Neymar, kunaweza kupunguza nafasi ya Cesc kwenye kikosi cha kwanza hasa katika kipindi hiki ambapo michuano ya kombe la dunia inakaribia.
United wanaweza kupata upinzani kwenye harakati za kumsajili Fabregas toka Arsenal ambayo ina makubaliano na Barca ya kuwa timu ya kwanza kupewa fursa ya kumsajili kiungo huyo ambae alikuwa nahodha wao wa zamani.
Mashabiki wa United bado wanaugulia machungu ya kumkosa kiungo mwingine wa Hispania Thiago Alcantarra ambaye alichagua kusajiliwa Bayern japo alidhaniwa kuwa yuko karibu kujiunga na Man United.
Story za Michezo hapa millardayo.com ni kwa nguvu ya NMB, chukua pesa yako popote kwenye ATM zaidi ya 500 Tanzania, kwa siku unaweza kuchukua mpaka shilingi milioni moja.

No comments:

Post a Comment