Pages


Photobucket

Sunday, October 20, 2013

MKUU WA WILAYA YA CHAWINO AIPONGENZA AIRTEL

                Mh. Mkuu wa Wilaya  ya Chamwino Bi.Fatma  S. Ally


Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Bi. Fatma S. Ally  Ameipongeza kampuni ya simu ya  Airtel  kwa  kutoa msaada wa vitabu  katika shule ya sekondari ITISO. Mkuu huyo amesema hayo wakati akitoa hotuba yake  katika Mahafali ya  Kidato cha nne  iliyofanyika   Shule ya Sekondari ITISO  Tarehe 18/10/2013 " Nimefurahi kusikia  juhudi zilizo onyeshwa na  Kampuni, ya simu ya  Airtel kwa  kutoa vitabu vya sayansi katika shule hii,hivyo nichukue  fursa hii kwa upekee kuipongeza kampuni hii  ya simu" Alisema Bi. Fatma.

Katika hatua nyingine aliwataka wanafunzi wa  kidato cha nne kujikita zaidi katika maadalizi ya mitihani iliyoko mbele yao na kuongeza kuwa bado wanayo nafasi ya kupitia vyema kile walicho kisoma  ili waweze kuwa katika hali nzuri ya kujibu mitihani yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi CCM  Wilaya ya  Chamwino  Mh. Joel Mwaka  alisema  wazazi bado wanayo nafasi kubwa kuhakikisha watoto wao  wanafanya vema katika masomo yao kwa maana ya kufatilia kwa ukaribu maendeleo yao  kitaaluma.Jukumu la  ufaulu kwa mwanafunzi  linahusisha Mwanafunzi mwenyewe,Mwalimu pamoja na Mzazi,Alisema Bw. Joel


      Mkuu wa Shule ya Sekondari  Itiso  Bw. Andrea  A. Mauki  Akisoma Risala mbele ya Mgeni Rasmi
     Baadhi  ya wahitimu wa Kidato cha Nne  wakisikiliza kwa umakini hotuba ya Mgeni Rasmi.




         Mkuu wa Shule ya ITISO Akikabidhi Risala kwa Mgeni Rasmi
                       Mwenyekiti wa Kijiji cha ITISO akizungumza  wakati wa mahafali hiyo.


                         Afisa Elimu (Sekondari) wa  Halmashauri ya Chamwino  Bi.Nyemo  Masimba
        Mkuu wa  Shule  ya  Sekondari ya ITISO Bw. Andrea  A. Maukia  kifuatilia kwa umakini Matukio mbalimbali katika Mahafali hayo 
           Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi  CCM (Wilaya ya Chamwino) Mh. Joel Mwaka
 
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule Ndugu Raymond  Mwakifamba akizungumza katika mahafali  hayo


   Chereko na shangwe kwa Wahitimu...!!!!!

No comments:

Post a Comment