Pages


Photobucket

Wednesday, December 25, 2013

RAIS WA CBE AONGOZA WANAFUNZI WA CBE KATIKA KUTOA MKONO WA KHERI YA X MASS KATIKA KITUO CHA WATOTO YATIMA- MIYUJI


 Mhe, Remidius M. Emmanuel (Rais wa Serikali ya wanafunzi CBE ya Dodoma) akiwa na baadhi ya viongozi katika kituo cha Watoto Yatimu cha Miyuji leo tarehe 24/12/2013 mnamo saa tano asubuhi (JANA), akitoa pongezi kwa Mlezi wa kituo hicho Sister Glory Shayo kwa kulea watoto hawa. Rais aliwasilisha baadhi ya vitu kwaajili ya watoto hao
 "Napenda tuwe mfano mzuri ndani na nje ya chuo, hata Mkoa kuwatembele watoto hawa kujiona nao ni sehemu ya jamii kiujumla" Maneno ya Rais.
VILIVYOTOLEWA NI;
Mchele kilo 50
Ngano kilo 50
Mafuta kula lita 20
Mafuta ya kujipata  dazan 1
Maji carton 2
Mhe, Yohana akimsikiliza Mhe, Remidius M. Emanuel anavyo toa zawadi hizo
 Watoto hawa wakiongea na ndugu Dominicky Stephano na nyuso zao zikionekana ni za furaha 

 Waziri wa Fulsa na Mipango Mhe, Riziki Shaweji akiwa na Naibu Waziri wa Fedha Mhe, Simba

 Zawadi zilizo tolewa


 Mhe, Rais akikabidhi zawadi hizi kwa mlezi wa kituo hiki



 Rais akiwa na watoto hawa akionyesha upendo kwa watoto Yatima

 Hii ni nembo ya kituo hiki iyonacho sadifu mazingira harisi ya watoto wanolelewa mahari hapa.
 Mhe Ignas alipata bahati ya kutembelea shamba la mboga mboga hili ni shamba ambalo kituo kimeweza kuliwekeza kwa ajili ya kilimo hiki cha mboga mboga:

 Hakuna mahari popote duniani panapoweza kuondokana na janga la njaa pasipo kuwekeza katika kilimo vivyo hivyo hivyo katika kituo hiki wameamua kupigana na adui njaa kwa kujiandalia mazao yao: Tazama mashamba haya:

Saturday, December 14, 2013

HUYU NDIYE MWENYEKITI MPYA WA TAHLISO 2013/2014


   Bw, Musa  Mdede -Rais waChuo kikuu cha Bugando   (Katikati) Akizungumza Mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti  wa TAHLISO 2013/2014

Bw.Musa Mdede ameibuka Kidedea katika hatua ya pili baada ya kupata kura 18, akifuatiwa  na Rais wa  St. John  Dodoma Bw, Katumbi Edmund  kupata kura 7 akifuatiwa  na Bw.Hemed Ally Rais wa IFM aliyepata kura 6.
Ingwa katika hatua ya kwanza wagombea wa nafasi hiyo walikuwa  ni Watano,Ambapo matokeo yao ya awali   Musa Mdede  (Kura 16),Hemed Ally (kura 7) ,Katumbi Edmund (Kura  5) ,Bi. Tusubilege  Benjamin (Makamu wa Rais wa UDSM -Kura 3) na paschal  Mlela(  kutoka chuo cha Theophilo Kisanje  Mbeya -  kura  3) .Hali hiyo ilifanya  jumla ya kura kuwa 34   na kati ya wagombea wote katika hatua ya kwanza hakuna aliyefikisha  zaidi ya asilimi Hamsini (50%)  hivyo kuufanya uchaguzi kurudiwa katika nafasi hiyo kwa washindi watatu wakwanza katika hatua ya pili.

 Muonekano wa Viongozi wapya wa TAHLISO 2013/2014,kutoka kulia ni Mhazini  Bw.Mollel Hilary (Kutoka Chuo cha Kodi Dae es salaam),Bi.Halima Bakari -Katibu Mkuu(Kutoka chuo cha AMUCTA-Tabora),Makamu Mwenyekiti  Bw.Abdul Mohamed (Rais wa Chuo cha kikuu Zanzibar),Mwenyekiti  Bw.Musa  Mdede (Rais Chuo kikuu Bugando) na Naibu Mhazini  Bw.Khamis  Hamza (kutoka Chuo kikuu cha Zanzibar)


 
 Mwenyekiti  Anayemaliza Muda wake Bw. Amon  Chakushemeire   akizungumza  maneno machache baada ya  Mwenyekiti mpya kutangazwa.