Sunday, February 9, 2014
HII NDIO HISTORIA YA MASANJA MKANDAMIZAJI................SOMA HAPA KUJUA ZAIDI

Kwa wapenzi wa sanaa ya vichekesho, jina la Masanja Mkandamizaji si geni masikioni mwao kutokana na uwezo wake wa kuwavunja mbavu watazamaji pale anapoonekana katika runinga na Kundi la Original Comedy.
Licha ya kufika hapo alipo sasa, msanii huyu anakiri wazi kuwa amepitia katika ugumu hususani wakati alipoamua kuanza maisha binafsi ya kujitegemea baada ya kutoka nyumbani kwa dada yake alipokuwa akiishi
Anasema kabla ya kuondoka kwa dada yake alimuomba amtafutie chumba ili ajitegemea na kuanza maisha binafsi kama kijana .
Nilimwambia dada anitafutie chumba na alifanya hivyo ingawa alikuwa anahofia kama nitaweza ,basi nikapata 'geto' langu maeneo ya Tabata Aroma na nilitakiwa kulipa kodi ya Sh5000 kwa mwezi, anasema Masanja.
Anakiri wazi kuwa changamoto katika maisha ndizo zilizochangia kumfikisha mahali alipo sasa kwani licha ya kuwa katika hali ngumu hakukata tama bali alizidi kujituma kwa nguvu zake zote.
Anasema kuna wakati ilikuwa vigumu kuipata hata hiyo hela ya kodi kwahiyo ilikuwa inamlazimu kurudi kwa dada yake kwa muda unapofikia wakati kulipa kodi.
Yaani hiyo Sh5000 kuipata ilikuwa shughuli maana ilikuwa ikifika karibu na mwisho wa mwezi narudi kwa dada kuzuga kidogo ili mama mwenye nyumba ajue nimesafiri,anasema.
Anasema alianza kwa kulala chini mpaka siku alipofanikiwa kupata fedha kidogo iliyomuwezesha kununua godoro la sufi jambo ambalo anajivunia nalo kwani aliweza kununua kwa jasho lake.
Anaongeza kuwa kamwe hawezi kumsahau marehemu Steven Kanumba pamoja na mtu mwingine aliyemtaja aitwaye Mtitu kutokana na mchango wao uliosaidizi kumfikisha hapo alipo sasa .
Namshukuru sana marehemu Kanumba alikuwa anakuja kunichukua kule Tabata tunaenda kupiga 'inshu' ambazo zilikuwa zikiniingizia pesa kidogo iliyoniwezesha kuishi hata hivyo maisha yalikuwa magumu.
Wakati naanza maisha sikuwahi kutoa hela hata ya kununua chipsi kavu lakini siku moja nilifanya kazi na Mtitu ambayo alinilipa laki moja sikuamini macho yangu, kwa mara ya kwanza kununua chipsi kuku kwani nilikuwa nikitamani mlo huo nililazimika kusaidia kumenya viazi kwa washikaji,
Sambamba na uchekeshaji Masanja pia amejiingiza katika shughuli za kumtukuza Mungu baaada ya kuokoa na sasa anafanya vizuri pia katika uimbaji wa nyimbo za injili na kesho Jumapili atazindua albamu yake ya pili ya muziki wa Injili inayoitwa Hakuna jipya chini ya jua.
Saturday, February 1, 2014
CCM YAZIDI KUJIIMARISHA MBEYA MJINI
Katibu wa NEC
Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akigawa kadi kwa wanachma wapya
waliojiunga na CCM baada ya kuzindua shina la Wakereketwa la Madereva wa
Bodaboda Inyara,Iyunga mkoani Mbeya.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Inyara, Iyunga mjini mkoani Mbeya baada ya kuzindua shina la wakereketwa ambapo aliwaambia CCM imejiandaa vya kutosha kwa ushindi wa 2015..
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Inyara ,Iyunga baada ya kuzindua shina la wakereketwa la madereva wa Boda Boda.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wafanyabiashara ndogo ndogo wa Inyara ,Iyunga mkoani Mbeya.
Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Iyunga mara baada ya kufungua shina la wakereketwa ambapo alisisitiza kwa madereva wa boda boda kuwa Umoja ni Ushindi hivyo kukiwa na umoja dhabiti kati yao basi watafanikiwa sana na aliwasihi vijana waepuke dhambi ya kubaguana.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa na dereva wa BodaBoda wa Iyunga Itika Mwangosi ambaye amejiunga na chama cha mainduzi na kukabidhiwa kadi yake na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na baadhi ya viongozi wa CCM Iyunga mara baada ya kufungua shina no.3 la Bodaboda .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na mmoja wa wapenzi wa CCM aliyekuwa akisafiri kwa Bajaj ,Soweto mjini Mbeya.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitembea mitaa ya Soweto kwenda kufungua shina la wakereketwa wauza chakula na wauza matairi kata ya Ruanda,Jumla ya mashina manne yalizinduliwa leo mjini Mbeya.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Inyara, Iyunga mjini mkoani Mbeya baada ya kuzindua shina la wakereketwa ambapo aliwaambia CCM imejiandaa vya kutosha kwa ushindi wa 2015..
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Inyara ,Iyunga baada ya kuzindua shina la wakereketwa la madereva wa Boda Boda.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wafanyabiashara ndogo ndogo wa Inyara ,Iyunga mkoani Mbeya.
Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Iyunga mara baada ya kufungua shina la wakereketwa ambapo alisisitiza kwa madereva wa boda boda kuwa Umoja ni Ushindi hivyo kukiwa na umoja dhabiti kati yao basi watafanikiwa sana na aliwasihi vijana waepuke dhambi ya kubaguana.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa na dereva wa BodaBoda wa Iyunga Itika Mwangosi ambaye amejiunga na chama cha mainduzi na kukabidhiwa kadi yake na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na baadhi ya viongozi wa CCM Iyunga mara baada ya kufungua shina no.3 la Bodaboda .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na mmoja wa wapenzi wa CCM aliyekuwa akisafiri kwa Bajaj ,Soweto mjini Mbeya.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitembea mitaa ya Soweto kwenda kufungua shina la wakereketwa wauza chakula na wauza matairi kata ya Ruanda,Jumla ya mashina manne yalizinduliwa leo mjini Mbeya.
Friday, January 31, 2014
Chadema kususia Bunge la Katiba
Wakati
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akisema wabunge wa chama chake
watasusia vikao vya Bunge Maalumu la Katiba ikiwa hoja ya kuundwa kwa
Serikali tatu itapingwa na wabunge wa CCM, Mwakilishi wa Mji Mkongwe
(CUF), Ismail Jussa Ladhu ametaka kuvunjwa kwa Muungano.
Akihutubia
kwenye Uwanja wa Tubuyu nje kidogo ya Mji wa Morogoro juzi, Mbowe
alisema wabunge wa chama chake wataandamana nchi nzima kufikisha ujumbe
kwa wananchi kwamba maoni yao yamepingwa na wabunge wa CCM walio wengi.
“Tutawaeleza
wananchi kwamba maoni ya CCM ndiyo yameonekana ya maana kuliko ya
wananchi ambao ni wengi zaidi,” alisema Mbowe kwenye mkutano huo ambao
ni sehemu ya Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko - M4C Pamoja Daima.
Alisema Tume
ya Mabadiliko ya Katiba ilikusanya maoni na kubaini kuwa asilimia 62 ya
Watanzania wanataka Serikali tatu za Tanganyika, Zanzibar na ya
Muungano.
“Serikali ya
CCM haitaki kusikia maneno Serikali tatu wanasema sera yao ni ya
Serikali mbili, wanafanya kila hila ili kuikataa hoja hiyo. Natangaza
kwamba wakifanya hivyo tutasusia na kwenda kuwashtaki kwa wananchi,”
alisema Mbowe.
Aliongeza kwamba wataandamana kuanzia Kagera hadi Mtwara kuwaeleza wananchi kwamba hoja yao imepingwa na CCM.
Mbowe
alisema baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa wakitoa kashfa dhidi ya
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kwamba
amechukua maoni ya Chadema.
“Wanakosea hayo si maoni ya Chadema, bali ni maoni ya wananchi, Warioba amezingatia maoni ya wananchi,” alisema.
Mwenyekiti
huyo alisema Katiba inayotafutwa si ya chama, bali ni ya Watanzania na
kwamba inashangaza CCM kuipinga hoja Serikali tatu.
“Tunafahamu
wanaogopa kuikubali hoja ya Serikali tatu kwa sababu wanafahamu huo
ndiyo utakuwa mwisho wao wa kuwa madarakani,” alisema Mbowe huku
akishangiliwa na wafuasi wa chama hicho.
Alisema CCM
wanaelewa kwamba kukiwa na Serikali tatu, Chadema kitashinda Tanganyika
na CUF Zanzibar katika uchaguzi wowote utakaoitishwa.
“Kwa hiyo
hivi sasa wana wasiwasi kweli, wanatafuta kila njia ya kuichakachua hoja
ya Serikali tatu lakini wafahamu kuwa Chadema wanaifuatilia hoja hiyo
kwa ukaribu,” alisema.
Aliwataka
wananchi kufuatilia Bunge Maalumu la Katiba litakapoanza mwezi ujao ili
kuangalia wabunge wao wanavyowawalisha katika suala hilo muhimu.
Hata hivyo,
Mbowe alisema chama hicho kikishinda katika uchaguzi wa mwaka 2015
hakitahangaika kulipa kisasi kwa kuwachukulia hatua za kisheria
viongozi, bali kitajikita kutafuta maendeleo.
“Wasituogope
tutasamehe kama alivyosamehe aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson
Mandela. Hatutalipa kisasi tukiingia Ikulu, kwa sababu hakuna binadamu
asiye na makosa. Tutaelekeza nguvu zetu kuwaletea maendeleo Watanzania,”
alisema Mbowe.
Jussa na Muungano
Akihutubia
mkutano wa kampeni katika Jimbo la Kiembesamaki jana, Jussa alisema
hakutakuwa na maendeleo yatakayofikiwa Zanzibar ikiwa Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar hautang’oka.
Jussa ambaye
pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa la CUF, alisema Zanzibar yenye
watu milioni 1.5 haiwezi kuwa na tatizo la watu kukosa ajira lakini sera
na mipango ya kiuchumi imekuwa ikikwama katika utekelezaji wake
kutokana na kukosa mamlaka kamili.
Alisema
Zanzibar haiwezi kukopa katika taasisi za kimataifa bila ya kuwekewa
dhamana na Waziri wa Fedha wa Muungano wakati Zanzibar ni nchi na
kuwataka wananchi kutumia kura zao katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 kuleta
mabadiliko ya kiutawala.
“Hakuna
sababu ya vijana Zanzibar kukosa ajira, kuna watu wasiozidi milioni 1.5,
Muungano umefika wakati ung’oke, ndiyo kikwazo cha maendeleo ya
Zanzibar na watu wake kiuchumi na kisiasa,” alisema Jussa.
Alisema
mradi wowote unaobuniwa Zanzibar hauwezi kupata mfadhili bila kuwekewa
dhamana na Serikali ya Muungano na kukwama kwa juhudi zote za kujiunga
na jumuiya za kimataifa akitolea mfano Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu
(OIC).
Alisema Rais
wa Zanzibar amepoteza mambo muhimu chini ya mfumo wa Muungano ikiwa ni
pamoja na kutopigiwa mizinga 21 akiwa nje ya nchi, kupeperusha bendera
ya Zanzibar, kutokagua gwaride na kupigiwa wimbo wa Taifa la Zanzibar.
“Haya ya
sasa si mamlaka kamili, wapi Dk Shein alikokwenda akapigiwa mizinga 21
au alipeperushwa wapi bendera ya Zanzibar wakati wa safari zake za nje?”
alihoji Jussa.
FIRST MEETING OF THE AFRICAN AMBASSADORS IN THE AFRICA HOUSE
Balozi
wa African Union nchini Marekani Mhe. Amina Salum Ali (kulia) akiongoza
mkutano wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini
Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya African Union lililopo
Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano January 29, 2014
Waheshimiwa
Mabalozi waliohudhuria mkutano huo wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika
wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya
African Union lililopo Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano
January 29, 2014.
Waheshimiwa
mabalozi wakifuatilia mkutano wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika
wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya
African Union lililopo Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano
January 29, 2014
D’BANJ NA YAYA TOURE WAUNGA MKONO KAMPENI YA KILIMO YA RAIS KIKWETE
D’Banj alishirikiana na washirika wa Kilimo wa Afrika katika uzinduzi wa
kampeni ya ‘Shiriki Kilimo’ (Do Agric) kwenye kongamano la Umoja wa
Afrika. Kampeni hiyo inalenga kuwasaidia watu zaidi ya milioni 85 barani
Afrika kutoka katika lindi la umasikini kupitia uwekezaji maalumu
katika kilimo na sera za kilimo za Maputo zilizoboreshwa.
D’Banj alikuwa mmoja wa waliozungumza Addis Ababa jana wakati wa
uzinduzi wa kampeni hiyo yenye lengo la kuwahamasisha viongozi wa
kisiasa kutumia sera nzuri zitakazonyanyua uzalishaji, kuongeza kipato
na kuondoa mamilioni ya Waafrika kutoka katika umasikini.
“Nataka Waafrika kufahamu kilimo ni msingi mzuri wa uchumi ambacho
kinatakiwa kutiliwa mkazo na kuleta mabadiliko katika uchumi wa wananchi
na nchi na pia tukitilia mkazo tunaweza kuilisha dunia nzima kwa ujumla
sisi kama Waafrika,” alisema D’Banj.
Kwa upande wake mchezaji wa timu ya Manchester City, Toure alisema
wakati viongozi wengine wa Kiafrika wakitoa kauli zenye nia njema, kwa
sasa ni nchi 8 tu zililizotimiza ahadi zake za kuwekeza 10% ya bajeti za
nchi katika kilimo.
“Kwahiyo ni muhimu kufanya zaidi na kwenda mbele zaidi. Kilimo sio muhimu pekee, pia ni lazima. Kilimo kinalipa,” alisemaToure.
Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na asasi mbalimbali za kiraia zikiwemo Pan
African Farmers Association (PAFO), Action Aid International , Acord
International, Oxfam na Alliance for Green Revolution In Africa (AGRA)
mbali na asasi hizo mwanasoka wa kimataifa wa Ivory Coast Yaya Toure pia
ametia saini kuunga mkono uhamasishaji huo.
Source:Habari leo
JUSTIN BIEBER AJISALIMISHA POLISI NCHINI CANADA KWA KOSA LA KUMSHAMBULIA DEREVA WA LIMO
Polisi jijini Toronto wanasema Justin Bieber alikuwa miongoni mwa watu sita waliochukuliwa na limousine nje ya klabu ya usiku December 30. “Wakati kundi hilo linapelekwa hotelini, ugomvi ulitokea kati ya abiria mmoja na dereva wa limousine hiyo,” maelezo ya polisi yalisema.
Maelezo hayo yamedai wakati wa vurugu huyo, mmoja wao alimpiga dereva nyuma ya kichwa chake mara kadhaa na hivyo limousine kusimama na dereva akaita polisi lakini mtu aliyemshambulia dereva huyo alikimbia.
Kutokana na kosa hilo, Bieber atapanda kizimbani kwenye mahakama ya Toronto, March 10.
Mapema Jumatano hii, jumla ya sahihi 100,000 zilikusanywa kupitia website ya ikulu ya Marekani zinazodai Bieber afukuzwe nchini Marekani. Rais wa Marekani hana mamlaka ya kuagiza kufukuzwa kwa mtu na haijulikani kama White House itajibu malalamiko hayo.
Subscribe to:
Comments (Atom)













