Pages


Photobucket

Thursday, November 7, 2013

JACK WOLPER FAKE ANASWA AKIOMBA HELA MTANDAONI..JACK ORIGINAL ASIKITIKA KUCHAFULIWA

Akionyesha kusikitishwa na kile kinachoendelea facebook, leo hii muigizaji bongo movie,Jackline Walper ameanika maongezi yaliyokuwa yakiendelea katika akaunti ya Walper fake kupitia facebook ikionyesha chati iliyoonekana Walper akiomba sh 20,000 kwa ajili ya kununua umeme mara baada ya kutaikiwa na umeme huku akifanya kazi zake kwenye computer.

Walper aliweka maongezi hayo yakiambatana na manenoo haya kwa chini

Wolpergambe "mashabiki zangu haya ndo mambo ya fc bk dah hvii kweli ndo wanavyonidhalilisha plz nisaidien ata kuamdika huko kwa fc bk zenu situmii jina lolote zaidi ta wolper gambe real .siyoo vzuri jamani muwe na roho ya huruma kdogo dah"
----

BOB JUNIOR AKANA KATU KATU KUTOKA NA MKENYA ANAE ITWA ASHLEY TOTO

Ashley Toto na Bob Junior
Na Waandishi Wetu
MIEZI michache baada ya kufunga ndoa na kupata mtoto, Prodyuza na Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Raheem Rummy Nanji ‘Bob Junior’ na mkewe Halima Ally wameachana, Amani linakuhabarisha.
Habari kutoka katika chanzo chetu makini ambacho ni rafiki wa karibu na Bob Junior zinasema kwamba, ndoa hiyo ilivunjika muda mrefu lakini wahusika walikuwa wakifanya siri lakini Amani limeinasa


BOB JUNIOR TATIZO
Kwa mujibu wa jamaa huyo ambaye hakutaka kuandikwa gazetini, alisema chanzo cha kuparaganyika kwa ndoa hiyo ni Bob Junior mwenyewe kutokana na kutuhumiwa na mkewe kumsaliti.
“Mke wake alikuwa anamtuhumu Bob kutoka kimapenzi na mwanamke mmoja wa Kikenya na pia inasemekana anatembea na Vanessa Mdee (mwanamuziki). Maneno yalivyokuwa mengi, mkewe akaamua kuondoka, hivi ninavyoongea na wewe, yupo kwao,” alisema.

BOB JUNIOR AKIRI
Mashitaka yote yalifikishwa kwa Bob Junior kama yalivyo ambapo bila kumung’unya maneno, msanii huyo mwenye mauno sana awapo jukwaani alikubali kutengana na mkewe lakini akachomoa suala la Mkenya na 
Vanessa.
“Ni kweli nimeachana na mke wangu kama mwezi mmoja uliopita na ameondoka na mtoto, hayo maneno kwamba nina mwanamke wa Kikenya siyo ya kweli. Vanessa ni msanii mwenzangu, nafanya naye kazi tu, hakuna cha zaidi,” alisema.

YUKO NA NANI SASA?
Alipoulizwa kama ameshafungua ukurasa mwingine wa kimapenzi alisema: “Nimeshasema nimeachana na mke wangu, kwa sasa niko singo, sina mpenzi wala mchumba, niko singo tu.”
Bob Junior alipoulizwa kama atarudiana na mkewe alisema hana uhakika ila kama Mungu ndiye aliyepanga watarudiana lakini kama siyo hawatarudiana.

VANESSA NAYE
Vanessa alipopatikana kwa njia simu na kuelezwa kila kitu, alisema: “Siwezi kuzungumzia suala hilo maana kila jambo huwa lina mipaka yake.”

Chanzo :GPL

WEMA SEPETU AIPASUA BONGO MUVI PAAA.............BAADA YA KUSUSIWA MSIBA WA BABA YAKE.

KLABU ya mastaa wa filamu jijini Dar es Salaam, Bongo Movie ‘Bongo Muvi’ imepasuka katikati kisa kikidaiwa kuwa ni lile tamko linalodaiwa kutolewa na mwenyekiti wa klabu hiyo, Vincent Honorati Lasasi Kigosi ‘Ray’ kuwa mwanachama yeyote wa kundi hilio asitie miguu kwenye msiba wa baba mzazi wa mwenzao, Wema Sepetu, marehemu Balozi Isaac Sepetu.
Tukio hilo la katazo lilitokea wakati wa maombolezo ya kifo cha mzee Sepetu kilichotokea Oktoba 27, mwaka huu katika Hospitali ya TMJ kwa ugonjwa wa kisukari ambapo msiba ulikuwa nyumbani kwake, Sinza Mori jijini Dar es Salaam.
LAWAMA ZOTE KWA RAY
Kufuatia madai hayo, baadhi ya wasanii wa Bongo Muvi (majina tunayo) wamekuwa wakitoa lawama zao kwa Ray huku wengine wakidai wamejitoa kwenye kundi hilo kwa sababu halina umoja na limejaa unafiki.
Maneno hayo yalianza kusambaa baada ya Wema kumaliza kumzika baba yake Oktoba 31, mwaka huu mjini Zanzibar.

  
RAY AAGIZWA AITISHE KIKAO CHA DHARURA KUMJADILI
Habari za uhakika zinasema kwamba, wasanii waliotangaza kujiengua klabuni humo wameshamuomba Ray aitishe kikao cha dharura kwa ajili ya kuzungumzia hatua yake ya kuwapiga marufuku wasanii hao kutoshiriki msiba wa mzee Sepetu huku akijua wema wa binadamu unapatikana kwenye kushiriki mazishi ya wenzake.
“Kikubwa zaidi ni kwamba, Ray wakati akisambaza zile meseji alisahau kuwa kuna siku Wema aliwahi kuwaalika wasanii wa Bongo Muvi nyumbani kwake Makumbusho (Dar) wakala na kunywa, mbona hawakugoma kwenda?” alihoji staa mmoja aliyepinga katazo la Ray.

NJAMA ZA KUINGAMIZA KABISA BONGO MUVI ZAUNDWA CHINI KWA CHINI
Habari zaidi kutoka kwenye kundi linalodaiwa kujimega kwenye mpasuko huo zinasema kuwa kuna njama za makusudi za kuiangamiza klabu hiyo kwa kuwa mbali na mwenyekiti huyo kuwazuia wajumbe wasiende msibani kwa mzee Sepetu lakini imekuwa ikiendeshwa kitemi na kibaguzi.
Ilisemakana kuwa kuna wasanii wameifanya klabu hiyo kama yao huku wengine wakiwa hawatakiwi hata kukohoa jambo walilosema si sawasawa.
“Kwa mpasuko huu, wasanii waliochukizwa na Ray wamesema nao wao wanakazia hapahapa, Bongo Muvi lazima iangamie moja kwa moja, isiwepo tena,” alisema msanii mmoja ambaye jina lake linapanda kwa kasi.
KISINGIZIO CHA WASANII WANAFIKI CHAPINGWA
Maumivu makali zaidi yaliibuka kufuatia baadhi ya wasanii waliotaka kujifanya hawajapata meseji ya Ray ambapo walisema walishindwa kushiriki msiba huo kwa sababu walikuwa ‘shooting’.
“Kuna wasanii walishindwa kuweka wazi kwamba walipokea meseji ya katazo ya Ray, walipopigiwa simu na wenzao kuulizwa kwa nini hawaonekani msibani kwa Wema walisingizia eti wako location wanarekodi!
“Kwa akili za kawaida, mwenzenu kafiwa mnaweza kushikwa na ubize wa kurekodi filamu? Hawa ni wanafiki, walisingizia vile ili ionekane wana hudhuru,” alisema staa mwingine.
MAMA WEMA ASHTUSHWA
Akizungumza na waandishi wetu kwa mara ya kwanza baada ya kusikia mwanaye alisusiwa msiba wa baba yake, mama mzazi wa Wema, Mariam Sepetu alionesha kusikitishwa sana na kitendo hicho.
Alisema kitendo hicho kilitokea wakati ambao Wema au familia nzima ilikuwa inasaka faraja na si mfarakano kwa vile kufiwa kupo na hakuna dalili wala kujiandaa.
“Nilisikitika sana, lakini siwezi kusema mengi kwa sababu vijana wanataka mwongozo ili kwenda mbele, naamini watakaa na kuondoa tofauti zao,” alisema mama huyo mwenye mapenzi makubwa na mastaa wa filamu Bongo.
KATAZO LA RAY 
LILISIMAMIA HIVI

Habari kutoka chanzo chetu makini zilidai kuwa hoja dhaifu iliyotumiwa na Ray ni kwamba Wema huwa haendi kwenye misiba ya wenzake hivyo walitaka na yeye amzike baba yake mwenyewe.
MISIBA ILIYOTOLEWA MFANO
Ulitolewa mfano msiba wa aliyekuwa staa wa filamu za Bongo, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ aliyefariki dunia Januari 2, mwaka huu ambapo Wema alishindwa kufika kwa sababu alikuwa studio akirekodi wimbo wake mpya ambao haujatoka hadi leo.
MISIBA ALIYOSHIRIKI
Ilidaiwa kuwa Wema huwa hashiriki misiba ya wenzake, ikatolewa mifano misiba miwili aliyoshriki kuwa ni marehemu Sharo Milionea (Hussein Mkiety) na (Steven) Kanumba kwa sababu alikuwa mtu wake.
ANACHOSIMAMIA WEMA
Akizungumzia tukio la kususiwa msiba wa baba yake, Wema alifunguka:
“Nimesikitishwa na kitendo hicho naamini hakikuwa cha haki, mimi nimekuwa nikihudhuria misibani kwa watu mbalimbali na si kweli kwamba niko kivyangu, nimehukumiwa bure.”
RAY AINGIA ‘PANGONI’
Juzi Jumanne, Amani lilimsaka Ray kwa njia ya simu ili aelezee ukweli wa madai hayo lakini aliingia ‘pangoni’ (hakupokea simu).
Hata hivyo, katika gazeti ndugu la hili, Ijumaa la Ijumaa, Novemba Mosi, 2013 ukurasa wa mbele ambapo kuna habari yenye kichwa; WEMA SEPETU ASUSIWA MSIBA, Ray aliulizwa kuhusu madai hayo ambapo alijibu:
“Mh! Kweli Wema haendagi kwenye misiba ya watu, hata mimi sikumuona kwa Sajuki ingawa sijui kama alionekana baadaye ila kwa sasa niko sehemu mbaya nitakupigia baadaye tuongee kwa kirefu.”
Hakupiga.
MASTAA KIDUCHU MSIBANI
Pamoja na katazo hilo la Ray, wasanii wengine waliamua kwenda msibani Sinza – Mori (Dar) na wachache sana kwenye mazishi, Zanzibar.
Baadhi ya wasanii hao ni pamoja na Kajala Masanja, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’, Jacob Stephen ‘JB’, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’, Salum Mchoma ‘Chiki’, Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’ na Jacqueline Wolper.
WASIOFIKA MSIBANI 
Wengi walimsusia msiba Wema, lakini majina makubwa zaidi wakiongozwa na Ray mwenyewe ni Single Mtambalike ‘Richie’, Steven Mengele ‘Steve Nyerere’, Irene Paul, Blandina Chagula ‘Johari’, Ndumbangwe Misayo ‘Thea’ na Ruth Suka ‘Mainda’
Chanzo:GPL
-----------

HUYU NDIO MTANGAZAJI WA REDIO MWENYE USHAWISHI MKUBWA KULIKO WOTE TANZANIA

Millard Ayo

Jana tuliitisha kura za maoni Facebook na Twitter kutaka kufahamu kutoka kwa wasomaji wetu kuwa ni mtangazaji gani wa radio nchini mwenye ushawishi mkubwa na anayesikilizwa zaidi kuliko wengine.

Tanzania imeongea, na tunamtambulisha mtangazaji anayependwa zaidi, mwenye ushawishi kuliko wengine na ambaye kipindi chake husikilizwa zaidi, kuwa ni Millard Ayo aka ‘Mtu wa Nguvu’, wa Clouds FM.

Japo si kituo chake cha kwanza kuanza kazi, jina la Millard lilianza kufahamika nchini kupitia kipindi cha Milazo 101 cha Radio One. Sauti yake yenye mamlaka na ubunifu hewani, ulikifanya kipindi hicho kuwa maarufu kuliko vingine vya burudani katika radio hiyo inayomilikiwa na kampuni ya IPP.

Kuondoka kwake Radio One kulikuwa ni pigo kubwa lakini lenye neema kwa Clouds FM. Alihamia Clouds FM na kuanzisha kipindi kipya kiitwacho Amplifanya ambacho kilichukua nafasi ya kipindi cha nyimbo za kiafrika, Bambataa. Haikuchukua muda kipindi cha Amplifanya kikawa miongoni mwa vipindi bora kabisa Clouds FM. Kipindi hicho pia ni miongoni mwa vipindi vinavyoiingizia fedha nyingi redio hiyo na kumfanya Millard kuwa miongoni mwa watangazaji wa kituo hicho wanaolipwa mshahara mkubwa zaidi.

Leo hii Millard ni miongoni mwa watangazaji bora Tanzania na wanaosikilizwa zaidi. Si maarufu tu redioni bali pia ndiye mtangazaji wa Tanzania mwenye mashabiki wengi zaidi kwenye mitandao ya kijamii. Ana zaidi ya followers 67,000 kwenye Twitter huku Facebook akiwa na likes zaidi ya 145,530.

Umaarufu wake kwenye mitandao ya kijamii umemfanya ageuke brand na kuyavutia makampuni makubwa kama CRDB Bank, Fast Jet na mengine kudhamini kile anachotweet. Tweets zake tu zinamuingizia fedha huku akimiliki pia website yake binafsi yenye wasomaji lukuki na yenye matangazo mengi.

Kwa mshahara anaoupata, kazi ya uripota wa DSTV, ubalozi wa Fastjet, website yake, deal za voice-overs na mambo mengine, Millard anaingiza takriban ama zaidi ya shilingi milioni 10 kila mwezi.

Millard ni zaidi ya mtangazaji, bali ni mwandishi mwenye ‘pua ya habari’ (nose for news) huku akiongoza kwa kuja na angle za kipekee za habari zenye mvuto kwa watu (human interest stories) zinazokifanya kipindi chake cha Amplifaya kuteka matangazo ya jioni siku za wiki.

Pamoja na kupata mafanikio hayo, Millard ameendelea kuwa mchapakazi, simple, mtu anayejituma kutafuta habari hata sehemu za mbali kabisa, mcheshi na mtu wa watu.

Hakuna shaka kuwa, Millard ana mustakabali wa nguvu kwenye fani hiyo. Ni mfano wa kuigwa kwa watangazaji wengine na hazina kubwa kwa wazazi wake, Clouds Media Group na hata taifa kwa ujumla.
-Bongo5

Sunday, November 3, 2013

SLAA APONDA MFUMO MPYA WA UFAULU.

 
SIKU tatu baada ya serikali kutangaza mfumo mpya wa madaraja ya ufaulu, licha ya kupingwa na wengi, kitendo hicho pia kimemhuzunisha Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa.
Akizungumza na gazeti hili jana, Dk. Slaa alisema:  “Kwa kubadili mfumo wa maksi serikali sasa bila huruma imeamua kwa makusudi kabisa kuua ubora wa elimu nchini, ni kweli kwa kupanua wigo wa kufaulu serikali haitalaumiwa kwa akili ya kawaida, itaonekana  wamefaulu wote, lakini elimu haitawasaidia watoto wenyewe, haitawasaidia wazazi wenyewe,  na haitasaidia taifa letu. Tutapataje madaktari bora, tutapataje wanasayansi, walimu au wahandisi bora?  Mabadiliko yanahitajika kusaidia taifa hili lisizikwe na watu wasio na huruma.”
Kwa upande wake, Dk. George Kahangwa, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akizungumza kupitia kipindi cha ‘Tuongee’ kinachorushwa na Star TV,  alisema  hatua ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Profesa Sifuni Mchome, kutangaza mageuzi hayo ni kuonesha ni jinsi gani serikali  imeshindwa kutatua mzizi  wa tatizo la elimu nchini na baadala yake inatapatapa kwa kuja na sera iliyoiacha kuitumia toka mwaka 1995 iliyotumia alama hiyo ya 50 kwa 50  kwa Tanzania Bara na 40 kwa 60, kwa Visiwani Zanzibar ambapo safari hii imeamua kuitumia tena na kuiweka wazi.
Dk. Kahangwa alisema serikali licha ya kutoa tamko la kubadilisha daraja jipya huku ikikiri kuwa ilikuwa ikitoa alama za kuanzia 75 hadi 100 ndio ufaulu wa alama ‘A’ na daraja la kwanza, pasipo kuiweka wazi kwa muda mrefu, sasa wameamua kuiweka wazi, huku ni kuwaada Watanzania kwa kutumia sera ambayo hazitekelezeki.
“Hili ni janga la elimu, huko nyuma waliondoa ‘sifuri’ kwenye ufaulu na kuweka ‘feli’, leo hii wanakuja tena na kuongezea daraja la tano na kuita ‘ufaulu hafifu au ufaulu usioridhisha’, huku ni kucheza na masuala ya msingi katika taifa. Kuja mbele za umma na kutangaza tena juu ya sera hiyo waliyoiacha kwa muda pasipokuitumia ni jinsi gani sera hiyo haitekelezeki tena,” alisema Dk. Kahangwa.
Dk. Kahangwa amewaomba Watanzania na wadau wa habari nchini kujitokeza kuwahoji wadau wa elimu kama walishirikishwa kwenye kupitishwa kwa mabadiliko hayo.
Dk. Kahangwa alisema  hivi karibuni kuna shirika lilifanya utafiti wa shule za sekondari 100 ambapo shule nne tu ndizo zinahesabika kama shule bora huku 96 zikihesabika kama makambi ya shule.
Hata hivyo, Mhariri Mtendaji wa gazeti la Tanzania Daima, Ansbert Ngurumo, aliyekuwapo kwenye mahojiano hayo alifananisha kitendo cha serikali kupanga madaraja hayo kuwa ni sawa na kupanua magoli ya uwanja ili kila mchezaji afunge, huku akiitaka serikali iwaombe radhi wananchi kwa kuwa ilianza kutumia mfumo huo bila kuwaarifu.
Naye Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Mwanza, Edwin Soko, alisema mabadiliko haya yaliyolenga kuongeza idadi ya wahitimu bila kuangalia uzoefu, yamesababisha taifa kukosa falsafa na Dira ya Taifa.

PICHA ZA CHAFU ZA DENTI WA CHUO KIKUU CHA UDOM ZANASWA AKIWA NA PEDESHEE WAKIFANYA YAO

MDADA MWENYEWE NI HUYU. DENT mmoja katika Chuo Kikuu kimojawapo hapa nchini amepiga picha zisizo na maadili akiwa na njemba wake katika visiwa vya Zanzibar. Mwanafunzi huyo alionekana kutumia muda wa masomo kufanya mambo yake hayo, na kilichowashangaza wengi kile kitendo cha yeye kutoka DODOMA mpaka ZANZIBAR ili kutimiza haja zake katika kipindi ambacho wenzake walikuwa katika masomo..
DADA HUYO NA NJEMBA WAKE WAKIENDELEA KULA RAHA…..


HUDDAH ABARIKI PENZI JIPYA LA DIAMOND NA WEMA....AMPIGA VIJEMBE PENNY NA KUDAI KUWA WEMA NDIO DEMU SAHIHI WA DIAMOND KWA MAISHA.....!!


Mwanadada Huddah Monroe wa Kenya maarufu kama "The boss Lady wa Kenya" naye ameamua kufunguka yake ya moyoni kuhusu penzi linalotawala sana vyombo vya habari nchini- penzi la Diamond Platnumz na mwanadada Wema sepetu.
Leo kupitia ukurasa wa mtandao mmoja wa kijamii Huddah aliandika ujembe huu kwa Diamond huku akiweka picha ya mwanadada Wema Sepetu...
Too fresh @diamondplatnumz ,huyu Dame wako ,kipenzi chako.For life ,let nobody tell u otherwise.Hao wengine wapita njia tuu .God bless the two of u.RIP to her dad,I know how it feels to lose someone so dear to u.Take heart Ms Boss.I heart you!
Akimaanisha...
Huyu ndio msichana wako, kipenzi chako cha maisha. Usiruhusu mtu mwingine akwawambie vingine. Hao wengine wapita njia tuu. Mungu wabariki nyie wawili. Apumzike kwa amani baba yake. Najua ilivyo kumpoteza mtu wa karibu sana kwao. Kaza moyo Ms. Boss (Wema). Nakujali/nakupenda.

ROSE NDAUKA AAMUA KUMPUMZIKA KUIGIZA....ADAI KUCHOSHWA NA FILAMU ZA KIBONGO ZINAZOFANANA KARIBU ZOTE..!!!

Mwigizaji Rose Ndauka amesema kuwa anapumzika kwenye tasnia ya filamu kwa mwaka mmoja kwakuwa filamu za Tanzania zinafanana sana na anataka aje na kitu kipya na tofauti.


Kwa mujibu wa gazeti la mwanaspoti Rose Ndauka amesema wazo hilo limetokana na tatizo la kufanya kazi zinazojirudia mara kwa mara, hali iliyomfanya aamue kujipa likizo ya muda ili kujipanga.
Hata hivyo kauli hiyo inaweza kuwa na utata muigizaji huyo ni mjamzito kwa sasa na huenda hiyo ndio ikawa ni sababu kubwa ya yeye kusimama kwa muda.

MNYIKA AMSHUKIA RAIS KIKWETE

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amesema migogoro iliyojitokeza wakati wa Operesheni Tokomeza Majangili haiwezi kutenganishwa na agizo la Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete.
Mnyika alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akifungua mafunzo ya wajumbe na viongozi wa CHADEMA kutoka kata 35 kati ya 37 zinazounda Jimbo la Dodoma.
Alisema pamoja na baadhi ya wabunge wa CCM kumtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kagasheki na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi kuwajibika, Rais Kikwete hawezi kuachwa kando.
Alisisitiza kuwa Rais Kikwete asiwekwe kando kwani sababu kubwa ya mifugo ya wafugaji na wao wenyewe kuuawa, kumetokana na udhaifu wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), inayoongozwa na Rais Kikwete.
Mnyika alimtaka Rais Kikwete kutonyamaza bali atoe tamko kwanini Operesheni Tokomeza Ujangili imegeuka kuwa tokomeza mifugo na mauaji ya wafugaji.
“Pamoja na ukweli kuwa baadhi ya mawaziri wana udhahifu katika kusimamia operesheni hiyo, lakini Rais Kikwete naye anapaswa kujiuliza na kuwajibika kwanini yametokea hayo na yeye amekaa kimya hadi Bunge limefikia hatua ya kujadili jambo hili kwa uzito mkubwa?
“Haiwezekani Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa CCM na kiongozi wa nchi akanyamaza bila kutoa tamko, kwanini matukio hayo yametokea badala ya kupambana na majangili askari wanapambana na wafugaji na mifugo yao,” alisema.
Akiendelea kuzungumza na viongozi hao wa kata, Mnyika alisema CCM pamoja na serikali yake haina nia njema na wafugaji kwani kila kinachotendeka kina baraka ya serikali ya Rais Kikwete.
Aidha, alisema kuna kila sababu ya viongozi wa CHADEMA kuhakikisha wanasimamia vema mchakato wa rasimu ya Katiba mpya kwa kuhakikisha wanapiga kelele ili Katiba mpya iwe na kipengele cha kumruhusu Mtanzania kumiliki rasilimali ardhi.
Alisema haiwezekani Mtanzania asiwe na uhakika wa kumiliki ardhi, kwani kwa Katiba ya sasa ambayo ni mbovu inampa madaraka makubwa na ardhi yote ni mali ya Rais

Saturday, November 2, 2013

ALICHOKIANDIKA KIONGOZI WA KUNDI LA WAASI WA M23 KWENYE UKURASA WAKE WA FACEBOOK MUDA MFUPI ULIOPITA..!



Kwa muda mufupi sikupatikana kwenye mutandao wa facebook na kwenye simu, sababu nilikuwa mahali hakuna network, kwa sasa nimefika mahali kuna network, Mutaanza pata habari kwa wakati. hatukupigana, tulijitosha katika maeneo zetu bila kupigana, silaha zetu zote tulienda nazo hakuna yenye tuliaca. Ingelukuwa tulikimbiya hatugepata wakati ya kubeba bitu yetu. sasa mutu mwenye anayuwa fanya analyse, aifanye sasa. 1 kwa nini tilijitosha mumaeneo yetu bila kupigana? 2 Tulienda wapi? 3 Tutabakiya kwenye tulienda ama tutarundi, 3 Mbone FARDC haitufwate kwenye tuko? 4 kwa nini Kabila ameitika kuya zungumuza na japo kuwa alisha tushinda? Mwenye kicwa yake haitumike muzuri njo anaeza fanya fete eti M23 imeshindwa. Kwa marafiki, tuko tena tuko. Twasubiri kyenye kitatoka Kampala kwenye mazungumuzo, kama hakuna kizuri kinatoka huko. Na FARDC FDLR, NA MONUSCO inasubutu kuanza Vita tena, PALE MUTAJUWA SISI NI WANANI.

BREAKING NEWSSSSSSSSSS MATOKE YA DARASA LA SABA YAMETANGAZWA

Dar es salaam Tanzani Matoke ya Darasa la Saba yametangazwa hivi punde hivi punde na mwaka huu ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 30.72 mwaka jana mbaka asilimia 50.61 mwaka huu kutokana na wanafunzi walio fanya mtihani mwaka huu wa darasa la saba wamefaulu zaidi ukilinganisha na wanafunzi wa mwaka jana Kaimu mtendaji wa Baraza la Mtihani Charles Msonda amesema ufauru katika masomo yote umepanda kwa asilimia kati ya 6.01 na 28.06 ukilinganisha na mwaka 2012 Mwaka huu watainiwa wamefahulu zaidi katika somo la Kiswahilin kwa asilimia 69.06 na somo walilio faulu kwa kiwango kidogo zaidi ni somo la Hisabati wamefaulu kwa asilimia 28.62 Msonda amesema jumla ya watahiniwa 427,606 kati ya 844,938 walio fanya mtihani huo wamepata alama ya 100 kati ya alama ya 250 idadi hiyo nisawa na asilimia 50.61

PAMOJA NA UMAARUFU WA AY NDANI NA NJE YA NCHI HAJABADILIKA ANAONGEA NA KILA MTU POPOTE ALIPO

Hemdee Kiwanuka who is known for his contribution to AY’s international success, was in Dar es Salaam, August this year and he spoke about the CHOAMVA 2013 nominee exclusively to Bongo5.

Hemdee Kiwanuka

“He is the real deal,” Hemdee says as he describes AY. You don’t find too many artists like AY and I like that about him’ We have remained friends for a while; I worked with him back in the days when I brought him to Uganda to perform in Uganda for the first time. I saw the dude when I brought him out there and he was mad humble. Since then, he never changes bro. The dude is still the same. Most artists on his level would be walking like they are walking on water. But this dude speaks to everybody on the street man.

That time when me and him were talking, we had a translator because AY was not speaking English at that time but because of his determination, man right now me and him talking like am talking to Kanye, his English is on fire. He has remained the same and because of that, I am continuing to help him to get him where he needs to go and he allows me to do so cause we trust each other. Sometimes we are in the studio and I will tell him change that, do this and he will change it. Other artists on his level will be like ‘Yoo this is what I do man, why are you telling me what to do’.

That dude (AY) has lots of collabo;s with people in America. We just waiting for videos to be done. He is coming to American very soon to record videos. He has one track with Tyga, Lamyia is on there too and then we have another one with Young Joc so we got some fire coming. The reason why we are doing that, is that we are trying to show these Nigerians that East Africa is here! EA stand up. I represent East Africa so we gotta show them what we got.”

PICHA: LULU ATOA MSAADA WA FEDHA HOSPITALI YA OCEAN ROAD KWA WAGONJWA WA CANCER....


Mwanadada Elizabeth Michael ama LULU leo ametembelea hospitali ya Ocean Road Iliyopo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa zawadi za fedha kwa ajili ya wagonjwa wa cancer hospitalini hapo. kupitia ukurasa wake wa instagram LULU ameandika 
"Naamini Mimi sio mwema sana mpk Mungu akaniwezesha kuona mwezi huu nikiwa mzima na mwenye afya...!kwa kutambua Hilo nimeanza mwezi huu kwa kupita ktk hospital ya OCEAN ROAD na kutoa mchango ili kuwasaidia wagonjwa wa CANCER...!Tuwe na utaratibu wa kuwakumbuka wahitaji kwa chochote tulichonacho! Nawatakia mwezi wenye Baraka na mafanikio!..." Hongera sana lulu kwa moyo wako

PINDA, MAWAZIRI HATARINI KUNG'OLEWA

Waziri Mkuu Mizengo Pinda pamoja na mawaziri wake wawili; Khamisi Kagasheki (Maliasili na Utalii) na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, Dk Mathayo David wameingia matatani kutokana na shinikizo linalowataka wang’oke katika nafasi zao.

Pinda pamoja na mawaziri hao wanatakiwa kuachia ngazi kama hatua ya kuwajibika kutokana na matukio ya vifo na baadhi ya watu kujeruhiwa, katika matukio ya migogoro ya wakulima na wafugaji kwa upande mmoja na utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Majangili kwa upande mwingine.

Jana wabunge walicharuka na kuwataka mawaziri waliohusika katika Operesheni Tokomeza Ujangili wawajibishwe wakieleza kutoridhishwa na maelezo waliyoyatoa mapema jana, baada ya kipindi cha maswali na majibu.

Kelele za wabunge zilizuka baada ya wabunge kuanza kuchangia maelezo ya Serikali kuhusu migogoro ya wafugaji na wakulima, hifadhi za wawekezaji na maelezo ya Serikali kuhusu Operesheni Tokomeza Ujangili.

Aliyekuwa wa kwanza kuchangia mjadala huo ni Mbunge wa Kilolo, Profesa Peter Msola (CCM) ambaye katika hitimisho lake alitoa hoja ya kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza kile ambacho alikiita kuwa ni unyanyasaji wa wafugaji na uporaji wa mifugo yao.

Profesa Msola alielekeza shutuma zake kwa Serikali kuwa ilifanya operesheni zake kwa pupa bila kufanya maandalizi hivyo kuwaathiri wananchi wasiokuwa na hatia.

Spika wa Bunge, Anne Makinda kabla ya kuahirisha kikao cha Bunge jana mchana aliridhia kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kwa ajili ya kuchunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji, wakati ‘madudu’ ya Operesheni Tokomeza Majangili yatachunguzwa kupitia Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira.

Chimbuko la hoja

Jana asubuhi kabla ya Bunge kuanza kikao chake, Spika Makinda alitoa taarifa kwamba Kikao cha Kamati ya Uongozi kingekutana wakati kipindi cha maswali na majibu kikiendelea, kwa lengo la kutoa mwelekeo wa mjadala wa hoja za dharura.

Hoja hizo ni zile zilizotolewa na wabunge wawili kwa nyakati tofauti; Alphaxard Kangi Lugora wa Mwibara (CCM) kuhusu Operesheni Tokomeza Majangili na Saidi Nkumba wa Sikonge (CCM), kuhusu vita baina ya wakulima na wafugaji.

Kamati hiyo ilikutana baada ya kipindi cha maswali na majibu na Spika Makinda alitoa taarifa za kusitisha shughuli nyingine, ili wabunge waweze kujadili masuala hayo ambako kabla ya kuanza mjadala aliwaita mawaziri kutoa taarifa zao.

Alianza Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Kagasheki ambaye katika maelezo yake alihitimisha kwa kutangaza kusitisha Operesheni Tokomeza ili kupitia mpango huo na kufanya maboresho ili kuondoa upungufu uliopo.


Licha ya kueleza sababu nyingi zilizofanya Serikali kuendesha operesheni hiyo, alisema ina manufaa makubwa katika kuokoa wanyama aina ya tembo, lakini waziri alihitimisha kwa kusema itakuwa ni busara kuifanyia tathmini wakati ikiendelea, hivyo kutangaza kuisitisha mara moja.

Kwa upande wake Dk Mathayo alitoa maneno ya kuomba radhi na kuwapa pole watu waliopatwa na usumbufu ikiwa ni pamoja na kupoteza mali zao na mifugo.

Mathayo aliwaeleza wabunge kuwa Serikali imepanga kujenga malambo katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia wafugaji kupata maji ili kupunguza safari za kuhamahama kutoka eneo moja kwenda jingine.

Shinikizo kwa Pinda

Baada ya kumaliza hotuba zao, wabunge kadhaa walipata nafasi ya kuchangia maelezo hayo huku wengi wakielekeza shutuma zao kwa mawaziri hao na wenzao wa Mambo ya Ndani ya Nchi na yule wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Wabunge wawili wa Chadema, Paulina Gekul (Viti Maalumu) na John Shibuda (Maswa Mashariki) walitaka Waziri Mkuu Pinda ajiuzulu kutokana kushindwa kwake kudhibiti mauaji na mateso kwa wananchi.

Gekul alisema kinachotokea sasa ni utekelezaji wa kauli ya Pinda aliyoitoa bungeni akisema wahalifu wapigwe tu pamoja na ile ya Kagasheki aliyoitoa mjini Arusha akisema majangili watakaokamatwa wamalizwe hukohuko kwenye hifadhi.

Mbunge huyo alieleza operesheni hiyo kwamba imesababisha mauaji ya watu wasio na hatia ikiwemo mama Emiliana ambaye alifuatwa akiuza nyanya, lakini akateswa hadi kufa na hadi sasa mwili wake bado uko katika Hospitali ya Babati baada ya wananchi kugoma kuuzika.

Shibuda kwa upande wake alisema Pinda anapaswa kufungua milango kwa mawaziri wanaotakiwa kujiuzulu haraka, kutokana na kulea uzembe ambao umesababisha madhara makubwa kwa wafugaji.

Shibuda alisema kuwa Wizara ya Mifugo imekuwa na mtazamo hasi lakini akasisitiza kuwa uzembe wa viongozi wa ngazi za mikoa, wilaya hadi vijiji unatokana na ukimya wa Pinda ambaye anashindwa kuchukua hatua yoyote dhidi yao.

Wabunge wengine

Kwa upande wake Nkumba aliunga mkono kuundwa kwa kamati teule, lakini akasisitiza kuwa mawaziri hao wanne wana hoja za kujibu ndani ya chama tawala CCM na kwa Rais, vinginevyo Serikali haipaswi kuendeshwa na viongozi wazembe

BAADA YA NICK WA PILI KUMALIZA MASTER DEGREE MLIMANI HUU NDIO USHAURI ALIO TOKA KWA WANAMUZI

 
Rapper wa kampuni ya Weusi, Nick wa Pili amefanikiwa kuhitimu shahada yake ya pili kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam, UDSM.

Nick aliitoa taarifa hiyo kwenye kipindi cha Club 10 cha Clouds FM na kutoa ushauri kwa wanafunzi wanaofanya muziki.

“Mimi ni mwanafunzi, jana nimemaliza degree ya pili mlimani. Nimefurahi kuna wanafunzi wanataka kuwa kama mimi,kuna vitu vichache vya msingi vya kuzingatia kwa upande wa sanaa. Inabidi waache mambo mengi ya sanaa wachague kitu kimoja, atake kuwa msanii bora. Ukitaka kuwa msanii bora usihangaikie mambo ya kwenda studio, sijui kumtafuta nani ,sijui kutafuta interview, atake kuwa msanii bora hayo mambo mengine yatakufuata,” alisema Nick.

“Ukitaka kufanikiwa kitaaluma, njia moja ni kusoma lakini kusoma vipi,sio kusoma unasubiri kufika form 4 ndio unaanza kusoma au umefika form 6 ndio unaanza kusoma. Mwanafunzi bora ni yule anayesoma kila siku na unatakiwa kusoma kila siku. Soma kidogo, elimu sio ngumu, tatizo wanafunzi wanafeli katika mipango. Soma kidogo tambua masomo yako, tambua topic zako.Kila somo tambua topic ngapi, angalia muda wangu mwaka huu ilitakiwa nisome moja mbili tatu,nne ,tano jee nimefika? au unajipima. Pili ni kusoma kidogo hata ikawa ni kwa masaa mawili kila siku yanatosha kabisa.”

Hivi karibuni Nick wa Pili alipata shavu la kuwa miongoni mwa wazungumzaji wakuu kwenye semina za fursa kwenye mikoa zaidi ya 13

BAADA YA NICK WA PILI KUMALIZA MASTER DEGREE MLIMANI HUU NDIO USHAURI ALIO TOKA KWA WANAMUZI

 
Rapper wa kampuni ya Weusi, Nick wa Pili amefanikiwa kuhitimu shahada yake ya pili kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam, UDSM.

Nick aliitoa taarifa hiyo kwenye kipindi cha Club 10 cha Clouds FM na kutoa ushauri kwa wanafunzi wanaofanya muziki.

“Mimi ni mwanafunzi, jana nimemaliza degree ya pili mlimani. Nimefurahi kuna wanafunzi wanataka kuwa kama mimi,kuna vitu vichache vya msingi vya kuzingatia kwa upande wa sanaa. Inabidi waache mambo mengi ya sanaa wachague kitu kimoja, atake kuwa msanii bora. Ukitaka kuwa msanii bora usihangaikie mambo ya kwenda studio, sijui kumtafuta nani ,sijui kutafuta interview, atake kuwa msanii bora hayo mambo mengine yatakufuata,” alisema Nick.

“Ukitaka kufanikiwa kitaaluma, njia moja ni kusoma lakini kusoma vipi,sio kusoma unasubiri kufika form 4 ndio unaanza kusoma au umefika form 6 ndio unaanza kusoma. Mwanafunzi bora ni yule anayesoma kila siku na unatakiwa kusoma kila siku. Soma kidogo, elimu sio ngumu, tatizo wanafunzi wanafeli katika mipango. Soma kidogo tambua masomo yako, tambua topic zako.Kila somo tambua topic ngapi, angalia muda wangu mwaka huu ilitakiwa nisome moja mbili tatu,nne ,tano jee nimefika? au unajipima. Pili ni kusoma kidogo hata ikawa ni kwa masaa mawili kila siku yanatosha kabisa.”

Hivi karibuni Nick wa Pili alipata shavu la kuwa miongoni mwa wazungumzaji wakuu kwenye semina za fursa kwenye mikoa zaidi ya 13

BAADA YA NICK WA PILI KUMALIZA MASTER DEGREE MLIMANI HUU NDIO USHAURI ALIO TOKA KWA WANAMUZI

 
Rapper wa kampuni ya Weusi, Nick wa Pili amefanikiwa kuhitimu shahada yake ya pili kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam, UDSM.

Nick aliitoa taarifa hiyo kwenye kipindi cha Club 10 cha Clouds FM na kutoa ushauri kwa wanafunzi wanaofanya muziki.

“Mimi ni mwanafunzi, jana nimemaliza degree ya pili mlimani. Nimefurahi kuna wanafunzi wanataka kuwa kama mimi,kuna vitu vichache vya msingi vya kuzingatia kwa upande wa sanaa. Inabidi waache mambo mengi ya sanaa wachague kitu kimoja, atake kuwa msanii bora. Ukitaka kuwa msanii bora usihangaikie mambo ya kwenda studio, sijui kumtafuta nani ,sijui kutafuta interview, atake kuwa msanii bora hayo mambo mengine yatakufuata,” alisema Nick.

“Ukitaka kufanikiwa kitaaluma, njia moja ni kusoma lakini kusoma vipi,sio kusoma unasubiri kufika form 4 ndio unaanza kusoma au umefika form 6 ndio unaanza kusoma. Mwanafunzi bora ni yule anayesoma kila siku na unatakiwa kusoma kila siku. Soma kidogo, elimu sio ngumu, tatizo wanafunzi wanafeli katika mipango. Soma kidogo tambua masomo yako, tambua topic zako.Kila somo tambua topic ngapi, angalia muda wangu mwaka huu ilitakiwa nisome moja mbili tatu,nne ,tano jee nimefika? au unajipima. Pili ni kusoma kidogo hata ikawa ni kwa masaa mawili kila siku yanatosha kabisa.”

Hivi karibuni Nick wa Pili alipata shavu la kuwa miongoni mwa wazungumzaji wakuu kwenye semina za fursa kwenye mikoa zaidi ya 13

DIAMOND NUSURA AKAMATWE NA MAOFISA WA USALAMA WA TAIFA BAADA YA KUUTIBUA MSAFARA WA RAIS...

STAA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond.

STAA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Alhamisi iliyopita alijikuta akiutibua msafara wa Rais wa Zanzibar, Dk. Mohamed Shein kufuatia kuondoka kwenye msiba wakati ilitangazwa kiongozi huyo ndiye aliyetakiwa kuanza kuondoka.
Ishu hiyo iliyotafsiriwa kama jeuri ya staa huyo ilitokea Mbuzini Mjini Magharibi, Zanzibar baada ya kumalizika kwa mazishi ya baba wa Wema Sepetu, aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania Urusi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na Waziri wa Elimu wa zamani katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, marehemu Isaac Abraham Sepetu.
 
DIAMOND AINGIA
Awali, wakati waombolezaji wamekaa wakiusubiri mwili wa marehemu ufike, ghafla Diamond aliibuka akisindikizwa na kundi la wapambe mpaka alipokaa.
                                                     AWEKWA MSTARI WA MBELE
Diamond alipofika aliwekwa mstari wa mbele ambako walikaa ndugu wa karibu na watoto wote wa marehemu.
 
MC ATANGAZA ITIFAKI YA SERIKALI
Mwili ulipowasili, ratiba ya mazishi ikatangazwa na MC ambapo alitaja utaratibu wa mazishi mpaka watu watakaotakiwa kuweka mashada ya maua kaburini, akiwemo Rais Shein.
Baada ya mazishi, Mwongoza Shughuli ambaye jina halikujulikana aliwaomba watu wote wazingatie itifaki ya usalama wa taifa kwamba ni lazima viongozi wote wa serikali waondoke ndipo waombolezaji wengine watawanyike.
“Jamani naomba sana itifaki izingatiwe, asiondoke mtu yeyote kabla ya viongozi wetu wa serikali, akiwemo Rais Shein hawajaondoka,” alisema MC huyo.
 
DIAMOND APUUZA, ANYANYUKA
Baada ya MC huyo kutoa mwongozo, watu wote walitulia wakisubiri kiongozi wa kwanza kuondoka ambaye alikuwa ni Rais Shein kama itifaki ilivyotaka.
Lakini kabla Rais Shein hajaanza kusimama, Diamond alinyanyuka na kuzua kasheshe kwa sababu baadhi ya watu, hasa wa umri wake walianza kumkimbilia huku wakikanyagana na kusababisha hali ya taharuki.
 
MC AWATULIZA WATU
Baada ya watu kuanza kukimbizana hovyo muongozaji wa msiba huo aliwaomba watulie na kusema kuwa wasiogope ila kuna staa ambaye anapita ndiyo maana watu wamemkimbilia.
“Naomba utulivu huyo ni staa f’lani kapita huko ndiyo maana watu wanamkimbilia hivyo tulieni kwanza viongozi wetu waondoke,” alisema.

USALAMA WA TAIFA NUSURA WAMKAMATE
Baada ya kuona watu wakikimbia hovyo baadhi ya maofisa wa usalama wa taifa walitaka kumkamata msanii huyo wakisema alisimama kwa makusudi licha ya kusikia tangazo la kiitifaki.
 
WATU WAMSHANGAA DIAMOMD
Baadhi ya watu waliohudhuria msiba huo walionekana kushangazwa na kitendo cha Diamond na kusema kuwa ni vyema angesubiri viongozi wote waondoke ndipo na yeye atimke lakini kufanya vile si sahihi.
“Huyu Diamond kwani ana nini? Nakumbuka kwenye msiba wa Kanumba kule Dar pia aliingia kipindi ambacho ilitangazwa kuna kiongozi anakwenda, utaratibu ukatibuka, watu wakawa wanamshangilia yeye,” alisema mtu mmoja aliyetoka Dar kwenda

ALAMA MPYA ZA UFAULU MASHULENI ZAPINGWA

 
SIKU moja baada ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kufanya marekebisho katika upangaji wa viwango vya alama za matokeo ya wanafunzi wa kidato cha nne na sita kwa kufutwa daraja sifuri na kuwekwa daraja la tano, wadau na wasomi wameponda mfumo huo.

Wakizungumza na gazeti hili, wadau hao walisema kuwa tatizo si kushuka kwa kiwango cha ufaulu, bali uwepo wa elimu bora nchini.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally, alisema kuna mifumo miwili ya elimu nchini inayotumika, ambayo ni ule wa watu masikini na wenye nafuu ya maisha.

Alisema hali hiyo inaanzia chekechea hadi vyuo vikuu, huku akihoji wizara husika mfumo wa aina hiyo unamlenga nani, kwamba tatizo lililopo ni ubora wa elimu hasa katika shule za umma.

Bashiru alisema kwenye mifumo hiyo inayotumika, ule wa masikini upo kwenye shule nyingi za umma ambako ndiko kwenye watoto wengi wanaofeli kutokana na kukosa vifaa vya kufundishia, maabara na walimu.

“Katika shule za umma watoto wengi hawasomi, hawana maabara, sasa wizara inawatahini nini? Mageuzi yoyote ambayo yatashindwa kuondoa matabaka hayawezi kuleta elimu tunayoitaka,” alisema.

Alisema ubora wa elimu utawahusu wanafunzi hao wanaosoma shule za michepuo ya Kiingereza, kwani ndio watakaokuwa wanafaulu kwa kuwa shule zao zina mfumo mzuri unaoeleweka na viwango walivyojiwekea kama mwanafunzi hatafikia atarudia darasa ama kuachishwa shule.

Naye mhadhiri mwingine wa chuo hicho, Prof. Herme Mosha, alisema kama wizara inataka kuongeza idadi ya watu katika ufaulu waliofanya mtihani, inapaswa kuboresha elimu.

“Sio mara ya kwanza tumechezea vigezo, 2007 tulibadilisha viwango tulivyokuwa navyo tukaweka alama za chini, wanafunzi wengi wakachaguliwa, matokeo yake mtihani wa mwisho wa kidato cha nne kukawa na matokeo mabaya,” alisema.

Alisema lililofanyika sio utatuzi wa tatizo, bali wizara iangalie nini kinasababisha ubora wa elimu kushuka.

Kwa mujibu wa Prof. Mosha, wizara husika iangalie ni nini kinachowafanya wanafunzi wasisome badala ya kupandisha viwango kwa aina hiyo waliyoitumia.

Dk. Kitila Mkumbo wa Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema tatizo lililopo ni mfumo mbaya wa ufundishaji, kwani kupanga madaraja kwa aina hiyo si suluhu ya kutatua changamoto iliyopo.

Alisisitiza kuwa kwa staili hiyo, serikali haitoi tatizo bali inajaribu kuficha tatizo, hivyo hakuna cha kushangilia kwa mfumo huo walioutangaza.

Mwalimu wa sekondari, Josephat Ammy, alieleza kuwa mfumo huo utamfanya mwanafunzi kubweteka na kutochukulia umuhimu suala la elimu kwa kudhani kuwa uwezo wa kufaulu anao.

“Wao walitakiwa waje na suluhisho la elimu na kujua kwanini wanafunzi wanafeli, sasa wanachofanya nini? Wanaondoa daraja ziro halafu hao wa daraja la tano wanakwenda wapi?” alihoji.

Naye mmiliki wa shule za Green Acres, Julian Bujugo, alisema kuwa mfumo huo sio mbaya kwani wanafunzi watafanya mtihani kwa kutumia mitaala.

“Mfumo huu ulikuwepo hapo awali kabla ya kutolewa, sioni kama una ubaya. Ni mzuri, utasaidia kwa wanafunzi tofauti na mwaka jana walitunga mitihani ambayo haikuwa kwenye mitaala,” alisema.

Naye Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gracian Mukoba, alisema kuwa kubadilisha alama itakayowasaidia watoto wengi kuonekana wamefaulu haisaidii kwani ndiyo kwanza kunaongeza zao la ujinga.

Alisema kama walikuwa wanatafuta kufurahiwa na wazazi na wanafunzi, basi wangeweka alama A, B, C plus bila kuwa na alama hizo za daraja hadi la tano.

Kwa mujibu wa Mkoba, kilichofanyika ni siasa tu na kucheza na saikolojia za wazazi, ambazo tayari zimeathiriwa na mfumo mbaya wa elimu ambapo idadi kubwa ya watoto wanaofeli inaongezeka kila kukicha.

“Yaani hapa ni kama bomba, unakuta linatoa maji machafu ya tope. Baada ya kuangalia nini chanzo chake wewe unaamua kubadilisha koki na kuweka nyingine wakati si suluhisho,” alisema.

Mukoba alisema njia sahihi za kuboresha elimu serikali inazijua kwa kuwa tayari walishatumia fedha nyingi kwa ajili ya kuunda tume, kufanya utafiti, hivyo majibu tayari wanayo.

Naye mwalimu wa vituo vya elimu ya Taasisi ya Watu Wazima, Stanslaus Sekuru, alisema kuwa mfumo huo utaboresha elimu kwa sababu hapo awali wanafunzi walikuwa wakiumia sana.

Alitolea mfano daraja la nne akisema mwanafunzi anakuwa na alama 26, lakini akiwa na alama C tatu anashindwa kuendelea na kidato cha tano na mwenye daraja la tatu mwenye alama 25 na C tatu yeye anapewa nafasi ya kuendelea.

Mwalimu Charles Mkwidu ambaye ni mratibu wa Kituo cha Elimu ya Watu Wazima, alisema mpango huo ni mzuri ila uwekewe mkakati wa kuwasaidia wanafunzi kupenda kusoma, hasa masomo ya sayansi kwani wengi husoma wakati wa mitihani tu.

Naye mwanafunzi anayerudia mitihani, aliyeathiriwa na matokeo ya mwaka jana, Jesca Charles, alisema huenda ikawasaidia au la kwa kuwa mitaala ya elimu ndiyo iliyowaponza hadi wakafeli.