
 Afisa Mkuu Mtendaji wa Helvetic  
Solar Contractors Patrick Ngowi akisikiliza mawazo ya mmoja wa vijana 
wajasiriamali mwenye nia ya kukataka kukuza biashara yake na kuifanya 
kuwa endelevu wakati  wa uzinduzi wa Mara Foundation ambao uliotoa fursa
 ya washiriki kuzungumza na wafanyabiashara waliopiga hatua na wenye 
uzoefu katika kuendesha biashara zao.
 Afisa Mtendaji Mkuu  wa Relim 
Limited Emelda Mwamanga akimsikiliza mmoja wa washiriki ambaye ni 
mjasiriamali anayechipukia aliyetaka kupata uzoefu na mawazo zaidi jinsi
 ya kuendesha biashara yake.
Mkurugenzi Mkuu wa 361 Degrees 
ambaye ni Mbunifu Mkongwe wa Mavazi nchini Tanzania Mustafa Hassanali 
akimsikiliza mjasiriamali mdogo mwenye ndoto za kuwa mbunifu wa 
kimataifa.
Ma-Mentors waliokuja kuzungumza na
 wafanyabiashara wadogo kwa ajili ya kuwapa mbinu mbalimbali za 
kibiashara na kuwaongoza kufikia malengo yao.
Taasisi ya Mara Foundation  
ilianzishwa na Ashish Thakkar ambaye ndie mwanzilishi na Mkurugenzi Mkuu
 wa Mara Group. Ashish alitumia muda wake mwingi katika kutimiza malengo
 ya Taasisi hiyo kwa kuwa alikuwa na imani na wajasiriamali na 
kuendeleza biashara ndogo.
Tangu mwaka 2009 Taasisi hiyo 
ililenga mtazamo wake na imefanya vizuri sana nchini Uganda, Tanzania, 
Kenya na Nigeria katika muelekeo huo. Kuanzia mwaka 2013 mikakati ya 
taasisi ya Mara Foundation inaendelea kukua katika nchi za Kusini mwa 
Jangwa la sahara  huku ikiendelea kuongeza wigo wake katika nchi 
nyingine duniani. Mara Foundation inafanya kazi ya kubuni na kukuza 
uchumi endelevu na kufungua fursa endelevu kwa vijana wamiliki wa 
biashara za kati kwa kupitia vituo vya uwezeshaji vya Mara Launchpad na 
Mara Launch Fund.
Pichani juu na chini ni Washiriki 
na wageni waalikwa wakibadilishana mawazo kabla ya mgeni rasmi Dkt. Mary
 Nagu kuzindua Taasisi hiyo.
Mkurugenzi Mkazi wa Mara 
Foundation Tanzania Nina Werner (kulia) akizungumza machache kuhusiana 
na malengo ya Taasisi yake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mh. Dkt. 
Mary Nagu kuizindua rasmi.
 Mgeni rasmi katika ufunguzi wa 
taasisi ya kibiashara ya Mara Foundation Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri 
Mkuu Uwezeshaji na Uwekezaji Mh. Dkt. Mary Nagu akizungumza wakati 
kuzindua taasisi ya Mara Foundation ambapo amewataka vijana 
wajasiriamali kutumia fursa ya taasisi hiyo kujijenga kibiashara Taasisi
 ya Mara Foundation yenye makao yake makuu jijini Dubai sasa imejikita 
katika nchi za Afrika ambazo ni Uganda, Tanzania, Kenya na Nigenia kwa 
lengo kuwasaidia wajasiriamali wadogo kuwezeshwa kimuongozo na kuwa 
wafanyabiashara wakubwa ambao wataweza kutoa ajira kwa watu wengine.
Washiriki na wageni waalikwa 
wakifurahi jambo wakati mgeni rasmi Dkt. Mary Nagu akitoa risala kwenye 
uzinduzi wa Taasisi ya Mara uliofanyika hivi karibuni kwenye jengo la 
Mayfair Plaza.
 Mgeni rasmi katika ufunguzi wa 
taasisi ya kibiashara ya Mara Foundation Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri 
Mkuu Uwezeshaji na Uwekezaji Mh. Dkt. Mary Nagu akikata utepe kuzindua 
rasmi taasisi hiyo yenye matawi 28 barani Afrika. Kushoto ni Mkurugenzi 
Mkazi wa Mara Foundation Nina Werner.
Sasa imezinduliwa rasmi.
 Wageni waalikwa wakishangilia kwa makofi.
MC wa uzinduzi huo ambaye pia ni 
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Problem Solved Eric Mutta akimkabidhisha 
Mjasiriamali mdogo Peter Christopher kwa Afisa Mkuu Mtendaji wa Helvetic
  Solar Contractors Patrick Ngowi  (katikati) atakayekuwa mshauri wake 
wa kibiashara kwa muda wa miezi sita ijayo.
Mkurugenzi Mkuu wa 361 Degrees 
ambaye ni Mbunifu Mkongwe wa Mavazi nchini Tanzania Mustafa Hassanali 
(katikati) akimpokea mmoja wa wajasiriamali waliohudhuria uzinduzi wa 
Mara Foundation kwa lengo la kuhakikisha anatimiza malengo yake.
  Afisa Mtendaji Mkuu  wa Relim 
Limited Emelda Mwamanga (kushoto) akipata picha ya ukumbusho na kijana 
aliyemchagua kumsaidia kimawazo na kumwongoza kwa muda wa miezi sita 
ijayo mpaka kufikia lengo lake.
 Baadhi ya wageni waliohudhuria uzinduzi wa Mara Foundation uliofanyika hivi karibuni Mayfair Plaza.
 Afisa Mkuu Mtendaji wa Helvetic  
Solar Contractors Patrick Ngowi (kushoto) na Mkurugenzi Mshirika wa 
IMMMA Advocates Lawrence Masha wakibadilishana mawazo wakati wa hafla ya
 uzinduzi wa Mara Foundation.
  Afisa Mkuu Mtendaji wa Helvetic 
 Solar Contractors Patrick Ngowi (kushoto) Mkurugenzi Mshirika wa IMMMA 
Advocates Lawrence Masha (kulia) na Mkurugenzi wa man Magazine Dismas 
Massawe (katikati) katika picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa Mara 
Foundation.