Pages


Photobucket

Sunday, February 15, 2015

Balozi wa promosheni ya JayMillions awalipia nauli abiria wote

Balozi wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hilary Daud "Zembwela"(kushoto)akimkabidhi fedha mmoja wa abiria wa basi linalofanya safari zake kutoka kituo cha mabasi cha mawasiliano cha ubungo kwenda Mwananyamala jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuwalipia abiria wenzake nauli ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha wateja wa kampuni hiyo kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama wameshinda.

  • Awataka watanzania kuchangamkia fursa
  • Ahimiza wateja kuangalia kama namba zao zimeshinda kila siku
  • Atembelea stendi ya mabasi Ubungo na kumwaga ofa kwa wasafiri

Balozi wa promosheni ya Jaymilioni inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hillary Daud‘Jaymillions’ mwishoni mwa wiki alikuwa kivutio kwa wananchi wengi alipotembelea eneo kituo cha mabasi cha Ubungo Mawasiliano na kuwahimiza wananchi kuchangamkia fursa zinazojitokeza katika maisha yao ambapo pia alitoa ofa ya kuwalipia nauli wasafiri waliokuwa wamepanda mabasi kuelekea sehemu mbalimbali za jiji waliokuwa kituono hapo.

Ziara hiyo ilileta msisimko mkubwa wa wananchi waliokuwa eneo hilo ambapo baadhi yao walilazimika kuacha shughuli zao kumwangalia balozi huyo na wengine kuomba kupiga naye picha ikiwemo waliompiga picha kwa kutumia simu zao zao mkononi.

Balozi huyo alitumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi kuwa wanaotumia mtandao wa Vodacom wahakikishe kila siku wameangalia kama namba zao zimeshinda mamilioni ya fedha kwa kutuma neno JAY kwenda namba 15544 na aliwataka wale ambao hawako kwenye mtandao wa Vodacom wajiunge nao ili washiriki kwenye promosheni hii kubwa iliyolenga kubadilisha maisha ya watanzania wengi kuwa mamilionea.

“Leo nimewafuata huku kuwapatia ofa na kuwafikishia ujumbe kwa maana naona wengi wenu bado hamjachangamkia fursa hii kwa kuangalia iwapo namba zenu zimeshinda kila siku,bado tunayo mabilioni ya fedha kwa ajili yenu hivyo changamkia fursa hii muweze kujishindia mamilioni ya fedha katika kipindi hiki cha promosheni.Kila siku kuna mshindi 1 wa shilingi milioni 100,000,washindi 10 wa milioni 10 na washindi 100 wa shilingi milioni 1 hivyo kazi kwenu na Vodacom”.Alisema

Naye Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, aliwahimiza wateja wote kuchangamkia promosheni hii kwa kuhakikisha wametuma neno JAY kwenda namba 15544 ili kutopoteza nafasi zao za kushinda pia alisema kuwa njia nyingine ya kushinda ni kutuma neno AUTO kwenda namba 15544 iwapo simu haina fedha ambapo mteja akiweka fedha anakatwa shilingi 300/-

Alisema kuwa tangu promosheni hii ianze mapema mwezi uliopita mteja mmoja ameishajishindia milioni 100, wateja 2 wamekwishajishindia milioni 10 na wateja kumi na moja wameisha jishindia shilingi milioni moja kila mmoja na maelfu ya wateja wengine tayari wamejishindia muda wa maongezi.

Wateja wa Vodacom ambao tayari wamejipatia mamilioni ya fedha kupitia promosheni hii ni Uwezo Magedenge mfanyakazi nyumba ya wageni wilayani Kilolo mkoani Iringa ambaye amejishindia milioni 100. Waliojishindia milioni kumi kila mmoja wao Hynes Petro Kanumba mkulima kutoka Inyonga mkoani Rukwa na James Mangu mfanyabiashara kutoka wilayani Magu

Washindi wa milioni moja ni Chiphold Wanjara mjasiriamali wa Kutoka Mwanza ,Janeth Nganyange wa Njombe,Evarista Minja mwanafunzi kutoka Mwanza,Stanley Bagashe Mwalimu wa Shinyanga,Ramadhani Maulid Mkulima kutoka Dodoma, ,Lucas Masegese wa Shinyanga,Ayub Makonde mfanyabiashara wa Mbeya,Hyasinti Mlowe Fundi gereji kutoka Njombe,Florian Gwayu mchapishaji kutoka Arusha,Modesta Millanzi mjasiriamali kutoka Peramiho mkoani Ruvuma na Nobert Minungu mwanafunzi kutoka Mbwanga mkoani Dodoma.

“Promosheni hii itadumu kwa muda wa siku mia moja hivyo juma hili inaingia katika wiki ya nne na bado kuna mabilioni ya fedha yamewasubiri watanzania,wanachopaswa kufanya ni kuhakikisha kila siku wameangalia kama namba zao zimeibuka na ushindi kwenye droo ya siku kwa kutuma neno Jay kwenda namba 15544.”Alisisitiza.
Mkazi wa jijini Dar es Salaam Mudy Seleman(kushoto)akikabidhiwa fedha kwa ajili ya nauli na Balozi wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hilary Daud”Zembwela” wakati wa kuhamasisha wateja wa kampuni hiyo kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama wameshinda iliyofanyika katika kituo cha mabasi cha Mawasiliano ubungo jijini Dar es Salaam. 

Baadhi ya wanafunzi waliokuwa wakisubiria usafiri katika kituo cha mabasi cha mawasiliano ubungo jijini Dar es Salaam wakipiga picha ya pamoja na Balozi wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hilary Daud”Zembwela”(kushoto)baada ya kuwalipia nauli wakati wa kuhamasisha wateja wa kampuni hiyo kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama wameshinda iliyofanyika katika kituo hicho.

Meneja uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kushoto)akitoa elimu kwa mmoja wa abiria wa basi liendalo Gongolamboto kutoka kituo cha mabasi cha mawasiliano ubungo jijini Dar es Salaam juu ya Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na kampuni hiyo ambapo wateja wanatakiwa kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama wameshinda. 005.Baadhi ya abiria wakiwa na watoto wao katika kituo cha mabasi cha Mawasiliano ubungo jijini Dar es Salaam, wakifafanuliwa jambo na mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Joyce Mhina kuhusiana na Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na kampuni hiyo wakati Balozi wa promosheni hiyo alipoenda kituoni hapo kutoa elimu kuhusiana na promosheni hiyo na kuwalipia wasafiri wote bure wa daladala nauli kulingana na sehemu wanayo kwenda ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha wananchi kushirikia katika promosheni hiyo.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay kwenda 15544.


Balozi wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hilary Daud”Zembwela”(aliyesimama)akitoa elimu juu ya promosheni hiyo kwa abiria waliopanda daladala zinazofanya safari za mlandizi kutoka kituo cha mabasi cha mawasiliano ubungo jijini Dar es Salaam na aliwalipia nauli abiria wote bure ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha wananchi kushirikia katika promosheni hiyo.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay kwenda 15544.

Kondakta wa basi linalofanya safari zake kutoka kituo cha mabasi cha Mawasiliano ubungo kwenda Kawe jijini Dar es Salaam, Hamis Omari (kushoto)akikabidhiwa nauli ya abiria wote waliopanda gari lake na Balozi wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hilary Daud”Zembwela”(kulia) wakati alipokuwa akihamasisha wateja wa kampuni hiyo kituoni hapo kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama wameshinda. Ambapo abiria wote waliokuwepo kituoni hapo walilipiwa nauli kulingana na safari zao.

No comments:

Post a Comment