Pages


Photobucket

Saturday, November 2, 2013

PINDA, MAWAZIRI HATARINI KUNG'OLEWA

Waziri Mkuu Mizengo Pinda pamoja na mawaziri wake wawili; Khamisi Kagasheki (Maliasili na Utalii) na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, Dk Mathayo David wameingia matatani kutokana na shinikizo linalowataka wang’oke katika nafasi zao.

Pinda pamoja na mawaziri hao wanatakiwa kuachia ngazi kama hatua ya kuwajibika kutokana na matukio ya vifo na baadhi ya watu kujeruhiwa, katika matukio ya migogoro ya wakulima na wafugaji kwa upande mmoja na utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Majangili kwa upande mwingine.

Jana wabunge walicharuka na kuwataka mawaziri waliohusika katika Operesheni Tokomeza Ujangili wawajibishwe wakieleza kutoridhishwa na maelezo waliyoyatoa mapema jana, baada ya kipindi cha maswali na majibu.

Kelele za wabunge zilizuka baada ya wabunge kuanza kuchangia maelezo ya Serikali kuhusu migogoro ya wafugaji na wakulima, hifadhi za wawekezaji na maelezo ya Serikali kuhusu Operesheni Tokomeza Ujangili.

Aliyekuwa wa kwanza kuchangia mjadala huo ni Mbunge wa Kilolo, Profesa Peter Msola (CCM) ambaye katika hitimisho lake alitoa hoja ya kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza kile ambacho alikiita kuwa ni unyanyasaji wa wafugaji na uporaji wa mifugo yao.

Profesa Msola alielekeza shutuma zake kwa Serikali kuwa ilifanya operesheni zake kwa pupa bila kufanya maandalizi hivyo kuwaathiri wananchi wasiokuwa na hatia.

Spika wa Bunge, Anne Makinda kabla ya kuahirisha kikao cha Bunge jana mchana aliridhia kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kwa ajili ya kuchunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji, wakati ‘madudu’ ya Operesheni Tokomeza Majangili yatachunguzwa kupitia Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira.

Chimbuko la hoja

Jana asubuhi kabla ya Bunge kuanza kikao chake, Spika Makinda alitoa taarifa kwamba Kikao cha Kamati ya Uongozi kingekutana wakati kipindi cha maswali na majibu kikiendelea, kwa lengo la kutoa mwelekeo wa mjadala wa hoja za dharura.

Hoja hizo ni zile zilizotolewa na wabunge wawili kwa nyakati tofauti; Alphaxard Kangi Lugora wa Mwibara (CCM) kuhusu Operesheni Tokomeza Majangili na Saidi Nkumba wa Sikonge (CCM), kuhusu vita baina ya wakulima na wafugaji.

Kamati hiyo ilikutana baada ya kipindi cha maswali na majibu na Spika Makinda alitoa taarifa za kusitisha shughuli nyingine, ili wabunge waweze kujadili masuala hayo ambako kabla ya kuanza mjadala aliwaita mawaziri kutoa taarifa zao.

Alianza Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Kagasheki ambaye katika maelezo yake alihitimisha kwa kutangaza kusitisha Operesheni Tokomeza ili kupitia mpango huo na kufanya maboresho ili kuondoa upungufu uliopo.


Licha ya kueleza sababu nyingi zilizofanya Serikali kuendesha operesheni hiyo, alisema ina manufaa makubwa katika kuokoa wanyama aina ya tembo, lakini waziri alihitimisha kwa kusema itakuwa ni busara kuifanyia tathmini wakati ikiendelea, hivyo kutangaza kuisitisha mara moja.

Kwa upande wake Dk Mathayo alitoa maneno ya kuomba radhi na kuwapa pole watu waliopatwa na usumbufu ikiwa ni pamoja na kupoteza mali zao na mifugo.

Mathayo aliwaeleza wabunge kuwa Serikali imepanga kujenga malambo katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia wafugaji kupata maji ili kupunguza safari za kuhamahama kutoka eneo moja kwenda jingine.

Shinikizo kwa Pinda

Baada ya kumaliza hotuba zao, wabunge kadhaa walipata nafasi ya kuchangia maelezo hayo huku wengi wakielekeza shutuma zao kwa mawaziri hao na wenzao wa Mambo ya Ndani ya Nchi na yule wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Wabunge wawili wa Chadema, Paulina Gekul (Viti Maalumu) na John Shibuda (Maswa Mashariki) walitaka Waziri Mkuu Pinda ajiuzulu kutokana kushindwa kwake kudhibiti mauaji na mateso kwa wananchi.

Gekul alisema kinachotokea sasa ni utekelezaji wa kauli ya Pinda aliyoitoa bungeni akisema wahalifu wapigwe tu pamoja na ile ya Kagasheki aliyoitoa mjini Arusha akisema majangili watakaokamatwa wamalizwe hukohuko kwenye hifadhi.

Mbunge huyo alieleza operesheni hiyo kwamba imesababisha mauaji ya watu wasio na hatia ikiwemo mama Emiliana ambaye alifuatwa akiuza nyanya, lakini akateswa hadi kufa na hadi sasa mwili wake bado uko katika Hospitali ya Babati baada ya wananchi kugoma kuuzika.

Shibuda kwa upande wake alisema Pinda anapaswa kufungua milango kwa mawaziri wanaotakiwa kujiuzulu haraka, kutokana na kulea uzembe ambao umesababisha madhara makubwa kwa wafugaji.

Shibuda alisema kuwa Wizara ya Mifugo imekuwa na mtazamo hasi lakini akasisitiza kuwa uzembe wa viongozi wa ngazi za mikoa, wilaya hadi vijiji unatokana na ukimya wa Pinda ambaye anashindwa kuchukua hatua yoyote dhidi yao.

Wabunge wengine

Kwa upande wake Nkumba aliunga mkono kuundwa kwa kamati teule, lakini akasisitiza kuwa mawaziri hao wanne wana hoja za kujibu ndani ya chama tawala CCM na kwa Rais, vinginevyo Serikali haipaswi kuendeshwa na viongozi wazembe

BAADA YA NICK WA PILI KUMALIZA MASTER DEGREE MLIMANI HUU NDIO USHAURI ALIO TOKA KWA WANAMUZI

 
Rapper wa kampuni ya Weusi, Nick wa Pili amefanikiwa kuhitimu shahada yake ya pili kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam, UDSM.

Nick aliitoa taarifa hiyo kwenye kipindi cha Club 10 cha Clouds FM na kutoa ushauri kwa wanafunzi wanaofanya muziki.

“Mimi ni mwanafunzi, jana nimemaliza degree ya pili mlimani. Nimefurahi kuna wanafunzi wanataka kuwa kama mimi,kuna vitu vichache vya msingi vya kuzingatia kwa upande wa sanaa. Inabidi waache mambo mengi ya sanaa wachague kitu kimoja, atake kuwa msanii bora. Ukitaka kuwa msanii bora usihangaikie mambo ya kwenda studio, sijui kumtafuta nani ,sijui kutafuta interview, atake kuwa msanii bora hayo mambo mengine yatakufuata,” alisema Nick.

“Ukitaka kufanikiwa kitaaluma, njia moja ni kusoma lakini kusoma vipi,sio kusoma unasubiri kufika form 4 ndio unaanza kusoma au umefika form 6 ndio unaanza kusoma. Mwanafunzi bora ni yule anayesoma kila siku na unatakiwa kusoma kila siku. Soma kidogo, elimu sio ngumu, tatizo wanafunzi wanafeli katika mipango. Soma kidogo tambua masomo yako, tambua topic zako.Kila somo tambua topic ngapi, angalia muda wangu mwaka huu ilitakiwa nisome moja mbili tatu,nne ,tano jee nimefika? au unajipima. Pili ni kusoma kidogo hata ikawa ni kwa masaa mawili kila siku yanatosha kabisa.”

Hivi karibuni Nick wa Pili alipata shavu la kuwa miongoni mwa wazungumzaji wakuu kwenye semina za fursa kwenye mikoa zaidi ya 13

BAADA YA NICK WA PILI KUMALIZA MASTER DEGREE MLIMANI HUU NDIO USHAURI ALIO TOKA KWA WANAMUZI

 
Rapper wa kampuni ya Weusi, Nick wa Pili amefanikiwa kuhitimu shahada yake ya pili kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam, UDSM.

Nick aliitoa taarifa hiyo kwenye kipindi cha Club 10 cha Clouds FM na kutoa ushauri kwa wanafunzi wanaofanya muziki.

“Mimi ni mwanafunzi, jana nimemaliza degree ya pili mlimani. Nimefurahi kuna wanafunzi wanataka kuwa kama mimi,kuna vitu vichache vya msingi vya kuzingatia kwa upande wa sanaa. Inabidi waache mambo mengi ya sanaa wachague kitu kimoja, atake kuwa msanii bora. Ukitaka kuwa msanii bora usihangaikie mambo ya kwenda studio, sijui kumtafuta nani ,sijui kutafuta interview, atake kuwa msanii bora hayo mambo mengine yatakufuata,” alisema Nick.

“Ukitaka kufanikiwa kitaaluma, njia moja ni kusoma lakini kusoma vipi,sio kusoma unasubiri kufika form 4 ndio unaanza kusoma au umefika form 6 ndio unaanza kusoma. Mwanafunzi bora ni yule anayesoma kila siku na unatakiwa kusoma kila siku. Soma kidogo, elimu sio ngumu, tatizo wanafunzi wanafeli katika mipango. Soma kidogo tambua masomo yako, tambua topic zako.Kila somo tambua topic ngapi, angalia muda wangu mwaka huu ilitakiwa nisome moja mbili tatu,nne ,tano jee nimefika? au unajipima. Pili ni kusoma kidogo hata ikawa ni kwa masaa mawili kila siku yanatosha kabisa.”

Hivi karibuni Nick wa Pili alipata shavu la kuwa miongoni mwa wazungumzaji wakuu kwenye semina za fursa kwenye mikoa zaidi ya 13

BAADA YA NICK WA PILI KUMALIZA MASTER DEGREE MLIMANI HUU NDIO USHAURI ALIO TOKA KWA WANAMUZI

 
Rapper wa kampuni ya Weusi, Nick wa Pili amefanikiwa kuhitimu shahada yake ya pili kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam, UDSM.

Nick aliitoa taarifa hiyo kwenye kipindi cha Club 10 cha Clouds FM na kutoa ushauri kwa wanafunzi wanaofanya muziki.

“Mimi ni mwanafunzi, jana nimemaliza degree ya pili mlimani. Nimefurahi kuna wanafunzi wanataka kuwa kama mimi,kuna vitu vichache vya msingi vya kuzingatia kwa upande wa sanaa. Inabidi waache mambo mengi ya sanaa wachague kitu kimoja, atake kuwa msanii bora. Ukitaka kuwa msanii bora usihangaikie mambo ya kwenda studio, sijui kumtafuta nani ,sijui kutafuta interview, atake kuwa msanii bora hayo mambo mengine yatakufuata,” alisema Nick.

“Ukitaka kufanikiwa kitaaluma, njia moja ni kusoma lakini kusoma vipi,sio kusoma unasubiri kufika form 4 ndio unaanza kusoma au umefika form 6 ndio unaanza kusoma. Mwanafunzi bora ni yule anayesoma kila siku na unatakiwa kusoma kila siku. Soma kidogo, elimu sio ngumu, tatizo wanafunzi wanafeli katika mipango. Soma kidogo tambua masomo yako, tambua topic zako.Kila somo tambua topic ngapi, angalia muda wangu mwaka huu ilitakiwa nisome moja mbili tatu,nne ,tano jee nimefika? au unajipima. Pili ni kusoma kidogo hata ikawa ni kwa masaa mawili kila siku yanatosha kabisa.”

Hivi karibuni Nick wa Pili alipata shavu la kuwa miongoni mwa wazungumzaji wakuu kwenye semina za fursa kwenye mikoa zaidi ya 13

DIAMOND NUSURA AKAMATWE NA MAOFISA WA USALAMA WA TAIFA BAADA YA KUUTIBUA MSAFARA WA RAIS...

STAA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond.

STAA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Alhamisi iliyopita alijikuta akiutibua msafara wa Rais wa Zanzibar, Dk. Mohamed Shein kufuatia kuondoka kwenye msiba wakati ilitangazwa kiongozi huyo ndiye aliyetakiwa kuanza kuondoka.
Ishu hiyo iliyotafsiriwa kama jeuri ya staa huyo ilitokea Mbuzini Mjini Magharibi, Zanzibar baada ya kumalizika kwa mazishi ya baba wa Wema Sepetu, aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania Urusi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na Waziri wa Elimu wa zamani katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, marehemu Isaac Abraham Sepetu.
 
DIAMOND AINGIA
Awali, wakati waombolezaji wamekaa wakiusubiri mwili wa marehemu ufike, ghafla Diamond aliibuka akisindikizwa na kundi la wapambe mpaka alipokaa.
                                                     AWEKWA MSTARI WA MBELE
Diamond alipofika aliwekwa mstari wa mbele ambako walikaa ndugu wa karibu na watoto wote wa marehemu.
 
MC ATANGAZA ITIFAKI YA SERIKALI
Mwili ulipowasili, ratiba ya mazishi ikatangazwa na MC ambapo alitaja utaratibu wa mazishi mpaka watu watakaotakiwa kuweka mashada ya maua kaburini, akiwemo Rais Shein.
Baada ya mazishi, Mwongoza Shughuli ambaye jina halikujulikana aliwaomba watu wote wazingatie itifaki ya usalama wa taifa kwamba ni lazima viongozi wote wa serikali waondoke ndipo waombolezaji wengine watawanyike.
“Jamani naomba sana itifaki izingatiwe, asiondoke mtu yeyote kabla ya viongozi wetu wa serikali, akiwemo Rais Shein hawajaondoka,” alisema MC huyo.
 
DIAMOND APUUZA, ANYANYUKA
Baada ya MC huyo kutoa mwongozo, watu wote walitulia wakisubiri kiongozi wa kwanza kuondoka ambaye alikuwa ni Rais Shein kama itifaki ilivyotaka.
Lakini kabla Rais Shein hajaanza kusimama, Diamond alinyanyuka na kuzua kasheshe kwa sababu baadhi ya watu, hasa wa umri wake walianza kumkimbilia huku wakikanyagana na kusababisha hali ya taharuki.
 
MC AWATULIZA WATU
Baada ya watu kuanza kukimbizana hovyo muongozaji wa msiba huo aliwaomba watulie na kusema kuwa wasiogope ila kuna staa ambaye anapita ndiyo maana watu wamemkimbilia.
“Naomba utulivu huyo ni staa f’lani kapita huko ndiyo maana watu wanamkimbilia hivyo tulieni kwanza viongozi wetu waondoke,” alisema.

USALAMA WA TAIFA NUSURA WAMKAMATE
Baada ya kuona watu wakikimbia hovyo baadhi ya maofisa wa usalama wa taifa walitaka kumkamata msanii huyo wakisema alisimama kwa makusudi licha ya kusikia tangazo la kiitifaki.
 
WATU WAMSHANGAA DIAMOMD
Baadhi ya watu waliohudhuria msiba huo walionekana kushangazwa na kitendo cha Diamond na kusema kuwa ni vyema angesubiri viongozi wote waondoke ndipo na yeye atimke lakini kufanya vile si sahihi.
“Huyu Diamond kwani ana nini? Nakumbuka kwenye msiba wa Kanumba kule Dar pia aliingia kipindi ambacho ilitangazwa kuna kiongozi anakwenda, utaratibu ukatibuka, watu wakawa wanamshangilia yeye,” alisema mtu mmoja aliyetoka Dar kwenda

ALAMA MPYA ZA UFAULU MASHULENI ZAPINGWA

 
SIKU moja baada ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kufanya marekebisho katika upangaji wa viwango vya alama za matokeo ya wanafunzi wa kidato cha nne na sita kwa kufutwa daraja sifuri na kuwekwa daraja la tano, wadau na wasomi wameponda mfumo huo.

Wakizungumza na gazeti hili, wadau hao walisema kuwa tatizo si kushuka kwa kiwango cha ufaulu, bali uwepo wa elimu bora nchini.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally, alisema kuna mifumo miwili ya elimu nchini inayotumika, ambayo ni ule wa watu masikini na wenye nafuu ya maisha.

Alisema hali hiyo inaanzia chekechea hadi vyuo vikuu, huku akihoji wizara husika mfumo wa aina hiyo unamlenga nani, kwamba tatizo lililopo ni ubora wa elimu hasa katika shule za umma.

Bashiru alisema kwenye mifumo hiyo inayotumika, ule wa masikini upo kwenye shule nyingi za umma ambako ndiko kwenye watoto wengi wanaofeli kutokana na kukosa vifaa vya kufundishia, maabara na walimu.

“Katika shule za umma watoto wengi hawasomi, hawana maabara, sasa wizara inawatahini nini? Mageuzi yoyote ambayo yatashindwa kuondoa matabaka hayawezi kuleta elimu tunayoitaka,” alisema.

Alisema ubora wa elimu utawahusu wanafunzi hao wanaosoma shule za michepuo ya Kiingereza, kwani ndio watakaokuwa wanafaulu kwa kuwa shule zao zina mfumo mzuri unaoeleweka na viwango walivyojiwekea kama mwanafunzi hatafikia atarudia darasa ama kuachishwa shule.

Naye mhadhiri mwingine wa chuo hicho, Prof. Herme Mosha, alisema kama wizara inataka kuongeza idadi ya watu katika ufaulu waliofanya mtihani, inapaswa kuboresha elimu.

“Sio mara ya kwanza tumechezea vigezo, 2007 tulibadilisha viwango tulivyokuwa navyo tukaweka alama za chini, wanafunzi wengi wakachaguliwa, matokeo yake mtihani wa mwisho wa kidato cha nne kukawa na matokeo mabaya,” alisema.

Alisema lililofanyika sio utatuzi wa tatizo, bali wizara iangalie nini kinasababisha ubora wa elimu kushuka.

Kwa mujibu wa Prof. Mosha, wizara husika iangalie ni nini kinachowafanya wanafunzi wasisome badala ya kupandisha viwango kwa aina hiyo waliyoitumia.

Dk. Kitila Mkumbo wa Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema tatizo lililopo ni mfumo mbaya wa ufundishaji, kwani kupanga madaraja kwa aina hiyo si suluhu ya kutatua changamoto iliyopo.

Alisisitiza kuwa kwa staili hiyo, serikali haitoi tatizo bali inajaribu kuficha tatizo, hivyo hakuna cha kushangilia kwa mfumo huo walioutangaza.

Mwalimu wa sekondari, Josephat Ammy, alieleza kuwa mfumo huo utamfanya mwanafunzi kubweteka na kutochukulia umuhimu suala la elimu kwa kudhani kuwa uwezo wa kufaulu anao.

“Wao walitakiwa waje na suluhisho la elimu na kujua kwanini wanafunzi wanafeli, sasa wanachofanya nini? Wanaondoa daraja ziro halafu hao wa daraja la tano wanakwenda wapi?” alihoji.

Naye mmiliki wa shule za Green Acres, Julian Bujugo, alisema kuwa mfumo huo sio mbaya kwani wanafunzi watafanya mtihani kwa kutumia mitaala.

“Mfumo huu ulikuwepo hapo awali kabla ya kutolewa, sioni kama una ubaya. Ni mzuri, utasaidia kwa wanafunzi tofauti na mwaka jana walitunga mitihani ambayo haikuwa kwenye mitaala,” alisema.

Naye Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gracian Mukoba, alisema kuwa kubadilisha alama itakayowasaidia watoto wengi kuonekana wamefaulu haisaidii kwani ndiyo kwanza kunaongeza zao la ujinga.

Alisema kama walikuwa wanatafuta kufurahiwa na wazazi na wanafunzi, basi wangeweka alama A, B, C plus bila kuwa na alama hizo za daraja hadi la tano.

Kwa mujibu wa Mkoba, kilichofanyika ni siasa tu na kucheza na saikolojia za wazazi, ambazo tayari zimeathiriwa na mfumo mbaya wa elimu ambapo idadi kubwa ya watoto wanaofeli inaongezeka kila kukicha.

“Yaani hapa ni kama bomba, unakuta linatoa maji machafu ya tope. Baada ya kuangalia nini chanzo chake wewe unaamua kubadilisha koki na kuweka nyingine wakati si suluhisho,” alisema.

Mukoba alisema njia sahihi za kuboresha elimu serikali inazijua kwa kuwa tayari walishatumia fedha nyingi kwa ajili ya kuunda tume, kufanya utafiti, hivyo majibu tayari wanayo.

Naye mwalimu wa vituo vya elimu ya Taasisi ya Watu Wazima, Stanslaus Sekuru, alisema kuwa mfumo huo utaboresha elimu kwa sababu hapo awali wanafunzi walikuwa wakiumia sana.

Alitolea mfano daraja la nne akisema mwanafunzi anakuwa na alama 26, lakini akiwa na alama C tatu anashindwa kuendelea na kidato cha tano na mwenye daraja la tatu mwenye alama 25 na C tatu yeye anapewa nafasi ya kuendelea.

Mwalimu Charles Mkwidu ambaye ni mratibu wa Kituo cha Elimu ya Watu Wazima, alisema mpango huo ni mzuri ila uwekewe mkakati wa kuwasaidia wanafunzi kupenda kusoma, hasa masomo ya sayansi kwani wengi husoma wakati wa mitihani tu.

Naye mwanafunzi anayerudia mitihani, aliyeathiriwa na matokeo ya mwaka jana, Jesca Charles, alisema huenda ikawasaidia au la kwa kuwa mitaala ya elimu ndiyo iliyowaponza hadi wakafeli.

Upatikanaji Huduma za Maji Rombo Tatizo

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, Judathadei Mboya

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, Judathadei Mboya
Na Yohane Gervas, Rombo
IMEELEZWA kuwa hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Wilaya ya Rombo imekua mbaya hasa katika tarafa za Mengwe na Tarakea. Hayo yamebainishwa jana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya
ya Rombo, Anthoni Tesha katika kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Rombo.
Tesha alisema kuwa maeneo mengi ya Tarafa za Mengwe na Tarakea yanakabiliwa na uhaba mkubwa wa huduma ya maji, hali inayowafanya baadhi ya waalimu kuvunja vipindi vya mchana na kuwarudisha wanafunzi kwenda kutafuta maji.
Aidha Tesha alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, Judathadei Mboya, kuhakikisha wanakutana na Meneja wa Kampuni ya Maji ya Kiliwater ili kuzungumzia suala hilo mapema.
Uhaba wa maji katika vijiji mbalimbali katika wilaya ya Rombo imeonekana kuwa changamoto kubwa hasa katika maeneo ya ukanda wa chini wa wilaya hiyo ambapo baadhi ya maeneo hupata huduma ya maji kwa mgao na maeneo mengine kukosa kabisa huduma hiyo.